Monday, February 29


MAKAMU wa Rais, Samia Suluhu Hassan ameagiza uongozi wa Halmashauri ya Jiji la Tanga kumaliza haraka mgogoro wa uongozi ndani ya halmashauri hiyo, kuharakisha utekelezaji wa shughuli za maendeleo kwa wananchi.
Alitoa agizo hilo katika Ikulu ndogo ya Tanga wakati akizungumza na viongozi baada ya kupokea taarifa ya maendeleo ya mkoa wa Tanga baada ya kuwasili kwa ajili ya ufunguzi wa mkutano wa kimataifa wa mazingira unaoratibiwa na Unesco.
Alisema kwa kuwa uchaguzi mkuu umekwisha salama, ajenda inayopaswa kutekelezwa sasa ni utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi kuwezesha wananchi kupata maendeleo.
“Ni wajibu wa kila mkoa wa Tanga kutekeleza ilani ya CCM bila kujali kwamba jimbo moja limekwenda, kwa kuwa hapa hapako shwari ni dhahiri kwamba tutachelewesha utekelezaji wa ilani … ,” alisema.
Alisema serikali ina mpango mkubwa wa kuwekeza katika viwanda kwenye jiji la Tanga. Hata hivyo alisema endapo hakutakuwa na uongozi wa Baraza la Madiwani katika halmashauri hiyo, malengo hayo hayataweza kutekelezwa.
“Hasara nyingine ninayoiona hapa endapo hamtamaliza hayo makando kando katika baraza la madiwani ni kuvunjwa kwa halmashauri nzima … ipo hiyo hatari na naomba muelewe kwamba kama hamtafanya jitihada ya kumaliza mgogoro huu kwa utulivu, jueni kwamba serikali haitakuwa na fedha nyingine ya kurudia uchaguzi hapa,” alisema Makamu wa Rais.
Akizungumzia uwepo wa biashara za magendo ambazo hupitishwa katika bandari bubu, alisema, “magendo hapa Tanga ni mengi sana watu wanaleta bidhaa za magendo kutoka Pemba na Unguja kuja hapa Tanga bila kulipia ushuru… ” “Mapato yanavuja, kamati ya ulinzi na usalama mjitahidi kuzuia magendo hayo ili mapato ya mkoa yasivuje… mnaachia watu wanaleta magendo halafu baadaye wakishapata hela wanakuja kutupiga kisiasa ... sasa nawataka mbane hiyo mianya yote,” alisema.
Awali Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mwantumu Mahiza akisoma taarifa, alisema mkoa umejipanga na kuweka mikakati ya kutekeleza mipango mbalimbali katika sekta za elimu, afya, maji, viwanda na mazingira kuwezesha wananchi kujipatia maendeleo.



WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amekagua bandari ya Mtwara na kunusa ufisadi katika utoaji wa zabuni ya ujenzi wa gati mpya tatu.
Amekinyooshea kitengo cha manunuzi bandarini hapo, akisema kimekuwa chanzo cha upotevu wa fedha za serikali kutokana na ujanja wa watu wachache.
Waziri Mkuu aliigusa pia Bodi ya Korosho akisema yako majipu yanayohitaji kutumbuliwa kutokana na kukwamisha mizigo kupitia bandari ya Mtwara, badala yake inapitishwa kupitia bandari ya Dar es Salaam.
Utata wa zabuni Majaliwa ambaye juzi alitembelea eneo la ujenzi wa gati hizo, alisema mzabuni ameshashinda, lakini yapo madai kwamba watu wa manunuzi kupitia Mamlaka ya Manunuzi ya Umma Tanzania (PPRA) ndiyo wanakwamisha zabuni hiyo.
Alisisitiza, “Natambua kwamba kuna mpango wa kujenga gati nne ambapo moja kati ya hizo itajengwa na TPA (Mamlaka ya Bandari) lakini hizi tatu zilitangazwa na kupata mzabuni ambaye ni kampuni ya Hyundai kutoka Japan. Lakini hii kampuni imekuwa ikizungushwa bila sababu. Tutafuatilia kubaini tatizo liko wapi.”
“Sasa hivi tuna uwezo wa kupaki meli moja tu, lakini gati zikikamilika tutaweza kuwa na meli tatu kwa mpigo, cha msingi tusimamie maamuzi yetu kwamba lazima wafanyabiashara wa korosho watumie bandari hii kusafirisha mizigo yao na si kuipeleka kwingine,” alisema.
Kitengo cha manunuzi
Waziri Mkuu alimtaka Mkuu wa Bandari ya Mtwara, Prosper Kimaro kuwa makini na watu wa kitengo cha manunuzi katika bandari hiyo, akisema kimekuwa chanzo cha upotevu wa fedha za Serikali kutokana na ujanja wa watu wachache.
“Hapa si kuna mtu alitaka kuiba Sh milioni 300 kwa kufoji (kughushi) saini za wakubwa wake?” Alihoji Waziri Mkuu, swali ambalo lilijibiwa na Kimaro akikiri juu ya hilo na kusema, uongozi uliingilia kati kabla wizi huo haujakamilishwa.
Bodi ya Korosho
“Kwenye Bodi ya Korosho nako kuna majipu yanahitaji kutumbuliwa. RCC (Baraza la Ushauri la Mkoa) ilishakaa na kupitisha uamuzi kuwa mizigo yote ipitie bandari ya Mtwara lakini kuna watu ndani ya Bodi hiyo wanatoa vibali vya kusafirisha mizigo kupitia bandari ya Dar es Salaam,” alisema Waziri Mkuu.
Aliomba wabunge wa Mkoa wa Mtwara washirikiane kusimamia ujenzi wa gati uanze mara moja, ili ajira kwa wananchi mkoani humo zipatikane.
“Ujenzi ukikamilika siyo tu ajira zitaongezeka bali hata meli nyingi zitaleta mizigo katika bandari hii na mapato ya mkoa yataongezeka”, alisema.
Fidia kisiwa cha Mgao Kuhusu fidia kwa wakazi wa vijiji vya Kisiwa na Mgao ambao wamekubali kuhama ili kupisha upanuzi wa bandari hiyo, Waziri Mkuu aliwahakikishia wabunge hao pamoja na uongozi wa bandari kwamba Sh bilioni 13.8 zimekwishatengwa na Wizara na zitatolewa mapema mwezi ujao.
Alitumia fursa hiyo kusisitiza udhibiti wa bandari bubu ambazo zinatumiwa kuingiza sukari na mchele na kuikosesha Serikali mapato.
“Mkuu wa Mkoa, nilikwishatoa agizo kama hilo wakati nimeenda kukagua bandari ya Tanga. Kaa na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa nanyi pia muweke mbinu za kudhibiti upenyo huu wa kuingiza bidhaa za magendo kwa sababu hawa ndiyo wanaokwepa kulipa kodi ya Serikali,” alisisitiza.
Awali, Mkuu wa bandari ya Mtwara, Kimaro wakati akitoa taarifa ya utendaji wa bandari mbele ya Waziri Mkuu, alisema ilianzishwa mwaka 1950 na imekuwa ikikabiliwa na ufinyu wa gati ya kuegesha meli, vifaa vya kupakulia na kupakia mizigo.
Alisema hivi sasa wamekwishapata winchi ya bandarini yenye uwezo wa kubeba tani 100 na wako kwenye mpango wa kujenga gati moja.
Majipu bandarini
Waziri Mkuu, Majaliwa ameshafanya ziara kwenye Bandari za Dar es Salaam, Tanga na sasa Mtwara ambako amebaini mambo mengi hayaendi vizuri hali ambayo amekuwa akilazimika kuchukua hatua mbalimbali ikiwemo kuwajibisha watendaji.
Chini ya mkakati wa Serikali ya awamu ya tano ya kutumbua majipu, Rais John Magufuli alivunja bodi simamizi ya bandari siku chache baada ya kupatikana kwa kontena ambazo hayakuwa yamelipiwa ushuru Bandari ya Dar es Salaam.
Kampuni 43 ziligunduliwa kuhusika katika makontena hayo. Mwenyekiti wa Bodi, Profesa Joseph Msambichaka sanjari na Mkurugenzi Mkuu wa Bandari, Awadhi Massawe walivuliwa nyadhifa zao .
Pia Katibu mkuu wa wizara ya uchukuzi, Dk Shaban Mwinjaka aliondolewa kwenye wadhifa huo. Waziri Mkuu, Majaliwa alipofanya ziara ya kushitukiza katika bandari ya Dar es Salaam, aligundua kontena 329 zilipitishwa bila kulipiwa kodi kinyume na utaratibu wa bandarini.
Aidha, Waziri Mkuu, hivi karibuni alifanya ziara ya kushitukiza katika Bandari ya Tanga ambako pamoja na masuala mengine, alikuta tishali tatu zikiwa chakavu bila ya injini wakati serikali ilitoa fedha za ununuzi wa matishali ya kisasa.
Baada ya kubaini jipu hilo, alimwagiza Meneja wa Bandari ya Tanga, Henry Arika kutoa maelezo kwa maandishi ya nani alihusika na ununuzi wa matishali hayo badala ya zile mbili zilizopaswa kuwapo ambazo Serikali ilitoa dola za Marekani milioni 10.
Arika alijitetea kwamba tishari hizo ziliwasili nchini miaka minne iliyopita iliyopita lakini zilianza kufanya kazi rasmi mwaka jana na kwamba yeye hana muda mrefu katika bandari hiyo.



