WATU wanne wamefikishwa katika Mahakama ya Jiji kwa tuhuma za kununua
machangudoa katika eneo la Buguruni Rozana jijini Dar es Salaam.
Watuhumiwa hao waolifikishwa Jumanne ya wiki hii katika mahakama hiyo ni
Antidius Severian (25), Yaham Mihamed (24), Ally Hassan (35) na Mohamed
Hamis (27).
Wakisomewa mashtaka na wakili wa Serikali, Ramadhan Kalinga mbele ya
Hakimu Mkazi Mfawidhi Bernard Mpepo, alidai kuwa Februari 14, mwaka huu
katika eneo la Buguruni Rozana watuhumiwa hao walikamatwa na askari
mwenye namba E.7882D/CPL wakifanya manunuzi ya madada poa hao huku
wakijua ni kosa kisheria.
Hata hivyo, washtakiwa hao walikana kosa hilo, ambapo Hakimu Mpepo,
alisema dhamana kwa watuhumiwa hao ipo wazi ambapo aliwataka kila mmoja
kuwa na wadhamini wawili ambao kila mmoja atasaini dhamana ya Sh
200,000.
Watuhumiwa hao walishindwa kutimiza masharti ya dhamana na kurudishwa
rumande hadi Februari 24, mwaka huu kesi itakapotajwa tena.
0 comments:
Post a Comment