Friday, February 21

Baraza la Taifa la Mitihani (NECTA) leo February 21 limetangaza matokeo ya mtihani wa kidato cha Nne kwa mwaka 2013 na kuainisha kuwepo kwa wanafunzi wengi waliopata daraja Sifuri ambao ni asilimia 42.91 ya watahiniwa wote.
Matokeo hayo pia yameonyesha wasichana wakiwa wamefaulu kwa asilimia 56.73 na wavulana wamefaulu kwa asilimia 59.58 huku nafasi za juu za ufaulu zikishikiliwa na wasichana na shule binafsi huku shule nyingi zilizoshika nafasi za mwisho kumi ni za Serikali.


Matokeo hayo yametangazwa na Dk. Charles Msonde ambaye ni Kaimu Mtendaji wa Nectana kubainisha kuwepo kwa wanafunzi 10 waliofutiwa matokeo yao baada ya kuandika matusi ambapo matokeo ya wanafunzi 31,518 yamezuiliwa kutokana na madai ya ada.
Wanafunzi walioruhusiwa kurudia mitihani mwaka 2014 ni 23 ambao hawakufanya baadhi ya masomo na wanafunzi 24 waliopata matatizo ya kiafya.

0 comments:

-