Monday, July 27

1..
IMG_0062Mwenyekiti wa Taasisi ya kilimo (TASO), Engelbert Moyo (kushoto)akizungumza jambo, pamoja na  Meneja wa mawasiliano wa kampuni ya simu ya mkononi ya Tigo, John Wanyancha.

2.Wanahabari wakifuatilia mkutano huo.
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Jakaya Mrisho Kikwete anatarajia kuwa mgeni rasmi katika maonesho ya kimataifa ya sikukuu ya wakulima yajulikanayo kama Nanenane yatakayofanyika mkoani Lindi, Agosti Mosi mwaka huu.
Akizungumza na wanahabari leo jijini Dar es Salaam, Meneja wa mawasiliano wa kampuni ya simu ya mkononi ya  Tigo ambao pia ni wadhamini wa maonesho hayo, John Wanyancha amesema kuwa sikukuu ya maonesho ya wakulima  kutakuwa na huduma mbalimbali zitakazokuwa zikifanyika zikiwemo za kilimo.
Amesema kuwa mbali na huduma zitakazokuwa zikitolewa pia wananchi kutoka maeneo yanayozunguka Mkoa wa Lindi kama vile Mtwara wataweza kunufaika na  huduma zitakazokuwa zikifanywa na Tigo ambazo zinajulikana kama Tigo Kilimo, hivyo wananchi wajitokeze kwa wingi.
Naye Mwenyekiti wa Taasisi ya Kilimo (TASO), Engelbert Moyo amesema kuwa katika maonesho hayo wakulima wategemee kuona teknolijia mpya kama vile mbegu za kisasa pamoja na pembejeo hivyo maonesho hayo  yataweza kuwavutia wawekezaji katika nyanja mbalimbali kama vile; utalii, madini, mawasiliano pamoja na nyinginezo.
Maonesho hayo ni ya 22 tangu kuanzishwa kwake na yanatarajiwa kuhitimishwa Agosti 8, mwaka huu na Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Dk. Ali Mohammed  Shein.
 NA DENIS MTIMA/GPL

0 comments:

-