Saturday, June 27


Malaika ,Msanii anayetamba kwa sasa  katika game ya muziki wa tanzania na wimbo wake wa SARE amesema hivi karibuni video ya wimbo wake huo unatarajiwa kuanza kuchezwa katika kituo kikubwa cha kimataifa cha runinga

 TRACE TV
 

Akizungumza na MLIMANI TV malaika amesema walitakiwa wawe wametuma kazi hiyo lakini kuna baadhi ya mambo ambayo uongozi wake unasubiri kuyakamilisha ili kuituma.

‘’Juzi tulitakiwa tupeleke trace lakini bado tulikuwa hatujakamilisha kwa sababu wale watu waliokuwa wametuandalia kwenye mfumo wa cd ilikuwa haijafika ukubwa wa kwenda kule(trace)kucheza,kwa hiyo kwenye hizi wiki hizi,nafikiri management yangu itasimamia ili kuweza kupeleka pia’’..alisema malaika

Ameongeza pia kuwa video ya sare imeshaanza kuchezwa katika vituo vya televisheni vya baadhi ya nchi za afrika ikiwemo bostwana.

Malaika anasema wasanii wa kike wa Tanzania wanaofanya vizuri ni moja ya mambo yanayomfanya kuendelea kukaza zaidi na hata kujitangaza kimataifa.

Mwanadada huyu alianza kupata umaarufu kupitia katika wimbo wa chege USWAZI TAKE AWAY na katika video ya wimbo huo na baadae akaja na wimbo wa MWANTUMU ambao ulimtambulisha vema kwa mashabiki kabla ya kuja na huu unaotamba sasa SARE.


0 comments:

-