Kiongozi wa ''Mapinduzi'' kwa upande wake Meja Jenerali Godefroid Niyombare
19:00
Katibu mkuu wa umoja wa Mataifa Ban ki-Moon amewataka wahusika wakuu
nchini Burundi kuweka uhasama baina yao kando ilikulinda taifa
18:55 Mwandishi wa BBC aliyeko Dar es Salaam anasema kuwa ndege ya rais Nkurunzinza imepaa ikielekea Bujumbura 18:53 Kiongozi wa ''Mapinduzi'' kwa upande wake Meja Jenerali Godefroid Niyombare ametangaza kufungwa kwa mipaka 18:45 Mwandishi wa BBC huko Bujumbura Kazungu Lozy anasema watu wangali wanasheherekea 18:40 Rais Nkurunzinza ameingia ndani ya gari lake na kuondoka mjini Dar es Salaam akionesha dalili kuwa yuaelekea Burundi 18:37
Kiongozi wa ''Mapinduzi'' kwa upande wake Meja Jenerali Godefroid
Niyombare ameamrisha wanajeshi kuzuia rais Nkurunzinza kutua Burundi 18:30 Rais Pierre Nkurunziza anatarajiwa kuhutubia taifa baada ya kurejea kutoka Tanzania amesema msemaji wake Willy Nyamitwe. 18:25 Generali Niyombareh ametoa amri kwa majeshi kuungana na kulinda viwanja vya ndege kote nchini humo 18:20 Generali aliyeongoza
''Mapinduzi'' leo asubuhi amewataka maafisa wa jeshi na polisi kufanya
kazi kwa pamoja ilikulinda usalama wa nchi hiyo. 18:15 Viongozi wa kanda ya Afrika wametaka makundi hasimu kutulia na kukubali hali ya kikatiba Kurejea 18:10 Esipisu amesema kuwa rais Uhuru Kenyatta anaunga mkono kurejeshwa kwa utawala wa kikatiba 18:07 Msemaji wa rais wa Kenya Manoah Esipisu amesema kuwa viongozi wanataka hali ya kawaida irejee huko Burundi
Wananchi waendelea kusheherekea Bujumbura kufuatia tangazo la ''Mapinduzi''
18:06 Rais wa Tanzania amekashifu ''mapinduzi'' yaliyotoke leo huko Burundi 18:05 Rais amesema hayo katika mkutano wa upatanishi wa viongozi wa kanda ya Afrika Mashariki 18:01 Ujumbe wa mtandao wa facebook wa urais nchini Burundi umekanusha kutokea kwa ''Mapinduzi''. 18:01 Viongozi hao wanakutana dar es salaam kujaribu kutatua mzozo wa kisiasa unaoendelea nchini Burundi 18:01 Rais Jakaya Kikwete amesema hayo katika mkutano wa upatanishi wa viongozi wa kanda ya Afrika Mashariki 18:00 Rais wa Tanzania amekashifu ''mapinduzi'' yaliyotoke leo huko Burundi 17:55 Msemaji wa rais Nkurunzinza ameiambia BBC kuwa asilimia 95 ya taifa hilo ingali salama na wala hakuna tashwishi. 17:50 Manuari zaidi zaonekana barabarani mjini Bujumbura 17:45 Ujumbe wa mtandao wa facebook wa urais nchini Burundi umekanusha kutokea kwa ''Mapinduzi''. 17:30 Msemaji wa rais
Nkurunziza,Willy Nyamitwe ameiambia BBC kuwa rais huyo angali
madarakani na kuwa hajaondolewa madarakani 17:22 Redio ya taifa ya Burundi inasema kuwa rais Nkurunzinza angali Madarakani na kuwa hakujakuwa na ''mapinduzi'' 17:20 Maafisa wa jeshi wanaolinda kituo cha taifa cha redio wamewaonya watangazaji wasitangaze kuwa kuna ''mapinduzi'' 17:05
Mwandishi wa BBC aliyeko huko Ruth Nesoba anasema kuwa waandamanaji
wamefululiza hadi kwenye vituo vya polisi na magereza yaliyokuwa na
