Friday, January 22

Kenyatta  
Rais Kenyatta ameahidi kuwaandama walioshambulia kambi ya el-Adde
Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta anawatembelea wanajeshi waliojeruhiwa baada ya wanamgambo wa al-Shabab kushambulia kambi ya wanajeshi nchini Somalia Ijumaa iliyopita.
Rais Kenyatta atatembelea majeruhi hospitali ya Forces Memorial, Nairobi na baadaye kujumuika na jamaa, marafiki na maafisa wakuu wa jeshi kwa ibada ya kuwakumbuka wanajeshi waliouawa.
Majeshi Wanajeshi tayari wamekusanyika ndani ya hospitali hiyo ya majeshi
Serikali ya Kenya bado haijatoa idadi kamili ya wanajeshi wake waliouawa baada ya kambi hiyo iliyoko el-Ade kushambuliwa.
Kundi la al-Shabab awali lilisema liliwaua wanajeshi zaidi ya 60 wa Kenya.
Mamia ya jamaa na marafiki wamekuwa wakifika katika vituo vilivyotengwa na idara ya jeshi nchini Kenya kutafuta habari kuhusu wapendwa wao.
Mkuu wa jeshi Jenerali Samson Mwathethe aliambia wanahabari Alhamisi kwamba jeshi bado linaendelea kukusanya habari kuhusu wanajeshi waliokuwa kwenye kambi hiyo.
Majeshi  
Baadhi ya wanajeshi waliojeruhiwa wanatibiwa katika hospitali ya majeshi
Alidokeza pia kwamba huenda ikabidi uchunguzi wa vijinasaba kufanywa kutambua miili ya baadhi ya wanajeshi waliouawa.
Alisema bomu lililotumiwa na washambuliaji hao kuvamia kambi hiyo lilikuwa na nguvu mara tatu kushinda bomu lililotumiwa kushambulia ubalozi wa Marekani jijini Nairobi mwaka 1998.
Watu takriban 250 waliuawa kwenye shambulio hilo.

0 comments:

-