Saturday, August 12

Ulimwengu (Universe) ni mkubwa sana, yani mkubwa kupindukia na kila tunachoweza kuona kwa macho na pia kwa technolojia ya juu kabisa, kama hizi telescope za Hubble, Chandra na nyinginezo ni part ndogo tu ya ulimwengu na inaitwa “observable universe”. Size ya observable universe iliyokokotelewa na wanahisabati ni kipenyo chenye urefu wa miaka bilioni 46 ya kusafiri kwa mwanga. Hii inaweza kuelezewa hivi kama kuna nyota imelipuka leo katika kona ya mwisho ya upande mmpja wa ulimwengu, baada ya miaka bilioni 46 kiumbe aliyeko katika sayari upande wa pili wa ulimwengu ataona mlipuko huo. (hii ni iwapo mwanga huo utaweza kufika). Hii inafanya galaxy yetu iwe kitu kidogo sana zaidi ya punje ya vumbi ilivyo katika dunia.

Picha ya kufikirika ya kiumbe katika anga za mbali
Ni ukweli usio na shaka kwamba kuna nyota nyingi sana zinazofanana na jua letu katika maeneo mengine ya mbali sana katika universe. Wanasayansi wanasema nyota zinazofanana na Jua letu ni kati ya asilimia tano hadi ishirini (5% - 20%) ya nyota zote katika Universe tunayoweza kuiona (observable universe). Hili neno la universe tunayoweza kuiona lina maana kwamba pale tusipoona basi kuna uwezekano universe inaendelea au kunavitu vingine tusivyovijua lakini makadirio yanayofanyika ni ya ulimwengu tunaoweza kuuona. Sasa ukumbuke katika mada ile ya Maajabu na Ukweli kuhusu Nyota za Angani, nilisema nyota zinakadiriwa kuwa sextillion 100 au zaidi katika ulimwengu tunaoweza kuuona sasa tukisema mfano tuchukue tu asilimia 5 yake, basi tutakuwa tunaongelea nyota bilioni-bilioni 500 zinafanana kimazingira (joto, ukubwa, umri, aina, uwepo wa sayari) na jua letu. 



Sasa kwa number hizi basi ina maana uwezekano wa kuwepo sayari zenye maisha ni mkubwa ingawa maisha yanaweza yasiwe haya tunayoyajua sisi. Utafiti wa kisayansi uliyofanywa na PNAS (Proceedings of the National Academy of Sciences) unapendekeza kwamba kuna angalau asilimia moja (1%) ya sayari zinazofanana sana na dunia yetu katika hizi nyota zinazofanana na jua.


Wanaofikiri kuhusu dhana ya viumbe vingine nje ya sayari yetu hawatarajii sana kuwepo na binadamu wanaofanana na sisi.Ingawa hilo linawezekana lakini kumbuka kisayansi mazingira yanachangia sana mwonekano au matokeo ya viumbe. Kama mazingira yakiwa tofauti kidogo basi matokeo ya maisha au viumbe yatafuata mkondo. Hili tunaliona hata katika viumbe wa kawaida wa duniani jinsi wanavyokuwa na vigezo vinavyoendana na wao kumudu mazingira yao. Kwa kuwa hata hizi sayari zinazofanana na dunia haziwezi kuwa na mfanano pacha yani circumstance zile zile basi tusitegemee kukutana na viumbe wanaofanana asilimia mia na sisi. Jinsi kila kitu kinavyoonekana leo hii ni matokeo ya jinsi mazingira yalivyokuwa miaka milioni iliyopita na vivyo hivyo kadri muda unavyoenda. 
Kuwa na akili zaidi yetu au kuwa na maendeleo na technology kubwa sana zaidi yetu hili ni wazi na lina sababu zake. Kwanza kuna uwezekano wa utofauti wa maisha kuanza hivyo kufanya viumbe wengine kama wapo basi wengine wanaweza kuwa wame-evolve zaidi yetu kwa kuwa na muda mrefu zaidi katika ulimwengu. Kama tukichukua mfano wa dunia yetu (Earth), maisha yanakadiriwa ku-evolve kutoka katika simple form kati ya miaka bilioni 3.5 iliyopita hii ni kutoka kwa evolutionists. Kuna sayari zilizo na muda mrefu zaidi ya dunia na hapa lazima utaona katika hali ya kawaida sisi ndo tunaanza na kuna wengine waliokwisha piga hatua kubwa sana. Na hata tukisema katika sayari nyingine kuna viumbe waliumbwa au walitokea kabla yetu alafu sasa tujilinganishe nao lazima watakuwa wametuzidi mbali.
Kama kuna kiumbe kikifika katika sayari yetu basi hii ina maana technology inayowezesha kusafiri umbali huo si ya kawaida. Kuna umbali mrefu sana kati ya nyota moja na nyingine hasa zile ambazo haziko katika mfumo wa nyota panya au nyota kundi. Hata nyota iliyo jirani yetu si rahisi kuifikia kwa technolojia ya usafiri tuliyonayo sasa. Mwendo wake ni miaka elfu sabini njiani kutoka hapa na kufikia nyota jirani kwa speed kali kabisa ambayo space shuttle inaweza kwenda.

Katika mada zijazo nitazungumzia aina ya viumbe vinavyodhaniwa kuwepo huko kwenye anga za mbali na maelezo zaidi kwa kulinganisha na sisi.

0 comments:

-