Friday, April 24
Thursday, April 23
April 23, 2015
Unknown
April 23, 2015
Unknown
Uwanjani palinoga unaambiwa.. Hapa Bayern Munich vigogo wa Kijerumani, hapa FC Porto wababe wengine wa Ureno.. dakika 90 zikakamilika kwa kuiweka Bayern kwenye headlines zenye wino mzito wenye maandishi ya ushindi wa goli 6-1 !!
Nilichogundua ni kwamba kumbe camera za wanaspoti hazikuangalia matokeo hayo ya nguvu, walikua karibu pia na suruali ya Kocha Pep Guardiola, nna hizi pichaz ambao ni story kubwa bado mitandaoni mpaka leo yani !!
April 23, 2015
Unknown
Kuna
tafiti mbalimbali zilizowahi kufanywa, lakini leo nimekuja na hii list
ya Marais nane wanaoongoza kwa kuwa na utajiri mkubwa zaidi ya wenzao
Afrika.
Ukiachilia mbali marais wengi wa Afrika
kupenda kukaa kwa muda mrefu madarakani lakini kuna hili la
kujilimbikizia mali, wengine huzipata kabla ya kuwa marais lakini wengi
wao huzipata wakati wanashikilia madaraka kwa kipindi chote wanapotawala
nchi husika.
Saturday, April 18
April 18, 2015
Unknown
Kuna jamaa yangu yupo kwenye ndoa kwa miaka saba na hajafanikiwa kupata
mtoto..hivi karibuni analikuwa ananipigisha stori fulani hivi ambazo
nilikuwa sizielewielewi.
Juzi amekuja kutoka Morogoro amekuja nyumbani kwangu Dar anasisitiza
anataka nimsaidie kutafuta dawa ili mkewe apate ujauzito eti
wamekubaliana na mkewe wanishirikishe mimi kwa sababu ni msiri na
mstaarabu.
Ili mke wake apate ujauzito kumbuka mimi siyo daktari. Alivyoona nakuwa
mkali akaniambia atanipigia simu akifika Morogoro ili tujadiliane
vizuri.
Ameondoka leo asubuhi kimsingi mimi sijaoa na sijaona sababu ya kufanya ujinga huo. Wanajukwaa mimi msimamo wangu ni hapana.
Ushauri tafadhali
April 18, 2015
Unknown
Kinyume na hapo, kukiwa na tatizo katika upande mmoja, furaha ya tendo inaondoka. Mmoja kati ya wapendanao anakuwa na shauku ya tendo wakati mwingine hana. Kitakachofuata hapo ni yule ambaye hajaridhika kutafuta njia mbadala ili kupata tiba ya mapenzi.
Mwanaume anaweza kuwa anataka kumridhisha mpenzi wake lakini anashindwa au mwanamke anataka kumridhisha mpenzi wake lakini inashindikana.Wanapokutana faragha, kila mmoja anakuwa na nia njema kabisa kutaka kukamilisha tendo la ndoa lakini tatizo linakuwa kwa mmoja wao na kuwafanya washindwe kufurahia tendo.
April 18, 2015
Unknown
MSHITUKO wa matukio ya mfululizo ya ajali,
umeendelea kugubika nchi, baada ya watu 20 kupoteza maisha katika ajali
ya basi dogo aina ya Toyota Hiace, iliyotokea jana wilayani Rungwe
mkoani Mbeya.
Ajali hiyo ambayo taarifa na picha zake zilisambaa kwa kasi katika mitandao ya kijamii, imesababisha taharuki kutokana na ukaribu wake na matukio mengine ya ajali yaliyotokea wiki hii.
Mbali na ajali hizo, wiki hii Kamanda wa Jeshi la Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani, Mohamed Mpinga alitoa takwimu zilizosababisha huzuni kwa Watanzania, kwamba kati ya Januari mosi na Aprili 12 sawa na siku 102, watu 969 walipoteza maisha katika ajali za barabarani.
Ajali hiyo ambayo taarifa na picha zake zilisambaa kwa kasi katika mitandao ya kijamii, imesababisha taharuki kutokana na ukaribu wake na matukio mengine ya ajali yaliyotokea wiki hii.
Baadhi ya wakazi wa jirani na eneola tukio wakitazama gari lilivyopata ajali kando kando ya mto Kiwira.
