Sunday, June 29

wedding2
Wapenzi wa muda mrefu Richard Laslett na Collin Gunther ambao wamedumu kwenye mahusiano kwa muda wa miaka 37 wamepata nafasi ya kuwa moja kati ya wapenzi wa jinsia moja 115 waliofungishwa ndoa kwa wakati mmoja mjini Toronto, Canada.

weddind
Ndoa hizo zimefungwa kwa pamoja na kuwakutanisha wapenzi wa jinsia moja kutoka maeneo mbalimbali duniani kusherekea nguvu ya mapenzi yao.
Meya wa Toronto Norm Kelly amesema wanandoa hao wamekutana na kufurahia hatua hiyo muhimu ya kufunga pingu za maisha.
wedding3
Takribani nchi 15 duniani sasa zimeruhusu mapenzi ya jinsia moja .
lesbian





DAVID
Diamond Platinumz anaiwakilisha Tanzania kwenye tuzo za BET zitakazofanyika huko Los Angeles, Marekani
.diaa 
Jana Diamond akiwa na wasanii wenzake wanaowania tuzo katika kipengele cha International Act (Africa) walihudhuria party ya utangulizi (BET Pre Awards VIP Party).
Fally Ipupa aliungana na wasanii wanaowania kipengele kimoja na Diamond ambao ni Davido, Mafikizolo na Tiwa Savage na Sarkodie (hayupo kwenye picha hizi).
ddavidoo diamondtiwa2Mafiki zoloTIWAFally Ipupa

5
Diamond yupo L.A Marekani kwa ajili ya tukio la utoaji wa tuzo za B.E.T ambapo yupo kwenye category ya Best African Act. Hizi ni picha 6 na video moja akiwa huko Los Angeles  na kwenye hii video yupo eneo ambalo zinafanyika interview za wasanii mbalimbali.
Unaweza kumuona Buster Rhymes akiwa kwenye interview na mtangazaji mmoja na pia zamu ya Diamond ilifika kufanya mahojiano na waandishi mbalimbali.
6
1
2
3
4
7
8
9
10

An extreme body artist has taken piercing to a HOLE new level after
 creating giant flesh tunnels in his cheeks.
These pictures show how alternative model, Joel Miggler, 23, can poke his forked tongue through his CHEEKS following the dramatic piercing.
The 23-year-old, from Küssaberg, Germany, began experimenting with body modifications at the tender age of 13.
Since then he has acquired a grand total of 27 different piercings, as well as six tattoos, an implant and has even had his buttock branded.
His obsession with body modifications first began after stretching his earlobes and has now spent over £4000 altering his body.
As his piercings became more and more extreme, Joel eventually had two huge 36 millimetre holes created into the side of his cheeks but plans to eventually stretch them to 40 milimetres.

But despite his extreme look, Joel insists that his tunnels do not affect his daily life and instead simply takes smaller bites when eating.
Luckily, Joel’s mother is very supportive of his decision to change his body but he does admit that she is not too fond of his cheek tunnels.
It also seems that having huge holes in your cheeks doesn’t create any problems when it comes to his love life and has been dating an artist and body piercer for over six months.
The public’s response to Joel’s bizarre modifications seems to be pleasant overall, apart from a wave of negative response from the online community and social media channels, people either simply stare at him or occasionally stop him to ask questions.
When I walk around on the street, people only stare or sometimes ask me questions if they are interested in my jewellery.
It is only on social networks that they mostly discriminate and offend me.
My mother likes most of my modifications and she has supported my decision to look the way I do but she doesn’t think the more extreme things, like my cheeks, are very beautiful.
There is not one person or one thing that inspired me, I just enjoy playing with my body and blood.
Having my cheeks pierced was not really painful, there was a local anesthetic involved in the procedure.
My cheeks are currently 36 millimetre wide in diameter but my goal is to stretch them to 40 millimetres

KES HICHI KILICHOMTOKEA HUYU MCHUNGAJI SIDHANI KAMA ATARUDIA TENA, NA HII NI FUNDISHO KWA WENGINE

Tumekwisha! Mzee wa kanisa la kiroho (jina linahifadhiwa kwa sasa), aliyetajwa kwa jina la Luca Pesa, mkazi wa Segerea, Dar, ameaibika baada ya kukurupushwa kwenye nyumba ya kulala wageni (gesti) akidaiwa kutaka kuvunja amri ya sita na binti ambaye ni msanii chipukizi wa filamu za Kibongo, Debora Jacob, Ijumaa lina kisanga cha aina yakeMzee wa kanisa la kiroho aliyetajwa kwa jina la Luca Pesa,

HABARI KAMILI
Tukio hilo ambalo kamwe Luca hawezi kulisahahu maishani mwake, lilijiri kwenye gesti hiyo iliyopo karibu na Kituo Kikuu cha Mabasi cha Segerea, Dar, Jumanne iliyopita huku mzee huyo akishushiwa tuhuma nzito ya rushwa ya ngono kwa vibinti chini ya miaka 18.

