Friday, August 7


Wanamitindo, Happiness Millen.
LILE tamasha la burudani lililokuwa likisubiriwa kwa hamu kubwa la Usiku wa Mastaa Temeke, linatarajiwa kufanyika kesho Jumamosi kwenye Uwanja wa Taifa wa Burudani, Dar Live uliopo Mbagala-Zakhiem jijini Dar es Salaam.

 Jokate Mwegelo ‘Kidoti’.
Tamasha hilo lina lengo la kuwazawadia mastaa mbalimbali wa hapa nchini ambao wametoa mchango mkubwa katika kuiwakilisha vema Wilaya ya Temeke na viunga vyake.

Mratibu wa tamasha hilo, Richard Yalomba amesema mbali na kutoa zawadi kwa mastaa hao, pia siku hiyo kutatawaliwa na burudani za kutosha kutoka Kundi la FM Academia na Isha Mashauzi ambazo zitaanza saa moja usiku mpaka majogoo.
Yalomba amewataja baadhi ya wale watakaopewa medali kama zawadi kutokana na mchango wao kuwa ni wanamitindo, Happiness Millen Magesse na Jokate Mwegelo ‘Kidoti’, mkongwe wa Bongo Fleva, Juma Nature, mkali wa Bongo Fleva, Banana Zorro na mkali kutoka TMK Wanaume Family, Chegge.
“Katika shoo hiyo, mashabiki wataingia ukumbini hapo kwa kiingilio cha shilingi elfu kumi tu huku wakishuhudia burudani zote zitakazofanyika humo ndani,” alisema Yalomba.

0 comments:

-