Tangu Jumapili iliyopita mpaka jana, siku zisizozidi sita kumetokea
ajali kubwa tatu zilizohusisha mabasi ya abiria na kuteketeza maisha ya
watu 40.Mbali na ajali hizo, wiki hii Kamanda wa Jeshi la Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani, Mohamed Mpinga alitoa takwimu zilizosababisha huzuni kwa Watanzania, kwamba kati ya Januari mosi na Aprili 12 sawa na siku 102, watu 969 walipoteza maisha katika ajali za barabarani.
April 18, 2015
Unknown
Mwenyekiti
wa Tume ya Taifa ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Jaji Mstaafu Damian Lubuva
akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, kulia ni
Mkurugenzi Mkuu wa Manunuzi na Logistic, Gregory Kaijage na kushoto ni
Naibu Katibu wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) na Mkuu wa Teknolojia ya
Habari na Mawasiliano (Tehama), Sisti Chriati.
Baadhi ya Wandishi wa habari waliohudhuria katika mkutano wa habari wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi jijini Dar es Salaam jana.
TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imesema kuwa, Uchaguzi Mkuu
utafanyika kama ulivyopangwa na haiwezi kusegeza mbele tarehe ya
uchaguzi huo kutokana na suala hilo kuwa ni la kikatiba. Baadhi ya Wandishi wa habari waliohudhuria katika mkutano wa habari wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi jijini Dar es Salaam jana.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Jaji Mstaafu Damian Lubuva amesema kuwa wanasiasa wamekuwa na kauli ambazo zinawafanya wananchi wapate hofu wakati suala hilo kuhairisha uchaguzi halipo katika tume.
April 18, 2015
Unknown
Zamani
kulikuwa na misemo ambayo ilikuwa ikitumiwa sana, utasikia kazi f’lani
ni wito.. ilikuwa kawaida yani, ukikutana na Mwalimu utaambiwa ualimu ni
wito.. Daktari nae utasikia udaktari ni wito.. siku hizi sio maneno
ambayo yanasikika sana.
Nimekusogezea hii story toka Jamhuri ya
Czech, muuguzi mmoja kafikishwa Mahakamani na kuhukumiwa kifungo cha
maisha.. kesi iliyofanywa ashitakiwe imenishtua kiukweli.
April 18, 2015
Unknown
Hii burudani haikuwa ya kuikosa mtu wangu.. pata picha yani, hapa AY, hapa Mwana FA.. huku Barnaba, Godzilla, Ben Pol.. yani wote kwa pamoja kwenye stage moja kutoa burudani ya nguvu kwa watu wao pale Regency Park Hotel.
Hiyo ilikuwa jana, Birthday party ya
wote waliozaliwa April 17.. hawakuwa wachoyo, waliwashirikisha watu wao
ambao walitamani kushiriki nao siku hii kwa kununua ticket kwa sh. elfu
10, alafu wakakutana kusherekea pamoja.
Nikapata nafasi kuzipata PICHAZ za party ilivyokuwa.
Hapa nimeshea na wewe..
April 18, 2015
Unknown
POMBE si chai! Msemo huu ulitimia hivi karibuni baada ya staa wa filamu za Kibongo, Salma Jabu ‘Nisha’ kuzidiwa na kilevi na kuanza kushindana kukata mauno na kusababisha azingirwe na wanaume waliovutiwa naye.
Staa wa filamu za Kibongo, Salma Jabu ‘Nisha’ akikata mauno.
Tukio hilo la aina yake lilitokea Jumatano iliyopita katika sherehe
ya bethidei ya mtoto wa msanii mwenzake, Halima Yahya ‘Davina’
iliyofanyika katika viwanja vya Hoteli ya Lamada jijini Dar ambapo
kulikuwa na vyakula na vinywaji vikali vya kila aina.Wednesday, April 8
April 08, 2015
Unknown
Wasanii Ney wa Mitego (kushoto) na Diamond Platinumz (kulia
Kwa
muda mrefu sasa huenda nawe umepata kushuhudia baadhi ya mastaa wa
Bongo pamoja na watu maalufu wakiwa kwenye kurasa mbalimbaali za
magazeti na majarida, mitandao ya kijamii na mabagno ya matangazoa
wakiwa katika muonekano tofauti hasa katika kuonesha miili yao
kiuhalisia.
