Headlines za Siasa zinaendelea kubeba
uzito wa juu Tanzania, August 10 2015 Mgombea Urais anayewakilisha
UKAWA, Edward Ngoyai Lowassa amefika Ofisi za Tume ya Taifa ya Uchaguzi
NEC na kuchukua Fomu yake.
Pichaz za kwanza nilikusogezea msafara
uliotoka Makao Makuu wa CUF Buguruni Dar es Salaam, wwengine kwenye
maagari, wengine bodaboda.. wengine walifunga safari kwa miguu
kumsindikiza Mgombea huyo kutoka Buguruni mpaka Ofisi za NEC Posta alafu
safari ikaendelea tena mpaka Makao Makuu ya CHADEMA, Kindondoni Dar.
Ilionekana watu ni wengi sana, nafasi ya
eneo hilo haikutosha… ikabidi umati wote usogee Viwanja vya
BIAFRA ambapo Viongozi wa UKAWA walipata nafasi kuongea na Wanachama wao
walioshiriki mwanzo mpaka mwisho kwenye safari hiyo.