Baada
ya kuachia kisebusebu na noma ,Band ya muziki wa kizazi kipya inayotamba nchini
Ruby Band inajipanga kuachia video ya wimbo mpya kabla ya kumalizika kwa mfungo
wa mwezi mtukufu wa ramadhani na pia wanatarajia kuachia wimbo wao mpya
waliomshirikisha msanii mkubwa hapa nchini
ambaye wamemtambulisha kawa ‘’KING’.
Jina
hilo KING bado uongozi wa ruby band haujaweka wazi ni king yupi.lakini wengi
wamekuwa wakisema huenda vijana hao wamefanya colabo la hatari na ALIKIBA
ambaye kwa sasa ndiye anayejiita KINGKIBA.
Hata
hivyo mmliki wa band hiyo ruby yusuph maarufu kama Madam Ruby hajataka kuweka
wazi juu ya KING yupi kashirikishwa na vijana hawa.
‘’naomba
mashabiki wa ruby band wakae mkao wa kula tu,kazi nzuri ya vijana inakuja na
watu wajue tu ni ruby band featuring KING.Mengine watajua wimbo
ukishatoka,tunatarajia utatoka baada ya ramadhani ila video ya wimbo mwingine
tutaiachia hivi karibuni muda wowote kutoka sasa...alisema madam ruby.
RUBY
BAND ni band inayoundwa na vijana wanne ambao tangu waingie katika soko la
muziki wa Tanzania wamekuwa wakitoa changamoto kwa wasanii wa muziki wa band
wakiwa ni moja ya band chache zinazofanya vizuri katikamuziki wa bongo flavour.
Wimbo
wao wa kwanza unaitwa kisebusebu na wa pili unaitwa noma ambazo zote zina
video.pia wamekuwa wakitunga nyimbombalimbali zinazohamasisha masuala ya
kijamii kama ‘kitu kimojaúliokuwa unahimiza kupiga vita mauaji ya albino.
0 comments:
Post a Comment