Mastaa
hao pia tunawashuhudia kwenye video zao iwe filamu, muziki na
matangazo, wakionyesha sehemu za maumbilie yao kama kifua, tumbo,
mgongo, kiuno na hata miguu kwa baadhi yao wakiwemo wa kike.
Msanii Juma Jux
April 08, 2015
Unknown
Madereva wa vyombo mbalimbali vya moto, wanakusudia kushiriki mgomo wa nchi nzima Ijumaa wiki hii, kuishinikiza serikali kuondoa kero mbalimbali zinazowakabili ikiwemo ukosefu wa ajira za uhakika pamoja na agizo la kutaka kwenda kusoma.
Wakizungumza
kupitia Katibu wa Muungano wa vyama vya madereva Bw. Rashid Saleh,
Madereva hao wamesema kuwa suala la kurudia kusoma
kila wanapohuisha leseni zao ni aina nyingine ya unyanyasaji kwa maelfu
ya madereva nchini, ambao kwa kipindi kirefu wamekuwa hawana mfumo mzuri
wa ajira licha ya kutupiwa lawama kibao kuwa wao ndio chanzo cha
ongezeko la ajali.
April 08, 2015
Unknown
WAZIRI wa kilimo, Chakula na Ushirika Steven Wasira amewafukuza kazi wakurugenzi watendaji watatu wa Mamlaka ya Kuendeleza Bonde la Mto Rufiji (Yaani Rufiji River Basin Development Authority – RUBADA) kutokana na matumizi mabaya ya ofisi ya Umma ambayo yameitia hasara ya Bilioni 2.5 Serikali .
Akitoa
agizo hilo leo mbele ya Waandishi wa Habari, Waziri Wasira amewataja
Watendaji hao kuwa ni Bwana Aloyce L. Masanja – Kaimu Mkurugenzi Mkuu;
Bibi Tabu Ndatulu – Mkurugenzi wa Mipango na Uwekezaji; na Bwana Filozi
John Mayayi – Mkurugenzi wa Fedha na Utawala.
April 08, 2015
Unknown
Picha Ya Maktaba |
Mkazi mmoja wa Kijiji cha Ulowa Kahama, Chausiku Hamis ameuawa kwa kuchomwa moto na watu waliokusanyika katika msiba wa mtoto wa jirani baada ya kutuhumiwa kuhusika na kifo cha mtoto huyo.
Mtoto huyo mwenye umri wa mwaka mmoja
alifariki usiku katika mazingira tata ambapo mwanamke huyo aliuawa baada
ya mmoja wa waombolezaji kupandisha mapepo na kumtuhumu Chausiku kuhusika na kifo cha mtoto huyo.
April 08, 2015
Unknown
Labda
ulishtushwa na ile ya bibi harusi kujioa, kisa umri unaenda na
hajaolewa ..! Kuna ile nyingine ya mapacha kuolewa siku moja na mabwana
watatu ambao hata wao walikuwa wakiwachanganya siku ya harusi, labda
hiyo ilikufurahisha.. nyingine ilikuwa ya mwanamke kufunga ndoa na paka
wake.
Ya leo itakushangaza pia.. eti ndoa ya binadamu na nyoka?
Monday, April 6
April 06, 2015
Unknown
NI matumaini yangu wasomaji wa safu hii mko vizuri na mpo tayari kupokea mada mpya ambayo nimewaandalia. Namshukuru Mungu kwa kunipa afya, tuweze kujadili kwa pamoja mada iliyopo mezani.
Mada inajieleza hapo juu, kutokana na visa na uzoefu mbalimbali waliopitia, wanawake wamekuwa na mtazamo tofauti juu ya wanaume ambao wanatumia kilevi.Wapo wanaoamini kwamba mwanaume ambaye anatumia kilevi hafai kuwa mume lakini wapo wengine ambao wanaamini kwamba anafaa.
Wale wanaosema hafai wanakuwa na hoja zao mkononi lakini hata wale ambao wanasema anafaa, nao wanakuwa na hoja zenye mashiko.
April 06, 2015
Unknown
Mbunge wa Maswa Magharibi (CHADEMA), John Shibuda amekataa kuhusishwa na Chama cha Alliance for Change and Transparency (ACT-Tanzania), akisema hana mpango wa kujiunga nacho.
