Tuesday, April 29

   TZA AFISA WA POLISI KENYA 
taarifa kutoka Kiambu Kenya ambapo hisia tofauti zimetolewa kuhusiana na picha ya askari wa kike wa usalama barabarani iliyofanya mabosi wake kumkemea.
Sababu kubwa ni picha ya Trafiki huyo aliyekua amevalia sketi fupi iliyombana huku akiongoza doria wakati wa mashindano ya magari katika kaunti ya kiambu ilisababisha picha iliyopigwa na mwanahabari wa gazeti moja nchini Kenya kuzua mjadala kwenye mitandao ya kijamii Redioni na Televisheni nchini Kenya.
Linda Okello ni afisa wa trafiki mwenye cheo cha koplo
aliitwa ofisini na mkuu wa Trafiki kaunti ya kiambu James Mugeria na kumkemea vikali akitaja kwamba vazi hilo linakiuka maantiki ya kikazi katika kikosi cha polisi.
Baadhi ya watu waliotoa maoni yao kwenye mitandao ya kijamii wamesema Trafiki huyu alilengwa na wakuu wake bila kosa ikizingatiwa kwamba sare ama magwanda ya maafisa wa polisi hutolewa kwao na serikali na pia kumekua na madai kwamba Linda alikua amepewa uhamisho kaunti ya Mandera japo maafisa wakuu wa polisi wemekanusha madai hayo.
Haya yanajiri miezi kadhaa baada ya Naibu wa Inspekta mkuu wa polisi Grace kaindi kuwaonya vikali maafisa wa kike wa polisi dhidi ya kutumia lipstick, kuvalia mavazi ya kimtindo, bangili na vipuri virefu wakiwa kazini.
Kifupi taarifa kwa mafisa wa polisi iliyotolewa ilisema afisa yeyote atakayepatikana na mavazi yaliyopigwa marufuku atakua amevunja sheria Nambari 37 na sheria kwa maafisa wa polisi wa mwaka 2011 kipenge numbari 87-88 na atakabiliwa kisheria.

0 comments:

-