BAADA ya
kudaiwa kuwa wapenzi na kisha habari hizo kufifia, hatimaye penzi la
mwigizaji wa filamu za Kibongo, Jacqueline Wolper na Mbongo Fleva,
Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’, limeibuka upya ambapo safari hii Nay
ameamua kufunguka hadharani.
Kwa
mujibu wa chanzo makini, wawili hao walianzisha uhusiano wao mwishoni
mwa mwaka jana na sasa mapenzi ndiyo yamekolea hadi kufikia hatua ya Nay
wa Mitego kuanika hisia zake mtandaoni.
“Wamekuwa
wakibanjuka kwa siri sana si unajua Nay ana mchumba wake Siwema, bado
hajafanya maamuzi magumu ya kumtosa,” kilisema chanzo chetu.
Paparazi
wetu alifanikiwa kunasa ujumbe wa Nay wa Mitego kwenye mtandao wa
Instagram ambao ulionyesha wakiitana kwa majina ya wapendanao kuonesha
dhahiri wawili hao ni wapenzi.
Mbali
na kuitana huko, Nay alionesha kuwa amemmisi Wolper ambapo muda mchache
baadaye naye alijibu kwa kuwa amemmisi pia kisha Nay akaifuta posti
hiyo baada ya kuandamwa na maneno ya wapambe.
Alipoulizwa Wolper kama kwa sasa ameamua kutulia na Nay wa Mitego na
mipango ya uhusiano wao ipoje, alikataa kufunguka moja kwa
moja.“Kiukweli Nay ni mshikaji wangu tu, unajua nini? Kwa sasa siko
tayari tena kumwanika bwana au mchumba wangu kama nilivyofanya mwanzo
kwa Dallas, nitakuja kumweka wazi labda mwanaume nitakayezaa naye au
atakayenioa kabisa,” alisema Wolper.
Kwa upande wake Nay alipoulizwa kuhusu uhusiano wake na Wolper na hatua
ya kuunadi uhusiano wao mtandaoni huku ikifahamika kuwa ana mchumba
mwingine, hakutaka kufafanua zaidi ya kujibu:
“Mimi huwa siangalii nani atasema nini wala atafikiria nini, mimi
nilimmisi Wolper wangu, sikuwa na namna zaidi ya kutumia peji yangu kama
nilivyofanya, tena siku hiyo alikuwa hapatikani hewani nikaamua
kumtupia mtandaoni bila hofu kwani ni mtu wangu wa karibu na siogopi
kitu juu yake,” alisema Nay wa Mitego.
0 comments:
Post a Comment