Monday, August 26

Kutokana na Historia na mazingira tofauti tofauti, Mastaa wengi ambao tunawasikia sasa, umaarufu ndio umeweza kubadilisha maisha yao kwa kuwapatia utajiri mkubwa, na wengi wanafahamu kuwa umaarufu wao ndio chanzo cha utajiri wao.




On the other side of the coin, Kuna mastaa ambao umaarufu wao umekuja tu.. wakati wao tayari ni matajiri ama wametokea katika familia tajiri, soooo... www.sammisago.com, inakufahamisha mastaa hawa ambao 'mulla' walikuwa wamekwishazizoea 'fore hawajakuwa maarufu.

Wa kwanza ni Taylor Swift, mtoto wa Scott Kingsley Swift ambaye ni Financial Adviser wa kampuni maarufu ya Merill Lynch, Amesoma shule binafsi na maisha ya kifahari sana, Baba yake anamiliki lebo kubwa kabisa ya Muziki ya Big Machine ambayo Taylor mwenyewe ana shares asilimia 3.


Wa pili ni Willow na Jaden Sm

ith, Wazazi wa watoto hawa Will Smith na Jada Pinkett kwa miaka sasa wamekuwa big fishes wakiwa na utajiri wa zaidi ya dola milioni 200.. so u can imagine maisha ya watoto hawa kabla hawajaanza kutengeneza pesa zao wenyewe.
 

                    
Mwigizaji Ariana Grande, ni mtoto wa Edward Butera ambaye ni CEO wa kampuni kubwa ya Ibi Designs.

Mwingine ni Cassie, Hakuna taarifa za ndani kuhusiana na shughuli za wazazi wake ila model na mwanamuziki huyu amekua katika maisha ya kifari, amesoma shule ya gharama sana ingawa amekulia huko London katika sehemu ambayo si maarufu kwa matajiri kuishi, High School.. ada yake kwa mwaka ilikuwa ni dola 26,000/-.


Kuna Jordin Sparks pia, baba yake alikuwa ni staa wa American Football - Phillippi Sparks, na Jodi, mama yake ni mjasiriamali mwenye mafanikio makubwa.

                  
Psy pia, hit maker wa Gangnam Style kutoka Gangnam District huko Seoul, South Korea, Baba yake.. Park Won-Ho anamiliki kampuni ya DI Corporation, na mama yake, Kim Young-hee, anamiliki mgahawa mkubwa, Baada ya Gangnam style kufanya poa, Biashara za wazazi wake zimeweza kurekodi faida zaidi na zaidi.

Miley Cyrus, wakati anazaliwa mwaka 1992, Baba yake alikuwa anaongoza katika chati za muziki za Billiboard, Billy Ray utajiri wake una thamani ya dola milioni 50.
 
Robin Thicke, mtoto wa Alan Thicke ambaye ni mwigizaji maarufu, na pia mama yake ambaye ni naye amekuwa mwigizaji wa tamthilia zenye mafanikio makubwa na malipo mazuri.

0 comments:

-