mahabusu waliokamata kwa kuandamana na kuwaachilia huru 17:00 Redio ya taifa inasema kuwa bado rais Nkurunzinza angali madarakani. 16:50 Kituo hicho cha redio cha ''African Public Radio'' kinapeperusha tangazo la kupinduliwa kwa serikali ya rais Nkurunzinza 16:40 Redio iliyokuwa imefungwa na serikali ya rais Nkurunzinza kwa kupeperusha habari za maandamano imefunguliwa upya. 16:30 Mwandishi wa BBC Cyriac Muhawenay aliyeko Bujumbura anasema raia wanaonekana kuwa na furaha. 16:20 Picha za raia wakiwa wamekwea vifaru vya kijeshi 16:08 Watu wanaonekana wakininginia kwenye vifaru vya jeshi 16:05 Afisi ya urais nchini Burundi imetangaza kwenye mtandao wake wa twitter kuwa ''hali ni Shwari'' 16:00 Majeshi wameonekana nje ya kambi za kijeshi mjini Bujumbura 15:58 Viongozi wa jeshi wamewaamrisha maafisa wa polisi kuondoka mabarabarani. 15:55 Mwandishi Sonia Rolley,
wa Radio France International anasema kuwa halaiki ya raia wamefika nje
ya kituo hicho wakishangilia matukio hayo 15:50 Waandamanaji wanasemekana kuambatana na wanajeshi kuelekea katikati ya mji mkuu wa Bujumbura 15:45
Rais Pierre Nkurunziza ambaye analaumiwa kugombea urais kwa muhula wa
tatu, anatarajiwa kuhudhuria mkutano huo, kusikiliza hoja za viongozi
wenzake. 15:40 Mwandishi wa BBC aliyeko Bujumbura Maud Julien anasema kuwa Miili ya watu watatu imeonekane katika barabara za Bujumbura 15:36 Viongozi wote wa kanda ya Afrika Mashariki na kati wako Dar es Salaam kwa mwaliko wa rais Kikwete. 15:35 Rais Nkurunzinza yuko
mjini Dar es Salaam Tanzania kuhudhuria mkutano wa kutafuta suluhu ya
mgogoro wa kisasa uliokuwa ukiendelea Burundi. 15:30 Maelfu ya
raia wa Burundi waandamana a mabarabarani mjini Bujumbura wakishangilia
tangazo hilo la ''kutomtambua'' rais Nkurunzinza. 15:20 Jenerali huyo
aliyetimuliwa na Nkurunziza mwezi februari anasema kuwa Nkurunziza
alishindwa kuheshimu mwafaka wa amani mbali na sheria za kimataifa. 15:10
Meja Generali Niyombareh amesema wamechukua hatua hiyo baada ya watu wa
Burundi kukataa kwa kinywa kipana awamu ya tatu ya urais wa Nkurunziza. 15:05 Jenerali Niyombareh alikuwa ameandamana na viongozi wengine wa jeshi la Burundi. 15:00 taarifa zaibuka kutoka Burundi kuwa rais Nkurunzinza ameng'olewa'' madarakani.
Ripoti kutoka Bujumbura zinasema kuwa kamanda mmoja wa kijeshi
ametangaza kuwa hamtambui tena Pierre Nkurunziza kama rais wa Burundi Meja Jenerali Godefroid
Niyombareh amewaambia waandishi wa habari mjini Bujumubura, kuwa
kumeundwa kamati maalum ya kuiokoa Burundi itakayotawala taifa hilo kwa
kipindi cha mpwito. Kulingana na taarifa iliyopeperushwa na redio Isanganiro, serikali ya Nkurunziza imeon'golewa madarakani. Meja Generali Niyombareh
amesema wamechukua hatua hiyo baada ya watu wa Burundi kukataa kwa
kinywa kipana awamu ya tatu ya urais wa Nkurunziza. Jenerali huyo
aliyetimuliwa na Nkurunziza mwezi februari anasema kuwa Nkurunziza
alishindwa kuheshimu mwafaka wa amani mbali na sheria za kimataifa. Kwa sasa rais Nkurunziza yuko
nchini Tanzania alipokuwa anatarajiwa kujumuika na viongozi wa kanda hii
ya Afrika Mashriki kutafuta suluhu ya mgogoro wa Burundi tangu
Nkurunzinza atangaze nia yake ya kuwania awamu ya tatu. Jenerali Niyombareh alikuwa ameandamana na viongozi wengine wa jeshi la Burundi. Tayari wanajeshi wameshika doria nje ya makao makuu ya runinga ya taifa.
0 comments:
Post a Comment