Tuesday, December 1


Kama uliipata stori ya Mamlaka ya Mapato TRA kunasa makontena tisa eneo la Tanki Bovu Mbezi Dar es Salaam, nina muendelezo wake mtu wangu kuhusu majibu ya TRA walivyonasa mzigo huo.
Hapa ni nukuu ya alichokisema Mkurugenzi wa Kitengo cha Elimu ya Walipa Kodi wa TRA >>> ‘Tulipata taarifa kutoka kwa watu kwamba kuna kontena zinahamishwa kutoka bandari kavu ya Vingunguti usiku wa manane kuja kwenye godown iliyopo eneo la Mbezi Tanki Bovu ambayo sio rasmi na haiko kwenye orodha ya bandari kavu zilizo kwenye uangalizi wa TRA‘>>- Mkurugenzi Richard Kayombo.
IMG-20151201-WA0015
Kwenye sentensi nyingine za Richard Kayombo >>> ‘Tumeshirikiana na Jeshi la Polisi kuhakikisha tunafika eneo hili na kuliweka chini ya ulinzi…. Hapa yapo makontena tisa, vilevile tumekuta magari matatu ambayo yalikuwa yanabeba haya makontena, madereva wake wako chini ya ulinzi.’
Baada ya hapo kilichofatia ni hiki >>> ‘Uchunguzi wetu tumemfahamu mwagizaji wa makontena pamoja na wakala wa forodha ambaye alikuwa anashughulikia makontena haya… Makontena yalipata kibali cha kupelekwa eneo la EPZ Ubungo September 17 2015, lakini kibali kimepita muda wake na cha kushangaza ni kwamba kontena hizi zimeletwa huku ambako sio mahali rasmi, ni kiashiria kwamba kuna jambo baya lilitaka kutokea kama ukwepaji wa kodi.’
IMG_20151201_131138
Sentensi za mwisho kwenye ufafanuzi huo hizi hapa >>> ‘Tutabaini kila kitu baada ya kupata nyaraka halisi na kuwapata mwagizaji na wakala wa forodha ambao wanatakiwa kujitokeza ndani ya saa 24… wasipojitokea tutafungua makontena kuangalia kilichomo, kama ni bidhaa halali tutazitaifisha, na kama ni bidhaa haramu zitateketezwa…‘ >>- Richard Kayombo.

0 comments:

-