Leo February 16 kwenye show ya Mkasi kulikuwa na Interview na Mwandishi wa Habari Jerry Muro, mengi kayazungumzia ikiwemo kuhusu familia, kazi yake na kesi za rushwa, pamoja na mapenzi yake na timu ya Yanga yalikoanzia.
Alichokijibu kwanza kuhusu familia; “Nna
mke.. watoto hapana, ni suala la muda na wakati kujipanga. Hawa ambao
wana watoto sasa hivi hawakukosea lakini hata ukiangalia mfumuko wa
watoto wengi Panya Road wametoka wapi. Mtoto akipatikana kwa wakati
sahihi na ukimleta duniani kwa malengo sahihi hawezi kwenda kuwa Panya
Road“
Kuhusu ishu ya watu kukimbia taaluma ya ualimu; “zamani
wakati tunakua tukienda Kijijini tunaambiwa ‘ile ni nyumba ya mwalimu’,
zamani mtu kuwa mwalimu alikuwa na nafasi kubwa kwenye jamii kuliko
hata Waziri.. Ualimu wa Nyerere ndio ulimpa nafasi kubwa sana tangu
ameanza harakati zake mpaka kushika madaraka.. Hakuna jambo tulilikosea
na hatutasamehewa kwa Mungu tulipoamua kubinafsisha sekta nyeti sana,
elimu na afya“
Suala la kugombea Ubunge; ” Naamini
kiongozi bora ni yule ambaye amesha demonstrate tangu mwanzo kabisa na
ameshaonyesha vitu ambavyo vinaashiria huyu ni kiongozi. Mimi sijisemi
kuw ni kiongozi mzuri kwa wale wanaojua kazi nilizozifanya kipindi kile
niko kwenye uandishi wa habari nili demonstrate“
Kuhusu ishu ya kesi ya Rushwa; ” Mimi sikuomba rushwa nikakamatwa.. askari mmoja akahoji hapa tunaandikaje, tunakupa dhamana kwa kosa gani?
Baadaye nikaenda Mahakamani ikasomewa
niliomba Rushwa.. Kwenye kesi yangu wakati Hakimu anatoa ruling alisema
hapakuwa na ushahidi wa mimi kuomba rushwa..“
Sijawahi
kuomba Rushwa lakini nimekutana na mazingira mengi ya kupewa Rushwa.
Mimi ni mwandishi wa kwanza wa pekee wa television kuonesha mtu mwenye
dhamana ya Serikali.. mwenye crown akila rushwa hadharani.. Nilifanya
hiyo nikiwa ITV, baadhi ya watu wakasema huyu si ameotea tu.. Nilipoenda
TBC nikafanya tena story ileile nikarusha.. Tangu nilipomaliza kesi
yangu mpaka leo sijaajiliwa na mtu yoyote“
Hapa alizungumzia mapenzi yake na Klabu ya Yanga yalikoanzia; “Mapenzi
na Yanga yalianzia kwa baba yangu.. Baba yangu alikuwa anapenda Yanga..
Ukifanya utafiti wa juu juu tu katika nchi zilizo kwenye ukanda huu wa
Afrika Mashariki Tanzania inaongoza kuwa na mazingira mazuri sana ya
mchezo wa mpira wa miguu. “
0 comments:
Post a Comment