Shibuda ambaye ameshatangaza kutogombea ubunge kupitia CHAsdemA katika
uchaguzi mkuu wa mwaka huu, amesema “Pamoja na kusema sitagombea kupitia
CHADEMA lakini nisilishwe maneno…siendi kwenye chama hicho cha ACT.”
April 06, 2015
Unknown
Wakati wakazi wengi wa Jiji la Dar es Salaam wakiwa katika harakati za kusherehekea Sikukuu ya Pasaka, dada mmoja ambaye ni mke wa mtu yeye alijikuta akiiserebukia kwa fumanizi gesti, tena akiwa na mume wa mtu!
Tukio hilo lilijiri Alhamisi Kuu maeneo Buza jijini Dar, mishale ya
saa 7:00 usiku huku jamii ikiwa katika harakati za kununua hiki na kile
kwa ajili ya Sikukuu
April 06, 2015
Unknown
Tatizo
la ajira ni kilio cha vijana wengi TZ, watu wanalalamika kwamba
wamesoma lakini hawajaajiriwa.. unadhani hili liko BONGO pekeake?
Jamaa mmoja Uingereza, Huw Davies ana degree ambayo ameipata mwaka 2002 baada ya kusoma Chuo cha Glamorgan, lakini toka amemaliza mpaka leo hii amekuwa anatafuta kazi.. ni kwamba hajaajiriwa mpaka leo.
April 06, 2015
Unknown
Jina la staa wa kike anayefanya poa kwenye BONGO FLEVA sasa hivi, Vanessa Mdee aka Vee Money limeendelea kuonekana kwenye HEADLINES za events kubwa mtu wangu.
Jina lake lilipanda juu zaidi na wengi wakamjua nje ya East Africa baada ya kuchukua tuzo ya msanii wa kike East Africa ambayo aliipata mwaka 2014 Nigeria.
Saturday, April 4
April 04, 2015
Unknown
Mtandao wa Bongo5.com umepata nafasi ya kupokea pichaz Exclusive kutoka kwenye harusi hii ambayo imefungwa kwenye ardhi ya nchi ya Mauritius kwenye mwisho wa mwezi March 2015.
Hii ndoa pia ilishuhudiwa na watoto wao wawili mapacha kama wanavyoonekana kwenye picha pamoja na marafiki wengine wa familia pamoja na ndugu ambao idadi yao inafikia 50.
Ndoa imefungwa miezi minne baada ya Reginald Mengi kumchumbia Jacky Dubai kwenye siku ya kuzaliwa ya mrembo huyu December 2014.
April 04, 2015
Unknown
Ukwasi wa Kiongozi Mkuu wa Chama Cha Alliance for Change and Transparency(ACT Wazalendo), Zitto Kabwe umeongezeka kutoka umiliki wa shamba moja na Sh milioni 30 alizokuwa amezihifadhi katika akaunti za benki mbili tofauti hapa nchini, na sasa anamiliki mali na fedha zinazofikia Sh milioni 690.
Kwa mujibu wa taarifa hizo mpya alizoziweka hadharani wiki hii katika
fomu maalum ya kuonyesha mali zinazomilikiwa na viongozi wa chama
hicho, Zitto ametanabaisha kuwa kwa sasa anamiliki nyumba mbili.
Nyumba hizo, moja ina thamani ya Sh milioni 180 na nyingine Sh
milioni 43, Pia anamiliki kitalu cha ekari 12 ambacho kinathamani ya Sh
milioni 25, vyote vikiwa Mwandiga mkoani Kigoma.
April 04, 2015
Unknown
Mtanzania mmoja ambaye hajafahamika amekamatwa kuhusiana na shambulio la kigaidi katika Chuo Kikuu cha Garissa, Kenya.
Taarifa zilizopatikana jana usiku na kutangazwa na Shirika la
Utangazaji la Uingereza (BBC), zilieleza kuwa Mtanzania huyo anahojiwa
kuwapo kwake katika eneo hilo hasa ikizingatiwa kwamba siyo mwanafunzi
wala mtumishi katika chuo hicho.
April 04, 2015
Unknown
Katika hali isiyo ya kawaida, Polisi wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) wakiwa na mbwa nane, waliweka doria katika Kanisa la Mtakatifu Joseph jijini Dar es Salaam wakati wa ibada ya Ijumaa Kuu iliyofanyika jana.
