Tuesday, September 15

Kuna stori za baadhi ya Viongozi wa Africa kung’ang’ania kukaa madarakani hata baada ya vipindi vyao vya uongozi kuisha, pia wako ambao wanaendelea kuongoza kihalali kutokana na mabadiliko ambayo wameyafanya kwenye Katiba ili waendelee kuongoza !!
Siku chache zilizopita nilikusogezea stori kuhusu Rais mwenye umri mdogo kuliko wote Duniani, leo nakupa hii toka ndani ya Africa… unajua Marais wanaoongoza kwa kuwa na umri mkubwa? List niko nayo hapa mtu wangu, kila mmoja na picha yake kabisa !!
rais
1. Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe ana miaka 91, ndiye Rais mzee kuliko wote, ameshinda urais kwa muhula wa saba

tuni
2. Beji Caid Essebsi-Ana miaka 88, amekua Rais wa Tunisia tangu Desemba 31 2014
biya
3. Rais Paul Biya wa Cameroon ana miaka 82, ameingia madarakani tangu mwaka 1982
alge
4. AbdelAziz Boeteflika ni Rais wa Algeria toka April 1999, ana miaka 78
gine
5. Rais wa Guinea Alpha Conde ana miaka 77, amekua madarakani tangu December 2010
da
6. Rais wa visiwa vya Sao Tome, Manuel Pinto da Costa ana miaka 77, aliingia madarakani tangu mwaka 2011

lib
7. Rais wa Liberia Ellen Johnson Sirleaf ana miaka 76, aliingia madarakani tangu Januari 2006
muth
8. Rais wa Malawi, Peter Mutharika ana miaka 74, aliingia madarakani May 2014
ivoo
9. Rais wa Ivory Coast, Alassane Ouattara  ana miaka 73, aliingia madarakani tangu mwaka 2011
zzzzz
10. Rais wa Afrika Kusini, Jacob Zuma ana miaka 73, aliingia madarakani tangu May 9, 2009

0 comments:

-