Tuesday, April 3


 
THE HIDDEN POWER.!!
By Malisa GJ,
Mwaka 1836 binti mmoja aliyekuwa na umri wa miaka 18 kutoka familia ya kitajiri huko Lexington, Kentucky alimuomba Mungu aolewe na Rais wa Marekani. Licha ya kwamba utajiri wa familia yao ulitokana na biashara ya utumwa lakini wazazi wake waliamua kuachana na biashara hiyo mwanzoni mwa miaka ya 1800's na kuwa wacha Mungu.
Mary alikuwa muumini wa makanisa ya uamsho kwa wakati huo (Presbyterianism), kama ilivyo makanisa ya kiroho leo. Siku moja akamwabia baba yake, "Mungu ameniambia kuwa mwanaume wa maisha yangu atakuwa Rais wa nchi hii".
Baba yake akastaajabu, lakini hakutaka kumkatisha tamaa. Akamwambia "binti yangu, nchi hii ni kubwa sana, na wasichana wengi wangependa kuolewa na watu mashuhuri na wenye madaraka, lakini si jambo rahisi kuolewa na Rais. Na ukisubiri hali hiyo kutokea unaweza usiolewe kabisa katika maisha yako".
Lakini yule msichana akamtizama baba yake kisha akamjibu "sijali ni wasichana wangapi wanaotamani kuolewa na watu mashuhuri, sijali nchi hii ni kubwa kiasi gani. Ninachojali ni kuwa Mungu ameniambia kuwa siku moja nitakuwa first lady wa nchi hii. Hilo tu"
Maka mmoja baadae (1837) yule binti akachumbiwa na mwanasiasa machachari chipukizi aliyekuwa mwanasheria na mbunge wa Illinois (the rising young lawyer and Democratic Party politician) aitwaye Stephen Douglas. Kwa kuwa Stephen alikuwa mbunge, baba wa yule binti aliamini kuwa huyo ndiye angemuoa mwanae na angekuja kuwa Rais wa Marekani baadae. Kwahiyo ndoto za binti yake zingetimia kupitia Stephen.
Lakini miaka miwili baadae (1839) uchumba wao ukavunjika.
Mwaka huohuo (1839) katika mji wa Springfield, Illinois, yule binti akakutana na kijana mmoja msomi wa sheria lakini kutoka familia maskini huko Indiana. Kijana huyu alikuwa amekuja Illinois kutafuta kazi. Wazazi wake walikua wakulima maskini. Ardhi yao huko Kentucky ilitaifishwa na hivyo wakahamia Indiana.
Kijana huyu akapendana na yule binti na kuamua kuoana. Mwaka 1840 mwezi December kijana akamvisha pete ya uchumba yule binti. Baba wa binti hakufurahishwa. Akajiuliza iweje mwanae amkatae "mbunge" na akubali kuolewa na "mtoto wa mkulima??". Kwa masikitiko akamuuliza binti yake "unakumbuka ahadi ya Mungu kwako?". Binti akajibu "hata sasa bado naamini."
Miaka minne baadae (1843) wakafunga ndoa.
Miaka 17 baadae (1861) yule kijana akachaguliwa kuwa Rais wa 16 wa Marekani. Jina lake aliitwa Abraham Lincoln, na mkewe aliitwa Mary Todd Lincoln.
Mary ndiye aliyekataa kuolewa na Steven Douglas (Mbunge) kwa ajili ya Lincoln (mtoto wa mkulima).
Baba yake Marry akiwa mzee wa zaidi ya miaka 80 alishuhudia mwanae akiwa "First Lady" akamwambia "Mungu wako ni mkuu sana. Aliahidi na ametimiza". Mwaka mmoja baadae (1862) mzee Robert Todd (baba yake Mary) akafariki.
MORAL OF YHE STORY.!
Hadithi hii ni ya kweli kabisa inayomhusu Rais Abraham Lincoln na mkewe Mary Todd Lincoln. Kuna mengi ya kujifunza kwenye kisa hiki, lakini ningependa kukushirikisha machache niliyojifunza mimi.
