Cesc Fabregas ameweka kwenye picha kwenye akaunti yake ya
Instagram wakiwa kwenye ndege leo Jumatatu na wachezaji wenzake wa
Barcelona kuelekea England kwa ajili ya Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi
Manchester City.
Ameposti
picha akiwa na wachezaji wenzake Alex Song, Carles Puyol na Gerard
Pique wakati ndege inataka kuruka mabingwa hao wa Hispania wakienda jiji
la Manchester kwa ajili ya mechi ya kwanza ya hatua ya 16 Bora,
itakayopigwa Uwanja wa Etihad.
Tayari
kuondoka: Cesc Fabregas ameposti picha hii katika Instagram yake akiwa
na Alex Song, Gerard Pique na Carles Puyol kwenye ndege kwa ajili ya
mechi dhidi ya City kesho usiku
Barcelona
inakwenda kwenye mechi hiyo ikitoka kuichapa mabao 6-0 Rayo Vallecano
Jumamosi katika La Liga, matokeo ambayo yanawafanya waendelee kukabana
koo na Real Madrid na Atletico kileleni.
Lakini
watakutana na Manchester City ambayo pia iko vizuri, ikiwa imetoka
kuing'oa Chelsea katika Raundi ya Tano ya Kombe la FA mwishoni mwa wiki
na kocha Manuel Pellegrini, ambaye ana uzoefu wa kucheza na Barca, anajiamini City inaweza kufanya vizuri katika mchezo huo.
0 comments:
Post a Comment