Katika tukio hilo, mzee huyo wa kanisa na msanii huyo wa Kundi la Maigizo la Vivif lenye maskani yake maeneo hayo walikuwa wamejichimbia kwenye gesti hiyo katika chumba ambacho mlangoni kilikuwa kimeandikwa Rombo kabla ya kuchomolewa na kufikishwa kanisani kisha polisi.
TUHUMA NZITO
Timu ya Oparesheni Fichua Maovu (OFM) ya Global Publishers, ikiwa kwenye mingo zake, ilipokea simu kutoka kwa dada aliyejitambulisha kwa jina moja la Diana na kujieleza kuwa anatoka kundi la sanaa za maigizo la Vivif lililopo Segerea jijini Dar.

OFM: Ndiyo hujakosea unazungumza na 
OFM, tukusaidie nini?
Diana: Kuna mzee wa kanisa la kiroho la (anataja jina la kanisa hilo) lililopo maeneo ya Segerea, aliomba kuwa mfadhili wa kundi letu.

Akiwa kwenye geti la kanisa.
Tulimkubalia na baada ya muda alianza kutumia fedha zake vibaya kwa kufanya vitendo visivyofaa.
OFM: Vitendo gani visivyofaa? 
Diana: Anawarubuni mabinti wadogo anawaweka kambini na kula nao tunda tamtam eti ndiyo tiketi ya kuchezeshwa kwenye maigizo.
OFM: Tiririka!

Diana: Yaani hadi muda huu ninapozungumza na ninyi mzee huyo wa kanisa anachati na msanii mwingine wa kundi hilo. Anaitwa Debora anataka waende kwenye gesti fulani wakanogeshane, wahini tayari mtego umewekwa utafyatuka muda wowote.
UDHALILISHWAJI?
Diana alisema baada ya Debora kuombwa ‘mambo’ ndipo akawataarifu wasanii wenzake na kuwataka wote kwa pamoja waungane kuikomesha tabia hiyo chafu ya Luca anayelichafua kanisa la kiroho na kulidhalilisha kundi lao la sanaa.

OFM MZIGONI
Baada ya kuseti kila kitu, Diana aliiomba OFM iambatane nao kwani muda huo tayari Debora alishatangulia kwenye gesti hiyo kumfuata mzee huyo wa kanisa ambaye alishachukua chumba.

.....akitaitiwa.
Taarifa hiyo ilipokelewa kwa mikono miwili na kiongozi wa OFM ambaye aliwaagiza vijana wake makini ambao walisitisha kazi nyingine za kiintelijensia kisha kuelekeza nguvu zao eneo la tukio.
Vijana hao walitumia pikipiki zao ziendazo kasi ambapo baada ya muda usiozidi dakika ishirini walikuwa wamefika kwenye gesti hiyo.

ENEO LA TUKIO
OFM walipofika eneo la tukio, walikuta kundi la wasanii hao wakimchomoa gesti mzee huyo wa kanisa ambaye aliruka ukuta na kudondokea kwenye matuta ya viazi.

Akiwa anajizoazoa kwenye matuta hayo, kundi la wasanii hao lilimuunganishia ambapo kabla ya kumnasa aliingia kwenye chumba cha nyumba iliyopo jirani na gesti hiyo ili kujisalimisha.
Hata hivyo, zoezi lake lilifeli baada ya wasanii hao kumtahadhalisha mwenye nyumba hiyo kuwa wanamtaka mtuhumiwa wao la sivyo wangeichoma moto.

Baada ya kuzingirwa na wasanii hao huku akihatarisha maisha yake kwa kuwa wasanii hao walikuwa na hasira, aliona yasiwe makuu akaamua kuwaruhusu wamtoe mtuhumiwa wao wakamalizane naye kanisani.
KABANG!
Alipotiwa mikononi, mzee huyo wa kanisa aliomba apelekwe kanisani ambapo hapakuwa mbali na eneo la tukio ili akahifadhi vitu vyake muhimu pamoja na kuomba ushauri.

