He trusts lions enough to stick his arm in their mouth! |
YANGA
SC imetoa onyo kwa wapinzani wao katika Ligi ya Mabingwa Afrika mwezi
ujao, Al Ahly ya Misri baada ya kuifumua mabao 7-0 Ruvu Shooting ya
Pwani katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara Uwanja wa
Taifa, Dar es Salaam jioni hii.
Ushindi
huo unaifanya Yanga SC irejee kileleni mwa Ligi Kuu baada ya kutimiza
pointi 38, mbili zaidi ya Azam inayoangukia nafasi ya pili sasa, ambayo
kesho itamenyana na Prisons ya Mbeya Uwanja wa Azam Complex, Chamazi,
Dar es Salaam.
Wawili wabaya; Emmanuel Okwi kulia na Mrisho Ngassa wakishangilia baada ya bao la nne leo na chini Kavumbangu anapongezwa baada ya kufunga moja ya mabao yake |