#Lesson_1: Ukiomba usichoke kusubiri. Mungu akisema atakupa, basi amini atakupa tu. Mungu wetu ni mwaminifu na hutupa kwa wakati wake. Mary aliona maono ya kuwa first lady akiwa na miaka 18, lakini ilimchukua robo karne (miaka 25) hadi maono yake kutimia. Sasa wewe ndugu yangu umemaliza chuo mwaka jana umeomba kazi hata mwaka haujaisha umeshaanza kumlalamikia Mungu. Subiri. Au umeomba mchumba mwaka wa 3 hujapata, unaanza kumlalamikia Mungu eti wenzio wote wameolewa/kuoa. Tafadhali subiri. Mungu atakupa kwa wakati wake unaofaa.
#Lesson_2: Ishi katika misimamo. Baba yake Mary Todd alipoona mwanae amemuacha "Mbunge" akaolewa na Mtoto wa mkulima alimuona kama vile amepoteza dira. Lakini binti alijua ipo siku Mungu atatenda. Na Mungu alivyo mwaminifu hakumruhusu baba yake Mary kufa kabla hajashuhudia Mwanae akiwa "first lady" wa Marekani. Point hapa ni kwamba jifunze kushikilia imani yako na uwe na msimamo usioyumba hata kama dunia nzima itakuacha. Wengi waliobarikiwa ni wenye misimamo. Jifunze kuwa focused and visionary. Usitazame vinavyong'ara leo, tazama vitakavyong'ara milele.
#Lesson_3: kuna kitu kinaitwa "Hidden Power" yani nguvu iliyofichwa. Ni nguvu ambayo unakuwa nayo wewe lakini inatokana na watu wengine. Unaweza kufanikiwa sana, lakini si kwa juhudi zako bali kwa sababu nyuma yako kuna watu wanaofanya wewe ufanikiwe. Wanakuombea, wanafunga kwa ajili yako, wanamsihi Mungu kwa ajili yako, wanaomba ulinzi, baraka, na neema kwako. Wanaweza kuwa wazazi wako, mwenzi wako, watoto wako, rafiki zako, ndugu zako etc.
Lincoln alikuwa na nguvu iliyofichwa kupitia mkewe. Yani mke wa Lincoln (Mary) ndiye aliyemfanya mumewe kuwa Rais. Kama Lincoln asingemuoa Mary Todd asingekuwa Rais wa Marekani. Na hata Lincoln mwenyewe aliwahi kukiri kwamba "Urais haukuwahi kuwa ndoto zake katika maisha"
#Lesson_4: Our GOD is the GOD of imposibilities. Yale tunayoona na kudhani hayawezekani, kwa Mungu yanawezekana. Wakati Mary akiwaza atakuwa first lady wa Marekani, Lincoln hakuwahi kuwaza kama angekaa awe Rais. Sijui kama unauona ugumu huu.! Imagine Mungu anakuahidi utakua "first lady", halafu anakataa usichumbiwe na Mbunge. Anakupa mchumba mwingine, halafu huyo mchumba anakwambia "sina hata ndoto za Urais". Ingekua ni wewe ungejisikiaje? Wengine mngemlaumu Mungu na kutamani kurudi kwa mbunge, right? Lakini Mungu akiahidi ni lazima atimize.
#Lesson_5: Mungu huinua vyenye nguvu katikati ya vinyonge. Unakumbuka hadithi ya Daudi? Yesse alipoambiwa aite watoto wake wote maana mmoja wao atakua Mfalme, aliita wote akamsahau Daudi. Imagine baba yako mzazi anakusahau. Lakini Mungu akamfanya huyohuyo mdogo, mnyonge, aliyesahaulika kuwa Mfalme. Lincoln nae pengine alionekana mnyonge, lakini Mungu akasema "huyu ndiye"
Katika maisha usimdharau mtu yoyote. Heshimu kila mmoja. Unayemdharau leo aweza kuinuliwa kesho ukabaki unashangaa. Ipo nguvu iliyofichwa (the hidden power) kwa kila mmoja wetu. Unaweza usiione nguvu hiyo leo lakini ipo siku itafanya kazi.
The hidden power.!!!

