Kila mmoja atakubaliana na mimi kwamba mahusiano baina ya
wapendanao kwa kawaida yanakusudia kuwa ya upendo, maelewano, kuaminiana
na urafiki wa hali ya juu ingawa hali halisi siyo hiyo katika uhusiano
wa wengi. Wengi wetu wameumizwa kwa mapenzi. Inawezekana mara moja au
nyingi na hasa kutokana na tatizo la uaminifu katika mahusiano yao.
Zifuatazo nia alama zitakazokusaidia kuwa macho mara utakapoona mazingira ya kufanana nazo yanatokea katika uhusiano wenu.
Yawezekana mpenzi wako alikuwa amezoea kuvaa
kawaida, hapa simaanishi kutopendeza na wewe ulikuwa umemzoea katika
halifulani ya mavazi au mitindo mara ghafla anabadilika na kuwa
mtanashati zaidi ana badilisha mavazi, anapenda mavazi ya garama, labda
alikuwa hatumii manukato lakini gafla anaanza kupenda manukato,
anajijali zaidi ya kawaida yake kiasi ambacho hukumzoea. Katika hali hii
jaribu kuwa macho zaidi kufahamu nini kilicho sababisha mabadiliko
hayo..
2.Kuanza kuchelewa kutoka kazini mara kwa mara.
Sio kwamba kila mtu anapochelewa kutoka kazini
basi anakuwa sio mwaminifu, lakini zaidi ya asilimia 75 (kutoka kwenye
tafiti) ya ambao wamekuwa na mahusiano nje wamekuwa wakitoa visingizio
vinavyohusiana na kazi, vikao, mikutano na safari za kikazi, yamkini
wewe ni shahidi wa hili.
3.Anapenda kutembea na mipira ya kinga mara kwa mara (kondomu)
Inashangaza mara nyingine kusikia mpenzi mmoja ana
tabia ya kubeba kondomu kwenye pochi yake au mfukoni kwa kisingizio
kuwa anajali cha kushangaza zaidi unakuta yuko katika mahusiano na mkewe
au mumewe.
4.Mazingira tatanishi ya simu:
Gafla simu zinaanza kumiminika mpaka mida ya
usiku. Yamkini pia alikuwa yuko huru hata simu yake inapolia waweza
ichukua na kumpatia lakini gafla anakuwa na hofu kubwa na kuificha simu
yake, nimeongea na wengine ambao wanakwenda na simu hadi bafuni isije
ikasikika.
Wengine wanaondoa milio katika simu zao wakati
haikuwa kawaida yao, kuwe siri (password) ngumu hadi mwenyewe anashindwa
kuikumbuka, wako ambao simu zao zikipigwa hawawezi kupokea na kuongea
kwa uhuru kama kawaida, ataondoka na kujitenga pembeni akijifanya
anaongea kiuaminifu kabisa.
5.Harufu ambazo hujazizoea:
Kwa kuwa wapendanao huwa wamezoeana, maranyingi hata aina ya
manukato mmoja anayotumia yanakuwa yanajulikana kwa mwenzake, Sasa hembu
fikiri unamkuta mpenzi wako ametokea na ana harufu ya tofauti kabisa na
uliyoizoea, umeisikia harufu hiyo akiwa amerudi toka kazini wakati
asubuhi alipoondoka alikuwa na harufu ile uliyoizoea.
6.Tabia za kuanza kukufuatiliasana au hata kukuganda:
Wapop wanaotawapeleka wapenzi wao kila wanakotaka,
nakutoruhusu mazingira ya wapenzi hawa wakike kuwa huru kufanya mambo
yao wenyewe, wengine waliitafsiri hali hii kama penzi kubwa lakini baada
ya muda unagundua kuwa ile ilikuwa ni ujanja wa kuficha uhalisi wake na
kuzuia mazingira kwa mpenzi wake kugundua au kupewa taarifa ya tabia
zake.
7.Mabadiliko katika tendo la ndoa:
Jambo hili linaweza kujidhihirisha katika picha
mbili tofauti. Kwa kawaida wapenzi huwa na mazoea fulani katika tendo la
ndoa, kwa muda waliokaa pamoja kila mmoja humfahamu mwenzake kwa kiasi
fulani. Inawezekana likawa jambo la kushangaza pale ambapo gafla
unamuona mpenzi wako anapoteza kabisa hamu ya tendo la ndoa, au hata
mnapokuwa katika tendo hilo humuoni akifurahia bali anakuwa kama
anayelazimishwa au kutohamasishwa na chochote.
8.Marafiki wa mpenzi wako kukukwepa:
Inabidi ujiulize sana pale inapotokea gafla wale
marafiki wa mpenzi wako uliowazoea, uliokuwa unawapigia simu wakati
wowote leo wana kukwepa na hata simu hawapokei na mara nyingine
wakipokea hawakupi taarifa yakueleweka au wanakudanganya. Hii yote
inawezekana wanamlinda rafikiyao, au wanakosa cha kujibu maana wanajua
uhalisia wa kinachoendelea.
9.Kuzungumza sentensi za kutatanisha:
Unaweza kukuta katika mapenzi yenu mpenzi wako
anaanza kuwa na sentensi ngumu na zisizo kuwa na msingi kwa mfano
anasema “kwa jinsi hii sidhani kama tutafika” “mi siamini kama mapenzi
yanadumu” “yani ndio maana watu wanashindwa kukaa na mpenzi mmoja” na
maranyingine anaweza kukuuliza baadhi ya maswali moja kwa moja ili
kukuona utajibuje. Sentensi hizi zina chanzo moyoni, kuwa macho.
10.Kuzidi kwa tabia za kutoonekana au kuponyoka:
Gafla sikuhizi haagi anakwenda wapi, ukiuliza
inawezakuwa vita. Anakuwa na vijisafari vingi na vijisababu visivyoisha
vya kumuwezesha kuponyoka.
11.Tabia za kuficha fedha:
Hii utaiona ghafla mpenzi wakeo anaanza kuwa na siri kuhusu fedha zake au matumizi yake, na wala hapendi kuulizwa ulizwa kuhusu suala hilo. Tabia hii ikidhihirika katika mapenzi yenu usichelewe kuchunguza maana kwa kukaa kimya unaweza kujikuta umechelea mwana na maji ya moto.
Hii utaiona ghafla mpenzi wakeo anaanza kuwa na siri kuhusu fedha zake au matumizi yake, na wala hapendi kuulizwa ulizwa kuhusu suala hilo. Tabia hii ikidhihirika katika mapenzi yenu usichelewe kuchunguza maana kwa kukaa kimya unaweza kujikuta umechelea mwana na maji ya moto.
0 comments:
Post a Comment