APELEKWA MSOBEMSOBE KANISANI
Kundi hilo la wasanii lilimpeleka kanisani msobemsobe ambapo baada ya hatua kadhaa polisi walitokea na kuwadhibiti wananchi wenye hasira na wasanii waliotaka kumdhuru mzee huyo wa kanisa wakati akipelekwa kanisani.

Mtuhumiwa akitembezwa mtaani.
MTAANI WERAAA!
Wakiwa mitaani, njiani mabinti walikuwa wakipiga kelele ‘weraaa…ukomeee…’ huku wakifurahia kufunga mitaa kwa madai kwamba mzee huyo wa kanisa alizidi.
Katika sekeseke hilo, polisi hao walimtia pingu mzee huyo wa kanisa na kuongoza safari ya kuelekea kanisani.

Wakiwa kanisani hapo polisi walijitambulisha na kuwauliza wachungaji pamoja na waumini wa kanisa hilo kama walimfahamu mzee huyo wa kanisa.
BREKI YA KWANZA POLISI
Kundi la wazee pamoja na vijana wa kanisa hilo walikiri kuwa Luca ni mmoja wa wazee wa kanisa hilo ndipo polisi hao wakamruhusu kuwakabidhi baadhi ya vitu vyake ikiwemo simu na fedha kisha breki ya kwanza ikawa Kituo cha Polisi cha Tabata-Shule ambapo alifunguliwa jalada la kesi namba RB/3843/2014 -RUSHWA YA NGONO, KUWAWEKA KAMBI KINYUME CHA SHERIA WASICHANA WENYE UMRI CHINI YA MIAKA 18 NA KUWADHALILISHA KIJINSIA.

Thursday, June 26

Star: Lionel Messi (above) hit a brilliant double to help Argentina defeat Nigeria
Nyota: Lionel Messi (juu) aliifungia mabao mawili Argentina dhidi ya Nigeria.
TIMU ya Taifa ya Nigeria maarufu kama Super Eagles imefanikiwa kufuzu hatua ya 16 ya kombe la dunia licha ya kufungwa mabao 3-2 dhidi ya Argentina.
Mshambuliaji hatari wa kikosi cha Alejandro Sabella, Lionel Messi amefunga mabao mawili katika dakika ya 3 na 45  katika ushindi uliowapa Argentina ushindi wa asilimia 100 katika kundi lao la F.
Bao la tatu la Argentina limefungwa na Marcos Rojo katika dakika ya 50.
Mabao mawili ya Nigeria yamefungwa na Ahmed Musa katika dakika ya 4 na 47.
Katika michuano ya mwaka huu, dhahiri, Argentina inamtegemea zaidi Messi katika mechi zake.
Baada ya kufunga mabao hayo, kocha Sabella alimpumzisha nyota huyu wa FC Barcelona kwa ajili ya mikikimikiki ya hatua ya 16.
Pia Sabella alishuhudia mshambuliaji wake, Sergio Kun Aguero akitolewa nje ya uwanja kwa kile kilichoonekana kupata maumivu ya misuli tena.
Main man: Messi (right) put his side into a 1-0 with this strike after just three minutes
Thank you: Messi points to the sky in celebration after his first goal of the game
Asante mungu: Messi akinyosha vidole kama ishara ya kumshukuru mungu baada ya kufunga .


Hapa chini ni vikosi vya timu zote na viwango vya wachezaji. Alama ni chini ya 10.
Kikosi cha Argentina (4-3-3): Romero 7; Zabaleta 6, Federico Fernandez 5, Garay 5, Rojo 6; Gago 7, Mascherano 6, Di Maria 8; Messi 9 (Alvarez 19 6), Higuain 6 (Biglia 90 6), Aguero 6 (Lavezzi 37 7). 
Wachezaji wa akiba ambao hawakucheza: Orion, Campagnaro, Perez, Maxi Rodriguez, Augusto Fernandez, Demichelis, Palacio, Basanta, Andujar.
Wafungaji wa bao: Messi 3, 45', Rojo 50'
Kocha: A Sabella 6
Kikosi cha Nigeria (4-5-1): Enyeama 7; Ambrose 6, Yobo 6, Oshaniwa 5, Omeruo 6; Odemwingie 6 (Nwofor 80 6), Onazi 6, Mikel 6, Babatunde 7 (Uchebo 66 6), Musa 8; Emenike 7.
Wachezaji wa akiba ambao hawakucheza: Ejide, Uzoenyi, Gabriel, Egwuekwe, Odunlami, Oboabona, Azeez, Ameobi, Agbim.
Mchezaji bora wa mechi: Messi
Kocha: S Keshi 7
Kadi ya njano: Omeruo, Oshaniwa