Thursday, January 18

IMG_20180117_150710.jpg

Kuanzia mwaka 1952 mpaka mwaka 1963 Isser Harel alipata kuwa boss mkuu wa mashirika yote Shin Bet (idara ya usalama wa ndani ya nchi) pamoja na Mossad (idara ya ujasusi wa nje ya nchi). Mwanzoni mwa mwaka 1963, alipata mbadala wake, aliyeitwa Meir Amit. Kwa siku za mwanzoni Meir Amit alikuwa hakubaliki sana na majasusi wa mossad waliokuwa watiifu kwa Harel, ila baada ya mwanzo mgumu, ulioanza kwa kukosa ushirikiano na uaminifu, alifanikiwa kujenga ushawishi katika uongozi wake ndani ya taasisi (MOSSAD)

Hata wale ambao hapo mwanzo walipinga kwa nguvu zote yeye kuwa boss mkuu wa mossad akichukua nafasi ya Harel walianza kumuheshimu, kumkubali na kumpenda. Meir Amit alifanikiwa kuja kuwa boss mahiri wa operations zote za mossad nje ya nchi. Chini ya uongozi wake pamoja na boss wa kitengo cha ujasusi cha jeshi Aharon Yariv kwenye miaka ya 1960's, idara za ujasusi za Israel zilipata mafanikio makubwa sana na ya kukumbukwa. Moja kati ya mafanikio haya ilikuwa ni ushindi wa Vita ya siku sita mnamo mwezi wa juni mwaka 1967 pamoja na wizi wa ndege za kivita iliyotengenezwa nchini Soviet Mig-21. Punde tu baada ya kutwaa u boss wa mossad mwaka 1963, Meir Amit aliomba ushauri wa mawazo kutoka kwa viongozi wa ngazi za juu wa kijeshi ili kuweza kumsaidia kuunda malengo makuu ya mossad, na kuwauliza ni yapi wanahisi mossad inaweza kuchangia katika ulinzi wa taifa la Israel. Jenerali Mordecai (Motti) kamanda wa kikosi cha anga cha jeshi la Israel mwaka 1963 alimwambia afanye juu chini wailete ndege ya kisasa kwa wakati huo (Mig-21) katika ardi ya Israel.

Ni ngumu sana kufahamu kama Motti aliamini kuwa mission kama hiyo inaweza kutekelezeka. Ezer Weizmann, ambaye alikuja kuwa kamanda wa jeshi la anga kutoka kwa Hod, alipata kumwambia Hamit kitu hicho hicho punde tu kabla ya vita ile ya siku sita. Kama ingewezekana
========
Mkasa ndio unaanza sasa.......
Mikoyan - Guverich almaarufu kama Mig-21 ni moja kati ya ndege za kisasa zaidi zinazokimbia kwa kasi kuzidi sauti kuruka kutoka nje ya anga la USSR. Bado inashikilia rekodi ya kuwa ndege iliyotengenezwa kwa wingi zaidi katika historia ya tasnia ya uundaji wa ndege za kasi, na imetumiwa na takribani nchi 60 na katika mabara manne. Sifa kubwa ya ndege hii ni kwamba ilikuwa na uwezo wa kubebeshwa makombora mazito na ya masafa marefu.

Kati kati ya miaka ya 1960, Mig 21 ilitumiwa kwa wingi sana na nchi za mashariki ya kati katika mogogoro yao. Vikosi vya anga vya nchi kama Misri, Syria pamoja na Iraq walitumia saaanaa ndege hizi hususan kwa mashambulizi dhidi ya wayahudi.

Kwa kipindi cha muda mrefu sana jeshi la anga la Israel lilipambana kupata kwa kuiba ndege hii ya Mig 21 ili kuweza kudadavua uwezo wake katika uwanja wa vita pamoja na udhaifu wake pamoja na kupata kujua ni mbinu gani hutumika na majeshi ya adui katika kupambana wakiwa na ndege ya aina hii.

