Huku kwetu tuna utaratibu wa kuwapa watoto wetu majina
tunayopenda, yapo majina ya watu maarufu kama viongozi, wanasoka,
waigizaji na wengineo.
New Zealand: Msajili wa Vizazi, Vifo na Ndoa nchi
hii ameagiza baadhi ya majina kupigwa marufuku ikiwemo majina
haya;Majesty, Queen Victoria, Lucifer na jina laMafia No Fear.
Venezuela: Wao wamezuia matumizi ya jina la Superman kwa kuwa ni gumu kulitamka.
Denmark: Wametoa list ya majina rasmi ambayo yako
zaidi ya 7,000 mtoto akizaliwa anachaguliwa jina kati ya majina hayo,
moja ya majina yaliyozuiwa huku ni jina la Monkey.
Brazil: Jina lililozuiwa huku ni jina laSaddam Hussein.
Mexico: Wamepiga marufuku mtoto kupewa majina ya Scrotum, Terminator, Burger King,Hitler na Virgin.
Uturuki: Mahakama imezuia mtoto kupewa jina la Osama Bin Laden
Portugal: Wao wamezuia jina la Tom.
Mfano hii ingekuja Bongo, majina gani ungependa yazuiwe wasipewe watoto wetu
0 comments:
Post a Comment