Mfungaji wa mabao: Musa 4', 47'
Mwamuzi: Nicola Rizzoli
*Viwango vya wachezaji na MATT LAWTON katika uwanja Porto Alegre
Jubilant: Messi (left), Di Maria (centre) and Marcos Rojo celebrate the opening goal
Double: Ahmed Musa (left) grabbed his first World Cup brace to give Nigeria hope
 Ahmed Musa (kushoto) alifunga mabao mawili katika mchezo wa leo.
Happy family: Musa ran towards the bench to enjoy his second goal with his team-mates

Kamanda wa Polisi wa Kanda hiyo,Kamisha Suleiman Kova


Kanisa Katoliki Parokia ya Makoka limefichua siri kuhusu mauaji ya Sista Cresensia Kapuli (50), aliyeuawa na majambazi kwa kupigwa risasi kwamba alifikwa na mauti hayo wakati akitoka benki kuweka fedha za sadaka ziliyopatikana Jumapili iliyopita.

Mwenyekiti wa Parokia hiyo, John Bosco Komba, aliliambia NIPASHE jana kuwa sista huyo aliuawa baada ya kutoka benki ya CRDB tawi la Mlimani City kuweka fedha za sadaka na makusanyo ya Shule ya Sekondari ya Mwenyeheri Anuarite.

“Taarifa zilizoripotiwa na vyombo vya habari kwamba ameporwa fedha zinaweza zisiwe na uhakika sana kwa sababu alitoka benki kuweka fedha za makusanyo ya sadaka, ndipo akapitia kununua mchele zaidi ya kilo mbili kwa ajili ya matumizi ya nyumbani kwa hiyo hakuwa na fedha nyingi kama inavyoelezwa na watu,” alisema.
Komba alisema Sista Kapuli mbali na kuwa mhasibu wa shule,pia alikuwa mhasibu wa Kanisa Katoliki Parokia ya Makoka na kwamba siku ya tukio alikuwa na mwenzake Sista Brigitha ambaye ni Mwalimu Mkuu msaidi wa Shule ya Sekondari Mwenyeheri inayomilikiwa na kanisa hilo.
Alisema walipofika katika duka walilokwenda kununua mchele Sista Brigitha ndiye aliyetelemka kwenye gari kwenda kununua na ndipo ghafla majambazi wawili waliokuwa katika pikipiki walitokea na kupiga risasi moja iliyovunja kioo cha gari ambayo ilimjeruhi dereva wa gari hilo, Mark Patrick Mwarabu. 
Aliongeza kuwa majambazi hao walidhani kuwa mkoba aliokuwa nao ulikuwa na fedha nyingi walimpiga risasi mbili Sista Kapuli eneo la titi upande wa kushoto na kufa papo hapo.
Alisema madaktari wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) wataufanyia uchunguzi mwili wa Sista Kapuli leo kwa ajili ya kumuondoa risasi kabla ya taratibu za kuusafirisha mwili huo kuupeleka kwao katika kijiji cha Mkulwe wilayani Mbozi, mkoani Mbeya.
Alisema baada ya taratibu za uchunguzi wa mwili huo kufanyika, kesho mwili utapelekwa katika Kanisa la Makoka kwa ajili ya misa na kuuaga na safari ya kuusafirisha kwenda kijijini kwao wilaya ya Mbozi itaanza huku akisema kifo hicho kimewasikitisha.
Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, limetangaza kuanza kwa msako ili kuwabaini na kuwakamata majambazi waliohusika katika tukio hilo.
Kamanda wa Polisi wa Kanda hiyo, Kamisha Suleiman Kova, alisema jana kuwa Jeshi lake limeandaa operesheni maalumu itakayohusisha vikosi tofauti ili kuwatia mbaroni wahalifu hao, ambao alisema walipora Sh. milioni 20

