Thursday, October 17

                          
                         
Mtoto wa mwandishi na mtangazaji wa kituo cha ITV,Ufoo Saro,Alvis Anthery akitoa heshima za mwisho mbele ya jeneza la marehemu Bibi yake Anastazia Saro aliyezuikwa jana katika makaburi ya kanisa la Urara wilayani Hai.
                        
Umati wa waombolezaji waliojitikeza katika kuaga mwili wa marehemu Anastazia Saro aliyezikwa katika makaburi ya kanisa la Urara wilayani Hai.
                            
Msemaji wa familia ya Saro,Allelio Swai akitoa maelezo ya familia wakati wa ibada ya kumuombea marehemu Anastazia Saro.
                                
                               
                                
Jeneza lililobeba mwili wa marehemu Anastazia Saro likiwekwa kaburini.
                         
                        
Mkuu wa jimbo la Hai,Aminirabi Swai akiongoza ibada ya maziko katika makaburi ya kanisa hilo na kisha kuweka shada la maua katika kaburi la marehemu Anastazia Saro.
                     
mwakilishi wa serikali katika maziko ya marehemu Anastazia Saro ,mkuu wa wilaya ya Hai Novatus Makunga akiweka shada la Maua katika kaburi.
                                 
Mtoto Alvis Anthery akiweka shada la maua katika kaburi la Bibi yake marehemu Anastazia Saro.(picha na Dixon Busagaga)

Na Dixon Busagaga waglobu ya jamii Moshi

VILIO,simanzi na hali ya huzuni jana vimetawala kwa mamia ya wakazi wa kijiji cha Shari, Machame wilayani Hai waliojitokeza kuuaga mwili wa marehemu ,Anastazia Saro (56),mama mzazi wa Mwanadishi na Mtangazaji wa Kituo cha Televisheni cha ITV,Ufoo Saro.

Wakazi hao wakiwemo wale waliotoka maeneo mbalimbali ya miji ya Moshi,Arusha na Dar es Salaam baadhi yao walionekana wakiangua vilio huku wengine wakipoteza fahamu muda mfupi baada ya jeneza lililobeba mwili wa marehemu kuingizwa kanisani.

Hali ilikuwa ya Simanzi zaidi wakati wa kutoa heshima za mwisho kwa waombolezaji wakipita mbele ya jeneza ambapo ililazimika kuwepo na watu maalumu ambao walikuwa na jukumu la kutoa huduma ya kwanza kwa baadhi ya ndugu walioshindwa kujuzuia.

Hali kama hiyo ili rejea kwa mara nyingine tena pale msemaji wa familia Allelio Swai akitoa maelezo ya namna marehemu alivyo uawa na hali aliyokutwa nayo mara baada ya kufanyiwa uchunguzi na madaktari.

Akitoa maelezo ya wasifu wa marehemu aliyefanyiwa ibada ya mazishi katika Kanisa la Urara lililopo chini ya Jimbo la Hai la Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT),Swai alisema marehemu Anastazia Saro alifikwa na mauti hayo baada ya kupigwa risasi na mkwewe Anthery Mushi ambaye alikwenda nyumbani kwa mama huyo eneo la Kibamba CCM,nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam.

Alisema taarifa ya madaktari katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), inaonyesha,Anastazia Saro alifariki dunia baada ya kushambuliwa kwa risasi tano katika mwili wake.

Swai aliomba kufanyika maombi kwa ajili ya Ufoo aliyelazwa katika hosptali ya Muhimbili ambako anapatiwa matibabu baada ya kufanyiwa upasuaji mkubwa hali iliyolazimu madaktari kumpa muda mrefu wa mapumziko.

“ Ufoo taarifa ya madaktari inaonesha alichanika utumbo mkubwa na kiasi utumbo mdogo,lakini tunashukuru hali ya Ufoo inaendelea kuimarika ,lakini maombi yenu yanahitajika ili aweze kurejea katika hali yake ya zamani ,na aweze kulitumikia taifa kwa kuhabarisha “alisema Swai.

Kwa upande wake,baba mdogo wa Ufoo Saro, mzee Eshikaeli Saro, akizungumza katika ibada ya mazishi kanisani hapo,alisema familia na kanisa imepoteza mtu aliyekuwa kiungo muhimu kati ya jamii na kanisa.

“Mama alikuwa ndiye mpambaji wa madhabahu ya kanisa ,na alihakikisha kanisa linakuwa katika hali ya usafi kabla ya ibada na hata pale wanakwaya walipokuwa na mazoezi ya kutwa hapa kanisani alihakikisha wanapata chakula”alisema Saro.

Alitoa shukrani kwa Mwenyekiti wa makampuni ya IPP, Dk.Regnald Mengi,mkurugenzi mtendaji wa ITV na Redio One, Joyce Mhavile pamoja na wafanyakazi wote wa makampuni hayo kwa kuifanya familia hiyo iweze kumfikisha marehemu Machame na kuzikwa.

Marehemu Anastazia Saro, aliuawa baada ya mkwewe kufika nyumbani kwake Kibamba CCM akiwa na mzazi mwenzie Ufoo kwa lengo la kusuluhishwa kile kinachodaiwa ni ugomvi uliokuwa ukifukuta kati ya wawili hao.

Tukio hilo lilitokea alfajiri ya Jumapili ya Oktoba 13 mwaka huu, huku mwanae Ufoo Saro ambaye ni Mwandishi na Mtangazaji wa ITV, akijeruhiwa vibaya kwa risasi mbili baada ya kutokea ugomvi kati yakena mzazi mwenzie Anthery Mushi ambaye hata hivyo na yeye alijiua kwa kujipiga risasi baada ya tukio hilo.

0 comments:

-