February
24 2014 kupitia vyombo mbalimbali vya habari stori imesambaa kuhusu
milipuko kwenye visiwa vya Zanzibar ikiwa ni milipuko iliyoanza Jumapili
ya February 23 2014 na kuendelea mpaka kesho yake.
Polisi kutoka Zanzibar wamethibitisha kutokea kwa milipuko hiyo
mitatu ya mabomu kati ya Jumapili na Jumatatu leo mchana visiwani humo
ambapo mkuu wa Polisi Zanzibar Hamdan Omar Makame amethibitisha kutokea
kwa milipuko miwili leo February 24 2014.
Milipuko ya leo imetokea katika eneo la mgahawa wa Mercury huku
mlipuko mwingine ukiwa umetokea katika eneo la Mkunazini pamoja na
mlipuko uliotokea jana Jumapili katika eneo la Pangawe.
Taarifa ya Polisi Zanzibar inasema hakuna vifo wala majeruhi katika
matukio yote matatu na pia hakuna mali iliyoharibiwa lakini kutokana na
hofu na taharuki ya matukio hayo, kuna madhara ya kisaikolojia
yametokea.
Upelelezi bado unaendelea ili kuwabaini waliohusika katika matukio
hayo ingawa hadi sasa hakuna mtu au kikundi chochote kilichokamatwa
kuhusiana na matukio haya.
Kwa sasa Polisi wanaendelea kuimarisha ulinzi katika sehemu
mbalimbali Zanzibar ikiwa ni pamoja na kufanya doria katika maeneo
kadhaa huku jeshi hili pia likiwaondoa hofu Wananchi.
0 comments:
Post a Comment