Idara ya ujasusi ya taifa hilo la kiyahudi (mossad) walipewa jukumu zito sana la kuipata ndege hiyo kwa udi na uvumba katika mpango wa siri sana uliojulikana kama "operation diamond"

Katika jaribio lake la kwanza, jasusi wa mossad aliyejulikana kama Jean Thomas aliyeishi nchini Misri alipokea amri ya kutafuta rubai ambaye angekuwa tayari kutoroka na ndege na kuipeleka Israel kwa kuhongwa kiasi cha pesa cha karibia dola milioni moja za wakati huo mwaka 1966. Mission hii haikufanikiwa kwa vile rubani yule wa ndege za jeshi la anga la misri alitoa taarifa mapema kwa vyombo vya usalama vya nchi yake mpaka ikapelekea Thomas kukamatwa na kushitakiwa kwa makosa ya kufanya upelelezi ndani ya ardhi ya Misri.

Jaribio la pili la kuiba ndege hiyo ya Mig 21 kwa safari hii lilifanyika nchini Iraq lakini pia halikufanikiwa kwa sababu mpelelezi wa mossad aliishia kupigana na marubani wawili wa jeshi la anga la Iraq wakati akijaribu kuwanyamazisha baada ya kuwa walikwisha kataa kutoa ushirikiano wa dhati katika mpango huo.

Mnamo mwaka 1964, taarifa zilipatikana kutoka kwa mjahudi mzaliwa wa Iraq zilizopelekea mossad kufahamiana na rubani aliyejulikana kama Munir Redfa ambaye alikuwa akichukizwa na ukweli kwamba yeye kuwa na background ya ukristo ndio kunakofanya washindwe kumpandhisha cheo katika jeshi la Iraq. Serikali ya Israel ilimpa redfa kiasi kikubwa sana cha pesa, uraia wa Israel kwake pamoja na familia yake pamoja na ajira ya kudumu.

Katika mkutano wa siri baina yake na maofisa wa kiyahudi uliofanyia ulaya, walipanga mikakati madhubuti ikiwa pamoja na kwenda Israel kutembelea uwanja wa ndege wa kijeshi ambao engetumika kutua ndege hiyo ya wizi.

Ilipokika tarehe 16 August mwaka 1966, Redfa alipata fursa ya kutoroka na ndege alikwa katika mazoezi ya kawaida ya kuruka, ndege ikiwa ipo na mafuta full tank jambo ambalo ilikuwa hairuhusiwi kwa ndege kujazwa mafuta fully ikiwa katika mafunzo. Ndege ilipita kaskazini mwa Jordan ikiwa katika kasi ya ajabu. Redfa alitoka kutoka katika njia kuu ya ndege kama ilivyopangwa katika mazoezi. Ndege mbili za jeshi la Jordan ziliruka kuifuata Mig 21 ambao ilikuwa ikiruka katika speed ya ajabu tena juu kabisaaa kama futi 30,000 kiasi kwamba kuikamata kwa ndege za Jordan ikawa haiwezekani. Makombora ya kutungulia ndege ya Jordan yote yalizimwa kisha Mig 21 ikavuka anga la Jordan bila utata wowote.

Ndege hii ya wizi ilipokuwa inakaribia kuingia katika anga la Israel, ilipokelewa na ndege ndogo mbili. Ndogo lakini zilikuwa na nguvu kubwa sana aina ya Mirage III za jeshi ya Israel ambazo ziliaindikiza mgeni wao kwa utaratibu kabisaa mpaka katika uwanja wa ndege za kijeshi wa Hatzor. Baadaye sana rubani mwizi Redfa alikuwa kisema hadharani kuwa alitua na ndege ikiwa na mafuta kidogo sana sana sanaaaa.

Kuibwa kwa ndege ile kulizua mijadala dunia nzima (mpaka Tanzania) huku serikali za Urusi pamoja na Iraq wakitaka ndege hiyo kurudishwa mara moja. Serikali ya Israel walikataa kata kata agizo hilo la kurudhisha ndege. Ndani ya wiki chache ndege hiyo ilirushwa tena angani katika mazoezi ya kijeshi ili kuipiganisha na ndege ya jeshi la Israel aina ya Mirage III, pamoja na kuwafunza marubani wa IDF namna ya kupambana na ndege za waarabu aina hiyo hiyo ya Mig 21 wakati wa Vita. Wakaja kugundua kwamba Mig ilikuwa ni ndege nzuri sana katika mapambano ya anga za juu sana pia ni rahisi sana kuirusha angani. Pia wakaja kugundua baadhi ya madhaifu ya ndege ile. Mig 21 ikaja kupakwa rangi ya mistari miekundu pembeni mwake ili waitofautishe na ndege za adui wakati wa mapambano na ikaja kitumika wakati wa vita vya siku sita kati ya Israel na mataifa ya kiarabu.

