Kuhusu
elimu, nchi zote tatu za Afrika Mashariki zimechukua hatua mbalimbali muhimu
kuipatia lugha ya Kiswahili nafasi katika mifumo yao ya elimu. Katika hilo,
nchi ambayo imepata mafanikio makubwa, ikilinganishwa na zingine, ni Tanzania.
Pamoja na ukweli huo, kinyume na imani ya baadhi ya watu, mafanikio ya
Kiswahili katika elimu nchini humo hayakupatikana kwa urahisi.
Hili limeelezwa kwa muhtasari na BAKITA
(1999). Kufikia wakati wa kupatikana uhuru kutoka kwa mkoloni, lugha ya
Kiswahili ilikuwa imeibuka wazi kama lugha inayotumika na wengi, na ikateuliwa kuwa
lugha ya taifa mwaka 1964 na hatimaye ikateuliwa kuwa lugha rasmi pia. Mwaka wa
1967, iliamuliwa kuwa itakuwa lugha ya kufundishia elimu yote ya msingi, na
1970 ikaanza kutumiwa katika vyuo vya walimu wa shule za msingi.
Matarajio yalikuwa kwamba hatua hii
itapanuliwa na kujumuisha shule za upili na hatimaye vyuo vikuu. Lakini kufikia
mwaka 1984, serikali ilisema kuwa Kiingereza
kingeendelea kutumika. Wizara ya Elimu
na Utamaduni ilisema wazi tena mwaka 1995 kuwa Kiingereza kiendelee kutumika.
Licha ya Ripoti ya Tume ya Rais ya Elimu ya 1982 (Tume ya Makweta) kushauri
kuwa Kiswahili kiwe lugha ya kufundishia elimu ya juu nchini Tanzania (shule za
upili 1985 na vyuo vikuu 1992), hakuna lililofanyika hadi sasa.
Hii yote tukubali tukatae inatokana na ukweli
kuwa lugha ya Kiswahili bado inakuwa na haijakidhi viwango stahiki kuweza
kutumika katika mawasiliano kimataifa na ndiyo maana hata serikali ikaliona
hilo na kuona umuhimu wa kuzidi kuhimiza kuhusu kujifunza lugha ya kiingereza
katika shule za upili ili Kuhakikisha uthabiti, ubora na ufasaha katika
mawasiliano ya kimataifa na nikiri kuwa lugha ina nafasi muhimu sana.
Sambamba na hilo pia ndiyo maana hata waziri
mwenye dhamana na elimu nchini mheshimiwa Shukuru Kawambwa akafikia maamuzi
magumu ya kuanzisha mfumo wa mafunzo ya lugha ya kiingereza kwa wanafunzi wa
shule za msingi na upili nchini mwezi may mwaka huu kwa kushirikiana na
serikali ya uingereza BRITISH COUNCEL na shirika la VCO ambapo kwa pamoja
waliafikiana kushirikiana na serikali ya Tanzania katika kuhakikisha kuwa
wanafunzi na wananchi wote wanakuwa na uelewa na lugha hiyo ya kiingereza.
Wakati
wa uzinduzi huo mh.kawambwa alikiri wazi kuwa asimia 95 ya wanafunzi wa shule
za upili nchini hawajui lugha hii ya kiingereza na niseme kuwa sasa umefika
wakati wa kuacha mawazo mgando tuliyonayo wengi wetu na kuanza kujifunza lugha
hii ambayo naweza kukiri kuwa ni lugha ya dunia kwasasa ku
Na ndiyo maana sasa,MRADI WA VITABU KWA
WATOTO nao umeona haja pia ya kuunga mkono jitihada hizo ili kuweza kushindana
na si kushindana tu bali na kuleta ushindani katika Nyanja mbalimbali za
kidunia zitakazokua zikiandaliwa kwani lugha hii ya kiingereza ndiyo lugha kuu
ambayo hutumika katika kuwasiliana kimataifa.
Imefika wakatio sasa kwa kushirikiana na mradi
huu wa vitabu kwa watoto uwe mwanga katika kujifunza lugha ya kiingereza na
kuacha kasumba na lawama ambazo kiukweli hazina manufaa ya kiushindani katika
dunia ya sasa.Mradi huu wa vitabu kwa watoto ni mradi unaoendeshwa kwenye nchi
za Kenya,Tanzania,Ghana,Ethiopia na Uganda lengo kuu likiwa ni kukuza uelewa na
ufahamu wa lugha ya Kiingereza ncini na pia kuibua vipaji vipya vya uandishi wa
riwaya kwa watoto wa umri wa miaka 10-15 lengo likiwa ni kuwajengea msingi
mzuri tangu wakiwa wadogo.
Akizungumza na waandishi wa habari mapema leo
mkurugenzi mtendaji wa mradi wa vitabu kwa watoto Tanzania Bi.Pilli Dumea
amesema kuwa waliamua kuwa na mradi huo kwa lengo la kuungana na wizara ya
elimu nchini katika kuhakikisha kuwa wananchi hususani watoto wa Kitanzania wanakua
katika ufahamu wa lugha ya kiingereza ili kuweza kuleta na kukabiliana na
ushindani katika Nyanja za kimataifa ambapo kwa kipindi kirefu watanzania
wameshindwa kuwepo katika ushindani huo kwa sababu ya uelewa ama kutokujua
kabisa lugha zinazotumika kimataifa hususani kiingereza.
