Unaambiwa
huko Shinyanga kuna binti ambae anatabia ya kujipiga picha za utupu na
kuzisambaza kwa kuwatumia wanaume mbalimbali pamoja na magroup ya
what’saap aliyojiunga nayo na kujisifia kuwa yeye ni mzuri, watu
waliopata picha hizo ziliwakera na kuamua kwenda kuzisafisha na
kuzisambaza maeneo mbalimbali ikiwemo stand ya mabasi.
Wakizungumza kwenye Hekaheka marafiki
zake wameelezea kusikitishwa na kitendo alichokifanya msichana huyo kwa
kuwa amewazalilisha wanawake wote na yeye mwenyewe ndio aliowarushia na
kuzisambaza kwa makusudi katika mitandao na walishamkanya lakini
hakusikia.
Kijana mmoja ambae nae alitumiwa amesema
alishangaa kurushiwa picha hizo na binti huyo lakini hakujua alifanya
hivyo kwa lengo gani lakini alimchukulia kama msichana mwenye tabia
chafu.
Msichana huyo amesema hizo picha
amepigwa na mtu wake wa karibu kwa makubaliano yao wenyewe lakini badae
alishangaa kuona amezisambaza kwa makusudi na kumzalilisha na pengine
amepata chochote kwakupost hizo picha.
0 comments:
Post a Comment