Baadaye pia ndege ikaja kuvunjwa vunjwa na kumong'onyolewa yooote kisha kufanyiwa analysis ya kina zaidi.

Tukio hili lilionekana ndio la mafanikio zaidi kwa mossad kwa vile walifanikiwa kuvunjavunja ndege sita za maadui aina ya Mig wakati wa Vita na Syria wakati ndege yao aina ya Mirage III ikitoka bila kuchubuka hata kidogo.

Israel wakaja wakaipeleka ndege ile marekani mwaka 1968 jambo ambalo lilipelekea marekani kuwapa Israel ndege mpya na ya kisasa aina ya Douglas F-4 Phantom.
=========
Heri ya Mwaka Mpya 2018. Si makusudi yangu kusifia Uhalifu lakini katika Ulimwengu huu kuna akili za ziada au vipaji ambavyo watu wanavyo sema tu matumizi yake ndo huwa yanakuwa ya kihalifu. wazungu wenzetu bado hukaa chini na kutathmini faida na hasara ya akili za watu flan flan hata kama walikuw awahalifu. leo hii tunamzungumzia Frank Williams Abagnale Jr ambaye baadaye FBI ilibidi wamwajiri baada ya kumkamata na kustaajabishwa na uwezo aliokuwa nao.

index.jpg
Kwa wale ambao wamewahi kutizama movie inaitwa Catch me if You Can au kusoma kitabu chenye jina hilo hilo bila shaka watakuwa wamewahi kusikia kisa cha Tapeli/Msanii mmoja mwenye akili kuwahi kupata kutokea Duniani. Huyu jamaa aliyekuwa akifahamika kwa jina la Frank W. Abagnale Jr. Akiwa na miaka 15 alianza shughuli za kufanya utapeli au usanii kiasi kwamba mama yake ilibidi mapeleke shule ya watoto watukutu. Frank alipomaliza shule aliamua kutafuta ajira hasa baada ya baba yake kuyumba kiuchumi na kusababisha awe na maisha magumu. vyuma vilikaza.

Frank aliamua kuondoka nyumbani akiwa na checkbook pamoja na Usd 200 katika account yake akielekea New York City kutafuta maisha. Akiwa huko akawa anaishi na familia ya kijana mmoja ambaye walikutana kwenye train wakati wa safari yake basi akamuuzia uzia chai wakawa marafiki na badaye akafikia kwao. Haikuchukua muda mrefu alifanikiwa kupata kazi katika kampuni moja ya stationery akitumia uzoefu alioupata aliupokuwa akifanya kazi katika kampuni ya baba yake.

Frank aligundua ilikuwa ngumu sana kuishi maisha mazuri katika jiji la new York hasa hasa ukiwa hujasoma angalau kuwa na elimu ya kwa ngazi ya Diploma. Na ili kuweza kuishi vizuri pale jijini basi alipaswa angalau aweze kupata zaidi ya Usd 1.50 kwa saa kiasi ambacho alikuwa akipata. Hivyo alianza kuchangamsha akili kuwa afanye nini ili aweze kuongeza kipato.hakuchagua kuwa punga.no. alichagua kuwa Msanii. Alifanikiwa kupata wazo ambalo lingemsaidia kupata kipato cha ziada na hivyo kusababisha miezi ikutane.