“zaidi ya asilimia 95 ya wanafunzi wa elimu
ya msingi,elimu ya upili na elimu ya juu hawafahamu lugha hii,ni jambo la
kushangaza kiukweli na inabidi kuchukua hatua sasa kuondokana na aibu hii kwani
kama mwanafunzi wa chuo kikuu hafahamu lugha hii na wakati mameisoma tokea
shule ya msingi si jambo zuri hata kidogo”alisema.
Mradi huo ambao unadhaminiwa na
kuendeshwa na mcanada Willium Boots
umekuwa ni mradi endelevuna mpaka kufikia sasa umekwisha waibua na kuwajengea
uwezo kama siyo mwanga katika vipaji vyo zaidi ya watanzania 50 na kwasas
wamezindua rasmi mashindano hayo kwa awamu ya sita nchini.
Lengo kubwa na la msingi kwa mradi huu ni
kuibua na kukuza vipaji kwa waandishi wa riwaya vilevile kuhakikisha kuwa elimu
ya Tanzania inakwenda na wakati uliopo kwa kuhakikisha kila mara wanachapa au
wanaandaa muswada wa vitabu vya hadithi na riwaya ili viweze kutumika nchini
kwa wanafunzi wa shule za msingi.
Bi Dumea anasema.”ni wakati sasa wa kuacha
kasumba tuliyokuwa nayo,tokea mimi nasoma mwaka 69[1969]hadi leo vitabu
vinavyotumika vya kujifunzia mashuleni ni vile vile jambo ambalo linapelekea
kwamba kutokuendana na maisha halisi ya wakati huu kwa watanzania.kwa kuliona
hilo tuna hakika kuwa miswada tutakayoipata katika mashindano haya itaondoa
changamoto hii inayoikabili Tanzania yetu na wanafunzi wa wakati huu”alimalizia.
Ni
jambo la kufurahisha na linalotia matumaini katika muelekeo wa elimu yetu nchini
na hili litafanikiwa tu endapo juhudi za ziada na ushirikiano wa kutosha katika
kuyatimiza haya ya taasisi hii ya vitabu kwa watoto.kwani hakika kwasasa watoto
wetu mashuleni watakuwa na mwanga na vitendea kazi ambavyo vitasaidia katika
vita hii ama jitihada hizi za serikali na wizara ya elimu katika kuhakikisha
kuwa elimu na ufahamu wa lugha ya kiingereza unakuwa mkubwa nchini kwetu na
kuwaandaa vijana na wasomi wetu kuingia na kuleta ushindani katika Nyanja ya
kimataifa na kuleta ubora zaidi wa elimu yetu.
Mbali na zawadi watakazopatiwa washindi wa
uandikaji wa miswada hiyo ya riwaya chini ya mradi huu,pia mradi huo kwa
kushirikiana na serikali na wizara husika huchapa miswada ile yenye ubora
unaolingana na masharti ya uandikaji na ushiriki wa mashindano hayo hutumika
katika mitaala ya elimu ya msingi kwa watoto wa shule za msingi nchini na
katika maktaba mbalimbali nchini.
“mfano mzuri ni washindi wa mashindano ya
raundi ya tano bwana Richard mabala aliyeshinda na muswada wa riwaya yake ya
run free na Israel Yona aliyeshinda na muswada aliokuwa akiuita tears from
lonely heart tayari tumeanza kushirikiana na kampuni ya kuchapa na muda sii
mrefu vitapatikana mashuleni na kwenye maktaba zetu na maktaba mbalimbali
nchini Tanzania.
Akijibu swali la changamoto wanazokumbana
nazo katiak kuhakikisha wanafikia malengo waliyojiwekea bi Dumea
anasema”changamoto yetu kubwa ni ufahamu mdogo wa lugha hii nchini hali
inayopelekea hata kukosekana kwa washiriki wa kutosha katika shindano hili
kwani wengi wao hushindwa kutokana na kipengele cha lugha ya kiingereza,jambo
hili ni kubwa sana kwetu sisi kwani ukilinganisha washiriki wa Kenya na
Tanzania,Kenya wamepiga hatua kwa kuwa na washiriki zaidi ya 500 japo wameanza
mashindano msimu huu na sisi[watanzania] hatufikii hata robo ya washiriki
wao”alisema
Mashindano hayo ambayo hufanyika kila mwaka
nchini,mshindi wa kwanza kwa msimu huu atapata million 17,wa pili milioni 14 na
mshindi wa tatu ataondoka na kitita cha shilingi milioni 9 za kitanzania.
Mfano
mwingine mzuri ni kwa msanii Ramsey wa Nigeria alipokuja Tanzania,alisema hivi
nanukuu “Nimetembea na kujifunza mengi wasanii wa Tanzania wengi tuna vipaji
vya hali ya juu katika uigizaji lakini inawezekana tatizo letu lipo katika soko
letu kwa kazi zetu, nimeongea na mwigizaji wa kimataifa kutoka nchini Ghana Van
Vicker amenishauri umuhimu wa wasanii wetu kujua Kiingereza ikiwezekana
kurekodi hata filamu itakayotumia lugha hiyo,”anasema Ramsey.
Naamini utakuwa umepata mwanga wa kutosha juu
ya umuhimu wa kushirikiana na mradi huu wa vitabu kwa watoto nchini,tuwape
ushirikiano wa kutosha vijana wa chuo mjitokeze kushiriki kwa wingi na wadau
wote pia tushiriki kwani shindano hili ni kwa watanzania wote na kwa kufanya
hivyo tutafanya jambo katika kuikomboa elimu yetu na kuwasaidia watoto na
wadogo zetu waliopo mashuleni.kwa leo nawekea nukta hapa.
KEVIN R.LAMECK.
+255
769 91 29 31
+255
654 61 33 26
0 comments:
Post a Comment