Rapa
wa kike anayekuja kwa kasi katika industry ya muziki wa Tanzania chemical a.k.a
myself anayetamba na wimbo wake sielewi
ft soprano ameweka wazi kuwa yupo katika mahusiano ya kimapenzi na
boyfriend wake na siyo kama watu wengi wanavyomfikiria kutokana na muonekano na uvaaji wake wa kiume.
Msanii
huyo amesema taarifa za mitazamo mibaya iliyopo kwa baadhi ya watu kutokana na
muonekano wake na uvaaji wake wa nguo za kiume si za kweli na kwamba yeye ana boyfriend na anampenda ila
uvaaji wake unatokana na hassle zake tu na wakati mwingine analazimika hadi
kutembeakwa miguu katika mihangaiko yake.
Kuhusu
kazi zake na kujiingiza kufanya hiphop amesema
anavutiwa na kutamani sana kufanya kazi na msanii nguli wa hip hop hapa
bongo farid kubanda a.k.a fid q.
Chemical
ambaye kupitia wimbo wake wa sielewi ameweza kupata air time ya kutosha katika
vituo mbalimbali vya televisheni hapa nchini akiongea na kituo cha mlimani tv
amesema fid q ni rapa aliyemshawishi kuingia katika game ya muziki na tangu
akiwa mdogo amekuwa akiimba na kuchana ngoma za msanii huyo ikiwemo fid q.com
na nyinginezo.
Amesema
pia kuwa mafanikio yake yanatokana na management yake pamoja na saport ya
kutosha anayoipata kutoka kwa wazazi na ndugu zake bila kusahau mashabiki amabo
wamempokea kwa mikono miwili kama mmoja wa marapa wa kike.
Chemical
anakuwa moja ya wasanii wa kike wachache wanao rap akifuata nyendo za marapa
wengine kama chiku keto,rah p na wengine ambao hata hivyo harakati zao siyo
kubwa sana ukilinganisha na marapa wa kiuume.
Hata
hivyo ameahidi mashabiki wake kuendelea kukaza zaidi na kamwe hawezi kuacha
muziki.
0 comments:
Post a Comment