Ukiachia soka, mchezo wa ngumi na tennis nayo pia iko kwenye list ya kupendwa zaidi na watu hasa kwa nchi za Magharibi.
Kwa upande wa mchezo wa Tennis nao umejizolea umaarufu mkubwa kutokana na kuwa na mashabiki wengi na hata wachezaji kujikuta wakitajirika kupitia mchezo huo kama ilivyo kwa soka na masumbwi.
Leo nimekuletea list ya mastaa wa tenisi wanaoongoza kwa kuwa na utajiri zaidi duniani.
1. Roger Federer
ndiye mcheza tenis anaongoza kwa utajiri zaidi duniani ikiwa ni wa dola
milioni 320 pamoja na kuingia mkataba wa dola milioni 52 na makampuni
ya Nike,Rolex, Wilson
2. Andre Agassi amezaliwa katika mji wa Nevada USA, anashika nafasi ya pili kwa utajiri akiwa na dola milioni 175
3. Pete Sampras, amezaliwa Maryland USA, anashika nafasi ya tatu kwa utajiri duniani akiwa na dola milioni 150
4. Serena Williams,
amezaliwa Michigan USA, na anakamata nafasi ya nne kwa utajiri akiwa na
dola milioni 140, pia ameingia mkataba wa dola milioni 40 na kampuni ya
Nike na Kraft Foods
RSS Feed
Twitter
August 10, 2015
Unknown
0 comments:
Post a Comment