Inapotokea
hali ya kutoelewana katika uhusiano ni mara chache sana wote wawili
kukubali kwamba uhusiano huo ufike mwisho, lakini mara nyingi mmoja yao
huwa hakubaliani kirahisi na uamuzi huo.
Mwanamke mmoja China, Azuha Kikuchi amekamatwa baada ya kumuua aliyekuwa mpenzi wake, Yuji Hirata ambaye walikuwa wanaishi jengo moja kwa kumchoma kisu kifuani.
Polisi wamefanya uchunguzi na kugundua Kikuchi alimpiga
mwanaume huyo kichwani na kumchoma na kisu kifuan ambapo mwili wake
ulikutwa ndani ya chumba chake ukiwa na majeraha na walipomfikisha
Hospitali alikuwa tayari amefariki.
Kikuchi alipohojiwa alikubali
kuhusika na tukio hilo na kuwaambia Polisi kuwa kulitokea hali ya
kutoelewana baada ya mpenzi wake kutaka kuvunja uhusiano wao.Ndani ya chumba hicho kulikutwa pia fimbo yenye wavu wa kuchezea tennis ukiwa na damu pamoja na kisu kilichokuwa kwenye begi ambavyo vilinunuliwa na Kikuchi siku chache kabla ya tukio hilo kutokea.
0 comments:
Post a Comment