|  | 
Assalam
 alaikum mpenzi msomaji wangu wa safu hii. Mambo vipi? Natumani kwamba 
muwazima kabisa na mnaendelea vyema na majukumu yenu ya kila siku na naamini pia mtakuwa mmesherehekea eid vizuri zaidi. Mimi 
namshukuru Mungu kwani amekuwa akinipa nguvu ya kuandika haya 
ninayoamini yana manufaa kwenu.
Vivyo
 hivyo, amini tu kwamba mpenzi wako anakupenda kwa dhati licha ya kwamba
 hujaufungua moyo wake na kathibitisha kwamba ndani yake uko wewe peke 
yako.
Mpende,
 muamini na weka akilini mwako kwamba, kamwe hawezi kukusaliti licha ya 
kwamba kinyume chake pia ni sawa. Hiyo itakusaidia wewe kuendelea kuishi
 maisha ya furaha na amani bila kuwa na presha.
Jiulize,
 ni wanaume wangapi ambao wake zao wanagawa penzi nje ya ndoa lakini wao
 wanawaamini kupita maelezo? Ni wanawake wangapi ambao waume zao ni 
viwembe kwelikweli lakini wanawaamini kupindukia? Unadhani ni kwa nini? 
Ni kwa sababu wamejijengea mazingira ya kuwaamini wenzao wao wa kiwango 
kikubwa na kuziba masikio yao kukwepa wambeya.
Tutambue
 tu kwamba, katika maisha kuna kitu kuridhika. Unapokuwa na mtu ambaye 
anakupa kila aina ya furaha maishani mwako bila kuonesha tabia zozote 
zinazokutia mashaka juu ya penzi lake, huyo mpende, mheshimu na muamini.
Hata
 kama kuna uwezekano wa yeye kuwa anaficha makucha yake na kuyachomoa 
pale anapokuwa mbali na wewe, kwa sababu huna uhakika na hujawahi 
kumuona, chukulia kwamba yeye ni msafi kisha yaache maisha yenu 
yaendelee kuwepo.
Nasema
 hivyo kwa sababu, tukianza kuchunguzana hakuna ambaye ni msafi kwa 
asilimia mia moja. Kila mtu anajiamini mwenyewe lakini huwezi kuiamini 
nafsi ya mwenzako kwa asilimia zote.
Ndiyo
 maana nikasema, unapoingia katika uhusiano na mtu ambaye umetokea 
kumpenda sana, ongea na moyo wako. Moyo wako ndiyo utakueleza kama 
mpenzi wako ni muaminifu ama siyo na pindi utakapoona dalili za kwamba 
ni tapeli wa mapenzi mwenye lengo la kutaka kukuchezea kisha kukuacha 
solemba, usimng’ang’anie eti tu kwa sababu umeoza kwake, muache!
Tatizo
 tulilonalo wengi ni kutokuwa tayari kuwakosa wale ambao tumetokea 
kuwapenda sana bila kujua kwamba unaweza kutokea kumpenda mtu lakini 
yeye akawa hana mapenzi ya dhati moyoni mwake dhidi yako. Ifike wakati 
tukubaliane na uhalisia kwamba, unapoona uliyenaye anakuzingua, yupo 
mwingine mwenye penzi la dhati kwako ambaye anasubiri umuache huyo 
uliyenaye ili awekeze penzi lake kwako.
Kwa
 kumalizia naomba niseme kwamba, mapenzi ya siku hizi usipoangalia 
yanaweza kukufanya ukawa chizi. Hii ndiyo inayosababisha baadhi ya watu 
kufikia hatua ya kusema kwamba, hawahitaji kuwa na wapenzi katika maisha
 yao. Kwa nini? Kwa sababu kila uhusiano wanaoingia wanakutana na 
usanii.
Elewa
 kwamba, una haki ya kupenda na kupendwa, ukishampata yule unayedhani 
atayafanya maisha yako kuwa ya furaha, mpende kwa dhati na muamini 
kwamba hawezi kukusaliti lakini, wakati huo hutakiwi kubweteka, chunguza
 nyendo zake na kama utabaini kwamba anajiheshimu, ongeza mapenzi kwake 
lakini kama utabaini kuwa hajatulia, muache.
 RSS Feed
 RSS Feed Twitter
 Twitter October 17, 2013
October 17, 2013
 Unknown
Unknown







 
0 comments:
Post a Comment