+255 682 105 366
Duniani kuna mambo mengi ya ajabu ambayo
umewahi au hujawahi kusikia. Gazeti hili linapanda milima na kushuka
mabondeni kisha kupaa angani kukuletea simulizi ya undani wa viumbe wa
ajabu waishio au waonekanao angani. Ungana nami katika simulizi hii.
Huko nyuma niliwahi kudokeza kwenye
gazeti tumbo moja na hili, Ijumaa Wikienda lakini sikuingia ndani ili
kupata ukweli juu ya viumbe hao wa ajabu waishio angani. Wanaitwa
Aliens. Wana muonekano kama binadamu isipokuwa hawafanani moja kwa moja
na binadamu. Viumbe hao waliogundulika karne kadhaa zilizopita,
wameshatengenezewa filamu nyingi na wasanii mbalimbali duniani
(tutazichambua huko mbele).
Aliens wapo wa rangi tofauti kama kijani, weupe, weusi, njano, zambarau na kila aina ya rangi.
Inaaminika kuwa, Aliens wanaoishi angani
wana akili nyingi kuliko binadamu. Wana mfumo wa kompyuta uitwao Alien
Software na wapo juu kiteknojia kuliko binadamu tatizo tuu hawavai nguo!
Tofauti na binadamu ambaye anafanya kazi kwa hatua moja kwenda
nyingine, Aliens wao hufanya mambo kinyume kabisa. Kwa mfano wakitaka
kusema ‘naomba maji’ husema ‘maji naomba’ yaani cha nyuma kinakwenda
mbele na cha mbele kinarudi nyuma. Kama tunavyowashangaa, nao pia
wanatushangaa na kutuona viumbe wa ajabu.
Wachambuzi wa mambo ya anga walishaandika ripoti nyingi kuhusu viumbe hao ambao huja duniani na kurudi angani.
Swali ni je, viumbe hao wanaishi katika
sayari gani? Wataalam hao wanalijibu swali hilo kwa kusema haijulikani
moja kwa moja wanaishi sayari gani lakini kwa uhakika siyo kwenye mwezi
(kumbuka mwezi siyo sayari).
Inawezekana bado hujaelewa simulizi hii.
Bermuda Triangle ni eneo la pembetatu la bahari lililopo kati ya nchi
tatu katika Bahari ya Atlantiki. Miaka kadhaa huko nyuma viumbe hao
waliwahi kutua eneo hilo na kuweka historia (nitaisimulia huko mbele).
Pia waliwahi kuonekana Kisiwa cha Bermuda, Pwani ya Mashariki mwa
Marekani, Kisiwa cha Puerto Rico kilichopo Kaskazini mwa Carrebian na
Fort Lauderdale huko Florida, Marekani.
Umewahi kusikia vitu mbalimbali duniani
vikisemekana vimepotea katika mazingira ya kutatanisha? Aliens
wanahusishwa na upoteaji wa meli baharini hasa za mizigo huku watu
wakiamini huwa zinazama lakini uchunguzi ukifanyika meli hizo huwa
hazionekani hata ndani ya maji baharini.
Aliens wanatajwa kuhusika na upotevu wa
watu duniani ikiaminika kuwa labda watu hao walikufa lakini ukweli ni
kwamba huchukuliwa na viumbe hao.
Ndege za kijeshi zimeripotiwa mara
nyingi kupotea au kutokuonekana milele katika eneo la Bermuda Triangle
ikieleza kuwa Aliens ndiyo wahusika wa upotevu huo.
Ujio wa Aliens katika eneo la Bermuda
Triangle ulisababisha kisiwa hicho kupata umaarufu duniani na kupewa
jina la Devil’s Sea (Bahari ya Shetani) ambapo binadamu wamekuwa
wakiamini au kujenga imani potofu kuwa shetani amekuwa na makazi katika
eneo hilo na kuwapoteza wasafiri wa majini. Wengine huhisi ni
ushirikina.
Wapo binadamu wanaoamini kuwa Aliens walikuwepo duniani tangu enzi hizo kabla ya binadamu na hawajaondoka.
Si sehemu hizo pekee lakini wamekuwa wakitua maeneo mbalimbali duniani na kuna baadhi ya serikali duniani zinawajua.
Wataalam wa anga wanadai Aliens wako mbali kimaendeleo na wanafanya wanavyotaka.
>> Je, hawa ni viumbe gani? Ndiyo kwanza simulizi imeanza. Usikose kufuatilia wiki ijayo
0 comments:
Post a Comment