Thursday, September 19

Mkurugenzi wa mafunzo (AJTC) mwenye koti jeupe akiwa pamoja na baadhi ya wakufunzi wa chuo hicho wakisikiliza kwa makini moja ya mada za ujasiriamali zilizotolewa chuoni hapo hivi karibuni
 
 
·     Jumla ya wanachuo 227 wa chuo cha uandishi wa habari na utangazaji Arusha wanatarajiwa kushiriki katika mafunzo ya ujasiriamali na mbinu za ukuzaji wa biashara, yatakayotolewa na wakufunzi wa chuo hich
Baadhi ya wakufunzi wa AJTC wakifuatilia kwa makini semina ya ujasiriamili  iliyokuwa ikiendelea chuoni hapo


Akizungumza na blog hii mratibu wa mafunzo hayo Bwana Andrea Ngobole amesema kuwa: mafunzo hayo yatakuwa ya  siku mbili kuanzia tarehe 19-20/09/2013na  yanalenga kuwapa wanachuo hao juu ya  mbinu na maarifa  kuwa wajasiriamali na wafanyaiashara wenye mafanikio na kuwa chachu ya maendeleo kwa familia, jamii na taifa kwa ujumla

·       Amesema kuwa kitengo cha ujasiriamali chuoni hapo kimekuwa kikiandaa semina za ujasiriamali kwa wanachuo hao kila mwaka na kwa mwaka huu kinatarajia kuwasilisha mada 7 kutoka kwa watoa mada wanne ambao pia ni wakufunzi wa chuo hicho.

·       Semina hii itajumuisha mada kama Business Ventures, Business Networking na Business Family zitakazo wasilishwa na Neema Mwaipela pia kutakuwa na mada ya kutathimini biashara na misingi 10 ya ujasiriamali itakayowasilishwa na Ngobole pia Cash Flow Quadrant itakayowasilishwa na Adson Kagiye. Alisema Bw. Ngobole.
Baadhi ya wanafunzi wa chuo cha uandishi wa habari arusha Ajtc wakifuatilia kwa makini moja ya semina za ujasiriamali zilizowahi kuendeshwa chuoni hapo
 

     Ngobole amesema semina hiyo itatanguliwa na mada ya ufunguzi wa semina hiyo itakayowasilishwa na mgeni rasmi Bwana Joseph Kagiye Mayagila ambaye pia ni Mkurugenzi Mtendaji wa mafunzo wa chuo cha uandishi wa habari na utangazaji Arusha ( AJTC )

·        Ameyataja madarasa yanayotarajiwa kushiriki katika semina hiyo kuwa   ni MKOMANZI, TANGANYIKA, SERENGETI, UDZUNGWA, RUWENZORI, KILIMANJARO, MANYARA, NYASA,  KITENGO CHA ELIMU NA KOMPYUTA. na madarasa yaliyopo likizo kama SELOUS, NATRON RUAHA yataandaliwa semina mara watakaporejea kutoka likizo mnamo october au november kulingana na ratiba itakayotolewa na idara ya taaluma chuoni hapo

Amesisitiza kuwa semina hiyo ni ya muhimu sana kwa kila mwanafunzi kuweza kuhudhuria mafunzo hayo kwani kitengo hicho kinapenda kila mwanachuo aweze kupata mafunzo hayo ambayomada zake zimepangwa ili kumpa mwanachuo maarifa ya ujasiriamli na kuwa mmiliki wa iashara yenye mafanikio kwake na jamii kwa ujumla 

0 comments:

-