Thursday, September 25

Siku mbili baada ya Amber Rose kufuata taratibu za kisheria akidai talaka kwa mumewe Wiz Khalifa, Nick Cannon ameendelea kunyoshewa vidole kuwa chanzo cha yote na kudaiwa kuchepuka na mrembo huyo kwa kipindi kirefu.
Chanzo kimeiambia TMZ kuwa Nick ambaye hivi sasa ni meneja wa Amber Rose amekanusha tuhuma hizo na kudai kuwa hajawahi kuchepuka na Amber na hahusiki kivyovyote na uamuzi wake.
Ameeleza kuwa alikuja kufahamu Amber Rose alikuwa na matatizo ya kifamili kupitia mwanasheria wake wiki iliyopita. Nick anasema baada ya kufahamu hivyo wawili hao walianza kushare masimulizi ya kuacha na kuachana.
Vyanzo mbalimbali vinaeleza kuwa Wiz na Amber Rose, kila mmoja anamtuhumu mwenzake kwa michepuko.


Amber Rose, Wiz Khalifa na mtoto wao
Tangu taarifa hizo zilipoanza kusambaa, Amber Rose amekuwa akipost picha na jumbe za ajabu kwenye Instagram na Twitter akionesha mwili wake.
Kwa upande wa Wiz Khalifa amekuwa akitweet jumbe mbalimbali ikiwa ni pamoja na “Everyone deserves to be loved”.

Hayo yanajiri wakati ambapo Nick Cannon yuko kwenye wakati mgumu akisubiri uamuzi wa mkewe Mariah Carey kudai talaka kisheria au kurudisha ndoa yao ambayo hivi sasa iko vipande.

0 comments:

-