Wednesday, January 29


Asilimia 65 ya waliobakwa Liberia 2013 ni watoto
Theluthi mbili ya watu wote waliobakwa nchini Liberia mwaka jana wa 2013 walikuwa ni watoto. Hayo yameelezwa na serikali ya nchi hiyo ya Magharibi mwa Afrika. Wizara ya Jinsia na Maendeleo ya Liberia imetangaza kuwa asilimia 65 ya kesi 1,002 

 za ubakaji zilizoripotiwa mwaka jana zilikuwa za watoto wenye umri wa kati ya miaka mitatu na kumi na nne. Taarifa ya Wizara ya Jinsia na Maendeleo ya Liberia imesema, watoto kumi kutoka kaunti nane waliokuwa na umri kati ya miaka mitatu na 14 walifariki dunia mwaka jana baada ya kubakwa.
Hii ni katika hali ambayo ni wabakaji 49 tu ndio walioweza kufikishwa mahakamani na kushtakiwa kati ya jumla ya kesi za ubakaji 137 zilizoripotiwa mahakamani mwaka jana huko Liberia. Wizara ya Jinsia na Maendeleo ya Liberia imesema kuwa idadi ya watenda jinai hiyo ya ubakaji ingekuwa ya juu iwapo wazazi wa watoto wanaobakwa wasingekuwa wakifikia maridhiano na kumaliza kesi hizo, kwa kuwa wengi wa wabakaji huwa ni ndugu wa karibu au marafiki.

0 comments:

-