Wednesday, January 14


Jaribu kufikiria mwimbaji wa nyimbo maarufu kama Safari Siyo Kifo, Yako Wapi Mapenzi, Nani Kama Mama, Usilie na nyinginezo anapoamua kutengeneza video na watayarishaji wakubwa Afrika nini kitatokea?
Hiki ndicho alichopanga kukifanya mwimbaji wa muziki wa dansi ambaye mara nyingi hupenda kusimama kama ‘solo artist’, Christian Bella kwa ajili ya kukuza soko la muziki wa dansi Tanzania, akifuata nyayo za wasanii wa Bongo Fleva.
Bella amesema kuwa kuanzia Februari mwaka huu, atatengeneza video kubwa itakayoongozwa na mtayarishaji God Father nchini Afrika Kusini.
“Kwa nafasi niliyonayo sasa, nikiendelea na video za ‘kitoto’ nitafeli, natoa wimbo mmoja matata nitakaoanza nao mwaka, mwanzoni mwa Februari utakuwa tayari.
Namwomba Mungu mipango yangu iende kama nilivyopanga, ikiwamo kufanya video kubwajapokuwa zina gharama kubwa na mimi sitaangalia suala hilo, nataka mafanikio, hivyo lazima nijilipue ili kujitangaza kimataifa,” alisema Bella.
Bella alisema kwa sasa ameshatenga kiasi kikubwa cha fedha ili akamilishe mpango huo, kwani anaamini akitayarisha video kubwa, itakuwa rahisi kazi zake kuonyeshwa katika televisheni kubwa Afrika kama MTV Base, Channel O, Trace na kwingineko.
“Najua gharama yake inaweza kufika kiasi cha Sh68 milioni. God Father ndiye mtayarishaji nayemlenga kwa sasa, gharama hiyo ni video tu pasipo kuangalia mambo mengine, ikiwamo usafiri, mavazi na vitu vingine muhimu,” alisema.
Alisema uamuzi huo umetokana uchunguzi alioufanya pamoja na ushauri kutoka kwa watu kadhaa, wakiwamo wadau wa muziki.
“Mwaka huu sifanyi kawaida kama miaka iliyopita, kwa sababu tunakoelekea lazima tuangalie mwelekeo wa dunia, nini kinahitajika ili kufikia malengo ya kufanya vizuri.
“Ndoto yangu ni kutengeneza pesa, lakini hilo linawezekana kama nitafanya jitihada,” alisema Bella na kuongeza:
“Kwa mfano, leo wamemtambua Diamond Platnumz katika Channel O, Trace, BET kwa sababu ya video kubwa.
Haimaanishi kwamba Diamond anafanya muziki mzuri kuliko wasanii wote Tanzania hapana, lakini tunampongeza na kumuunga mkono na kumpa hongera kwa kuthubutu vitu vikubwa kama hivi, mtu anayeanza na anayefanya vizuri lazima umpongeze na wewe upite palepale.”

Alipoulizwa kuhusu umahiri wake katika tungo mbalimbali za mashairi na sauti yake yenye kuvuta hisia za mashabiki wa muziki wa dansi, Christian Bella alisema huchukua miezi kadhaa kutunga mashairi ya wimbo mmoja.
“Sikurupuki, inachukua muda mrefu, linaweza kuja wazo la mrindimo kwanza likakaa kichwani, baadaye nikarekodi kidogo kwenye simu nauacha naanza kutafuta meneno kidogo kidogo siyo kwa haraka.”
Alisema kuna nyimbo zingine za haraka ambazo, huingia studio siku hiyohiyo akatengeneza wimbo mara nyingi huwa ‘kolabo’ na siyo nyimbo zake.
“Nyimbo zangu zinachukua muda, natulia na wazo, nafikiria nini cha kufanya, sina haraka kufikia kutoa uamuzi,” anasema.
“Wakati mwingine nakaa na mtu na kuanza kumuuliza hivi hapa nifanye nini ili wimbo uwe bora nikiimba...Hivi naeleweka, nachunguza na kufanya utafiti kabla ya kuwalisha mashabiki.”
Ingawa hutumia miezi kukamilisha wimbo mmoja, Bella alisema anaweza kuimba mwanzo hadi mwisho katika mtindo wa moja kwa moja ‘freestyle’.
“Naweza kuimba ‘freestyle’, lakini linapokuja suala la kurekodi, lazima niifikirie kwanza inapendeza, inafaa kwa jamii, mfano wimbo Nakuhitaji niliouanza kama Rhumba, lakini kuandaa mdundo unaitwa mutwashi ndiyo

0 comments:

-