Monday, February 23


Uteuzi wa Makonda ni fimbo kwa mafisadi.Asibezwe anaweza.

Anaitwa Paul Makonda.Ni Katibu wa Hamasa na Chipukizi wa Uvccm.Kijana mdogo mwenye ujasiri wa kipekee asiyeogopa kejeli,dharau na fitna za mafisadi.Kwasasa ndio Mkuu wa wilaya ya Kinondoni.

Jamii ya wenye akili inashangaa wanaobeza uteuzi wa rais kwa Paul Makonda.Inawashangaa wanaomponda Paul Makonda.Haijajulikana hadi sasa nia na sababu zenye mashiko zinazotumika kumchafua Paul Makonda.Vijana wanaombeza ndio haohao wanaoomba kila siku kuwa vijana wapewe nafasi katika vyombo vya maamuzi.

Kumponda Paul Makonda ni kudharau uteuzi wa rais wa nchi.Rais anatambua umuhimu wa vijana kupewa nafasi.Anatoa fursa kwa vijana.Hili ni jambo la kupongezwa sana.Ni hatua kubwa na nzuri kwa ukuwaji wa demokrasia nchini.

Paul Makonda kaaminiwa.Mnalalamika kila siku kuwa kina January na Kigwangallah au Mwigulu wasibezwe tena wao wanaomba nafasi kubwa ya urais.Lakini Paul Makonda kupewa Udc mnaona kama kapendelewa na hawezi.Sisi tunaamini Paul Makonda anaweza na wilaya aliyopewa aiongoze ataimudu,aungwe mkono kwa asilimia mia moja.

Kelele za mafisadi zisiondoe imani kwa vijana wasiowaunga mkono.Paul Makonda anapinga ufisadi.Ni jasiri.Mpiganaji wa kweli dhidi ya maovu.Kambi za urais zisiwapotoshe.Wanaomsema hovyo wamepoteza dira ya kisiasa na kimaisha.Wana political stress isiyotibika inayotokana na kukosa maadili ya uongozi na kisiasa.

Abarikiwe Paul Makonda.Abarikiwe aliyemteua.Ibarikiwe Ccm.Ibarikiwe Tanzania.Ibarikiwe Kinondoni.Viva Paul Makonda "Jembe".

0 comments:

-