Tuesday, June 30


Indonesia
Kama uko karibu sana na TV za Kimataifa kama BBC, Sky News na CNN utagundua kwamba kwenye stori kubwa zilizopewa headlines sana iko ya Shambulio la Kugaidi lililotokea Tunisia na kusababisha mauaji ya Watalii.. Breaking News imeingia nayo kwenye stori kubwa zilizo kwenye headlines sasahivi, inahusu Ndege ya Kijeshi kuanguka kwenye makazi ya watu Indonesia na watu 30 wamefariki.
BBC Ajali II

Ndege hiyo ilipata ajali muda mfupi baada ya kuruka kutoka kwenye Uwanja wa Medan Polonia Airport.
. ndani ilikuwa imebeba jumla ya watu 12, ndege imeanguka kwenye mtaa ambao una makazi ya watu pamoja na Hoteli, gari moja pia limewaka moto baada ya kutokea ajali hiyo.. eneo lote la ajali limeshika moto.
BBC Ajali

Wenyeji wa eneo hilo wamesema hii ni mara ya pili kwa nyumba za eneo hilo kuangikuwa na ndege, iliwahi kuanguka Boeing 737 mwaka 2005 ikaua watu 143 na kati yao watu 30 walikuwa ni watu ambao wanaishi eneo hilo, hawakuwemo ndani ya ndege.
Map
Vikosi vya Zimamoto na Uokoaji vinaendelea na kazi ya kuzima moto pamoja na kutoa miili ya watu waliofariki kwenye ajali hiyo, huenda idadi ya waliofariki na majeruhi ikaongezeka wakati wowote kuanzia sasa.

0 comments:

-