Jana katika Channel ya CNN moja ya taarifa kubwa ilikuwa ni hii ishu ya mtangazaji wa CNN Brooke Baldwin kufanikiwa kupanda Mlima Kilimanjaro uliopo ndani ya Tanzania..
Kwake hili ni tukio kubwa sana kwa kuwa
alisikia mengi kuhusu huu Mlima kutoka kwa rafiki yake ambaye
alitembelea Kenya miaka ya nyuma, aliporudi alikuwa na story nyingi
kuhusu twiga, kabila la Wamasai na Mlima Kilimanjaro.. ikawa ndoto yake
nae aje aone.
Kaitimiza ndoto hiyo mwaka huu, ni kumbukumbu kubwa ambayo anajivunia Brooke.
CNN
waliipa uzito sana taarifa hii, nimeona nikusogezee na wewe uone PICHAZ
za mtangazaji huyo akiwa kwenye safari yake hiyo ndani ya Tz mtu wangu.
Alipata nafasi kupitia Zanzibar pia, alichoenjoy alishare na watu wake Instagram..
Hii sio mara ya kwanza kwa watu maarufu ama watu wakubwa duniani kutembelea Tanzania kimyakimya, kama unakumbuka Oprah aliwahi kufika pia hifadhi ya Serengeti mwaka 2013.
0 comments:
Post a Comment