Unaweza kuamini ukiambiwa kuwa, umaarufu hapa Bongo unakuja na rangi yake ya kipekee, hata kwa watu wanaochipukia na kutamani kuwa maarufu siku moja, wanaamini kuwa, ili kufanikiwa ni lazima kwanza uwe na rangi nyeupe ya ngozi yako, huwezi kushangaa kwa hili sababu hata Lupita Nyong’o pamoja na kufanikiwa kuwa mwanamke mwenye mvuto mwaka 2014, naye alikuwa anaamini hilo alivyokuwa mdogo.Hapa kwetu Bongo imekuwa kama ugonjwa vile wa kuambukizwa kati ya watu maarufu na hata wale wanaochipukia, kujikuta wanatumia kila hali kubadilisha ngozi yao, wapo wasanii wengi sana na watu maarufu, ambao hutoweza amini uonapo  jinsi walivyokuwa hapo nyuma na hivi sasa wanavyoneka, kama ulikuwa hujui hili ni kwamba endapo mtu akibadilika namna hii, ni vigumu kabisa kurudi hali yake ya zamani ya uhalisia.
Watu Wengi maarufu wamejikuta wakijutia kujibadili haswa pale miaka inavyozidi kwenda, kutokana na madhara yanayo wakumba kwenye ngozi zao hizo, kwa asilimia kubwa madhara yake yanatibika, ila pesa yake ya matibabu ni ndefu, jambo ambalo ni cost kubwa sana kuanza kujitibu ni bora kujiepusha kabisa na mambo hayo ya urembo wa muda.Hizi ni baadh tu ya picha za wasanii wetu wa hapa Tzee ambao hutoweza amini jinsi walivyobadilika, kabla na baada ya kupata umaarufu.
Wema Sepetu.
collmxmage
Ray-C.

collxage

Diva Loveness.
collagdjse

Monday, June 23


Habari njema kwa wote waliopata mwaliko wa kuhudhuria siku ya utoaji tuzo za watu, June 27 kuwa watapata fursa ya kuiona kwa mara ya kwanza video mpya ya Ben Pol, ya wimbo wake ‘Unachora’ aliomshirikisha Joh Makini. Video hiyo imeongozwa na nominee wa kipengele cha muongozaji wa video zinazopendwa kwenye tuzo hizo, Nisher. Ben Pol pia anawania kipengele cha video ya muziki inayopendwa ya mwanamuziki wa kiume kwa video yake ‘Jikubali’.

Sunday, June 22

20140622-122832-44912263.jpg
Timu ya taifa ya Nigeria ‘Super Eagles’ jana iliweka rekodi mpya katika michuano ya kombe la dunia, baada ya ushindi dhidi ya Bosnia.
Super Eagles jana walipata ushindi wa kwanza kwenye michuano hiyo tangu mashindano ya mwaka 1998 yaliyofanyika Ufaransa.
Goli pekee la mshambuliaji wa Stoke City Peter Odemwingie lilivunja mkosi wa kutokushinda mechi kwa Nigeria katika kipindi cha miaka 16 iliyopita.
Nigeria sasa wamefikisha pointi 4 wakishika nafasi ya pili nyuma ya Argentina ambao tayari wameshafuzu.
Mechi za mwisho ya kundi hilo zitakazowakutanisha Nigeria vs Argentina na Iran vs Bosnia ndio zitaamua timu gani itakayoungana na Argentina kwenda kwenye hatua ya pili ya michuano hiyo
Siku moja baada ya kutangaza kuondoka Hot 97, Radio Personality kutoka New York, Angie Martinez  anaungana na Clear Chanel Media - kampuni mama ya Power 105.1 iliyopo New York na The Beat 103.5 iliyoko Miami.
Martinez alikuwa ni mkongwe wa Hot 97 kwa zidi ya miaka 20, ambapo kwa sasa ataungana na Angle Yee, Charlamagne Tha God, DJ Envy, DJ Clue, and DJ Prostyle kupitia 105, na atakuwa aki-host kipindi cha mchana kupitia Power na The Beat.

"Welcome @angiemartinez the “Voice of New York” to @Power1051 !
— The Breakfast Club (@breakfastclubam) June 19, 2014
Martinez ameelezea furaha yake kuungana na kituo hicho kwa kuandika
“I am excited to join Power 105.1 in New York and The Beat in Miami and expand my brand even further in the coming months,” amesema Martinez kwenye statement yake.
Mara baada ya ku- resign Martinez aliandika hili kupitia post yake ya Instagram
"Today I resigned from HOT97,” the radio personalitywrote in a post on her Instagram account. "I am grateful to the Emmis family for my time with the company and the immeasurable way that it has shaped my life. We made history together in so many ways and I will cherish those memories and my friendships forever. This was one of the toughest decisions I've ever had to make but ultimately it is time to move on, to grow and to be challenged in new ways. Saying goodbye is always emotional and bitter sweet but I am extremely excited about the future. Thank you HOT97 and most importantly....the listeners... for an unimaginable journey. Today will be my last show stay tuned.... Love, angie”
-