Teknolojia inazidi kukua na watu hawajaridhika kabisa na kile kinachoonekana duniani kuwa ni mageuzi.
Mjasiriamali
 wa Marekani ambaye ni mzaliwa wa Afrika Kusini, billionaire Elon Musk 
ambaye amegundua teknolojia ya mwendo kazi wa hali ya juu ‘The Hyper 
loop’ amekuja na wazo la kuunda treni ambayo itakuwa na mwendo mara 
mbili ya mwendo kasi wa ndege za kawaida.
Mara
 tu treni hiyo itakapotengenezwa kwa teknolojia hiyo ya mwendo kasi, 
itakuwa na uwezo wakuondoka mara tu abiria watapokuwa ndani ya treni 
hiyo kwa idadi inayotakiwa bila kusubiri ratiba baalum kama ilivyo kwa 
treni za umeme nchini Marekani.
Elon
 Musk ameeleza kuwa endapo teknolojia hiyo itakubalika na kupitishwa 
chombo hicyho kitakuwa na uwezo wa kubeba abiria kutoka Los Angeles hadi
 San Francisco ndani ya nusu saa tu!! Mwendo ambao kwa kawaida ndege 
hutumia zaidi ya saa moja. inaweza kutoka New York hadi China kwa muda 
wa saa mbili tu.
Kwa
 maelezo ya Elon Musk, wengi wanamuona kama amechanganyikiwa na pesa 
hivi lakini baadhi ya engineers wanaonekana kuiamini idea yake kwa kiasi
 fulani hasa baada ya kuona vifaa alivyonavyo na kuelekeza jinsi 
itakavyofanya kazi.
CHEKI VIDEO HAPA LIKIWA LIMEKOLEA MOTO
 RSS Feed
 Twitter
August 14, 2014
Unknown

0 comments:
Post a Comment