Robyn Rihanna Fenty, Mwimbaji maarufu na mwenye mafanikio makubwa kimuziki na hata katika ulimwengu wa mitindo ameeleza kuwa hakupenda kabisa kuwa maarufu, ila umaarufu ulikuja tu.
Rihhana
amefunguka wakati akifanya mahojiano na jarida maarufu la Vogue la
nchini Marekani, ambapo yeye ndiye atakayelipamba jarada la toleo jipya
la jarida hilo litakalotoka rasmi March mwaka huu.
Katika
interview aliyofanyiwa na Plum Sykes, mwimbaji huyo alieleza kuwa
alikuwa anapenda sana kuimba wakati akiwa mdogo lakini pamoja na kuimba
sana hakuwahi kabisa kutaka kuwa maarufu.
“Nilikuwa
naimba sana kama mtoto, sana. Nilifanya mazoezi sana kuitengeneza sauti
yangu. Napenda kuimba. Nilipenda na haikuwa ratiba ya kila siku. It’s
an expression. Sikupenda kuwa maarufu. Nilitaka tu muziki wangu usikike
duniani kote. Kisha ikatokea na ikaja na umaarufu.” Rihanna aliliambia
jarida la Vogue.
Alifunguka
pia kuwa alipokuwa mdogo alipenda sana muonekano wa ki-tomboy aka jike
dume, na kwamba alikuwa anapenda sana kuvaa nguo za kiume na kuonekana
kama mwanaume.
“Nilipokuwa
na umri wa miaka 13 au 14, sikuwa nataka kuvaa nguo ambazo mama yangu
alikuwa anataka nivae. Nilikuwa napenda sana muonekano wa kivulana.
Marafiki zangu wote walikuwa wavulana. Nilikuwa napenda vitu ambavyo
wavulana wanafanya.” Alisema Rihanna.
Aliongeza
kuwa kutokana na kupenda muonekano huo, mama yake hakupata shida ya
kuchagua nguo kwa ajili yake kwa sababu nguo alizokuwa anamchagulia kaka
yake, alichagua kama hizo pia kwa ajili ya Rihanna hivyo wakawa wanavaa
saresare.
“Tulikuwa
tunavaa jeans zinazofanana, fulana zinazofanana.” Alisema Rihanna na
kufafanua kuwa alikuwa anafanya vitu ambavyo viko kinyume na mpangilio
wa jamii yake kuanzia maamuzi na muelekeo na kwamba alikuwa anafahamu
hicho.
0 comments:
Post a Comment