Usiku wa February 28 kundi la Navy Kenzo ambalo kwa sasa lina miliki air time ya vituo vingi vya Tv nje na ndani ya Tanzania kwa ngoma yao mpya ya “Kamatia Chini”, wamefanya uzinduzi rasmi wa Kamatia Chini Lights UP Tour ndani ya Maisha Basement. Mtu wangu wa nguvu hizi ni Pichaz 22 ya kilivyo happen katika uzinduzi huo.
DSC_8012
DSC_8016
DSC_8024
DSC_8027
DSC_8056
DSC_8057
DSC_8078
DSC_8084
DSC_8093
DSC_7876 - Copy
DSC_7955
DSC_7968
DSC_7969
DSC_7970
DSC_7972
DSC_7974
DSC_7976
DSC_7981
DSC_7983
DSC_7991
DSC_8011
  Millard Ayo


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amewasili Mkoani Arusha ambako pamoja na mambo mengine ataongoza Mkutano wa 17 wa kawaida wa wakuu wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki utakaofanyika Jumatano tarehe 02 Machi, 2016 Mjini Arusha.

Katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) Rais Magufuli amelakiwa na viongozi mbalimbali wa vyama vya siasa na serikali pamoja na vikundi vya burudani za ngoma kabla ya kuelekea Arusha Mjini.

Rais Magufuli ndiye Mwenyekiti wa sasa wa Jumuiya ya Afrika Mashariki inayojumuisha nchi za Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda na Burundi.Kabla ya kuongoza kikao hicho Rais Magufuli anatarajiwa kukutana na kufanya mazungumzo ya ana kwa ana na viongozi wakuu wa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Tarehe 03 Machi, 2016 Rais Magufuli na Rais wa Jamhuri ya Kenya, wataweka jiwe la msingi katika mradi wa ujenzi wa barabara ya Arusha - Holili - Taveta - Voi inayoziunganisha nchi za Tanzania na Kenya.

Barabara hiyo ni sehemu ya miradi ya maendeleo ya Jumuiya ya Afrika Mashariki inayotekelezwa na nchi wanachama wa Jumuiya hiyo.

Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU.
Dar es Salaam
28 Februari 2016

==

-