Ibada hiyo iliyoanza saa tisa jioni iliongozwa na Paroko wa Kanisa hilo,
Audax Kaasa na Mwadhama Kardinali Polycarp Pengo aliyetarajiwa
kuiendesha kama ratiba ya Baraza la Maaskofu Tanzania (TEC) ilivyoeleza,
lakini hakufanya hivyo bali alisali kama muumini wa kawaida.
Gari ya polisi yenye namba PT 0964 iliegeshwa karibu na lango kuu la
kuingilia kanisani humo, huku mbwa kadhaa wakizunguka katika maeneo
mengine kuangalia usalama na baadaye waliingizwa katika gari hilo.
April 04, 2015
Unknown
Juzi, magaidi wa Al-Shabaab walifanya shambulio
kubwa la ugaidi katika mji wa Garisa, uliopo mpakani mwa Kenya na
Somalia.Shambulio hilo limepelekea vifo vya watu takriban 150 huku
taarifa mbalimbali zikionyesha uwezekano wa kuwepo idadi kubwa zaidi ya
waliouawa.
Awali, nilikuwa upande wa watetezi wa serikali ya Kenya na vyombo vya
usalama vya nchi hiyo katika lawama kwamba walizembea kuchukua
tahadhari.
Hoja yangu kuu ilikuwa kwamba kupewa taarifa kuhusu ugaidi ni kitu kimoja, kuweza kuzifanyia kazi taarifa hizo na kuweza kuzuia ugaidi ni kitu kingine kabisa.
Hata hivyo, utetezi huo umepungua baada ya kupatikana taarifa mbalimbali zinazoashiria mapungufu makubwa ya serikali ya Kenya na taasisi za Usalama nchini humo kukabiliana na tetesi walizopewa kuhusu uwezekano wa shambulio hilo la kigaidi.
Hoja yangu kuu ilikuwa kwamba kupewa taarifa kuhusu ugaidi ni kitu kimoja, kuweza kuzifanyia kazi taarifa hizo na kuweza kuzuia ugaidi ni kitu kingine kabisa.
Hata hivyo, utetezi huo umepungua baada ya kupatikana taarifa mbalimbali zinazoashiria mapungufu makubwa ya serikali ya Kenya na taasisi za Usalama nchini humo kukabiliana na tetesi walizopewa kuhusu uwezekano wa shambulio hilo la kigaidi.
April 04, 2015
Unknown
Mtandao wa waandishi kupitia mitandao nchini, Tanzania Bloggers Network (TBN) tunamuomba Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. Jakaya Mrisho Kikwete kutumia mamlaka yake vyema kwa kutokupitisha muswada wa Sheria ya Makosa ya Mtandao, 2015 unaokandamiza uhuru wa mawasiliano mitandaoni.
Muswada
wa sheria ya makosa ya Mtandaoni unaainisha makosa yanayohusiana na
matumizi ya mfumo wa kompyuta na Teknolojia ya Habari na Mawasiliano, na
kuweka utaratibu wa upelelezi, ukusanyaji na matumizi ya ushahidi wa
kieletroniki na masuala mengine yanayohusiana na hayo.
Muswada Wa Sheria Ya Makosa Ya Mtandaoni,2015
Umoja
huu (TBN) ulishtushwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
kukubali kupitisha Muswada wa Sheria ya Makosa ya Mtandao 2015 kwa hati
ya dharura kitendo ambacho hakikutarajiwa kutokana na kuwa mitandao bado
ni kitu kipya nchini hivyo tulihitaji maridhiano na wadau na elimu kati
ya raia na Serikali ili wengi watambue yapi ni makosa kwa kutumia
mitandao na yapi yanakubalika
Friday, April 3
April 03, 2015
Unknown
Moja ya ishu zilizojadiliwa Bungeni
katika vikao vilivyofanyika ndani ya wiki hii ni suala la kelele ndani
ya Miji Mikubwa TZ kam vile Dar.. Wabunge wakasema
ikiwezekana kuwepo utaratibu wa kufungia kumbi za sherehe ambazo
zinaongoza kwa kupiga muziki na kusababisha kero ya kelele.
Nimepita mitandaoni nikakuta hii list mtu wangu.. Hapa ni Miji mikubwa mitano inayoongoza kwa kelele Marekani.
Subscribe to:
Posts (Atom)