Akaamua kuchezea leseni yake ya udereva. Ambayo mara ya kwanza ilikuwa inaonesha alizaliwa mwkaa 1948 akarudisha nyuma na kuifanya ioneshe amezaliwa mwaka 1938. Miaka 10 zaidi ya umri wake.hii mbinu ilifanya kazi.watu walikuwa wakimwona ni mtu mzima kutokana na yeye kubehave na kuonekana hivyo na pia hata urefu wake wa futi 6 na mvi za urithi ambazo zilikuwa zimeanza kumtoka.basi ilikuwa ni rahisi kumdhania kuwa ni mtu mzima. Frank hakuishia hapo. Kaanza kujifanya kama ni mtu ambaye amesoma sana akijua hii ingemsaidia katika kuongeza mshahara wake. Hata hivyo aligundua hata pamoja na kufanya sarakasi zote hizo yaani za kuongeza umri na kudanganya kuhusu elimu yake bado hakuweza kupata pesa ambayo ingemsaidia kuishi maisha mazuri kama alivyokuwa ametegemea.akaamua kuchemsha tena akili.

Atafutaye hachoki. Frank alikumbuka kuwa alikuja New York akiwa na chekcbook na alipofika new York alifungua check account kupata blank checks. Akadhamiria kutumia hizo checks kwa hali ambayo ingempa faida Zaidi kuliko ambavyo ilikusudiwa.yaani kufanya usanii/utapeli.

Frank akafanya maamuzi magumu. Akaamua kuacha kazi na kuanza kufanya utapeli kwa Mabank kwa kujiandikia check feki. Alishafanya jambo hili hapo kwanza na hivyo akawa ameendeleza huu mchezo wa kujiandikia check feki na kuvuta mapene kutoka bank.akijipatika Madollar kibao. Lakini alishtuka kuwa si muda mrefu mapolisi watakuwa wanafaham mchezo wake hivyo akaamua kuondoka kwenda sehemu nyingine na kubadilisha jina.

Mpango wa Kujifanya Rubani wa Shirika kubwa la Ndege Duniani.

Abagnale_and_Stewardess.jpg
Frank W akiwa na mtoto mmoja mkali baada ya kutoka kumgegeda.

Alipata wazo la kujifanya rubani hasa baada ya kushuhudia mara nyingi marubani walivyokuwa wakipata heshima katika jamii. Alishashuhudia marubani wengi wakiwa nje ya Hotel ya Commodore wakila bata na mademu wakali wa kibongo,kitasha,kihindi,kiarabu na kilatino aka admire sana ile life style na siku zote alikuwa akiwaza maisha yale ya kula bata kwa kwenda mbele.Na akaona ili sasa aweze kuzi cash zile bad checks zake bila bugudha au kutiliwa mashaka basi inabidi ajifanye naye ni rubani. Hapo tayari alikuwa ameshaziandika cash kadhaa ambazo inabidi akazi cash.

Basi akaamua kupata sare za marubani wa Shirika la ndege la Pan Am (Pan American) na kujifanya yeye ni mmoja wa Marubai wa Panam. Akaanza kufanya mchakato mtoto wa mjini… wanasema "kuku hafi kwa utitiri "na ndivyo ilivyo kwa mtoto wa mjini hafi kwa njaa. Akampigia simu wakala wa manunuzi wa Pan American Airlines Corporate makao makuu na kuwaambia kuwa yeye ni Rubani(pilot) wa Kampuni hiyo ya Panam na kuwa katika Hotel aliyokuwa anaishi walipoteza Sare yake ya kazi. Jamaa kule wakamwambia hamna noma basi aende kuchukua hiyo sare katika Kampuni ambayo wao wame specialize katika kutengeneza uniform za Pan Am mtaa wa 5th Avenue. Naye pasipo kuchelea alifanya hivyo. Siku hiyo hiyo aliafanikiwa kupimishwa Sare na akawapa namba ya Mfanyakazi ambayo aliibuni alipokuwa akijaza form.

Hatimaye frank alitoka katika lile jengo akitabasamu kimoyo moyo akiwa ameshikiria sare yake mkononi akiwa amefanikiwa kuvuka kikwazo kimoja wapo katika mchakato wake. Ili sasa kujihakikishia nafasi ile akaamua kutengeneza na kitambulisho cha Pan Am. Baada ya kuangalia katika vile vitabu vya simu maarufu kama Yellow Pages frank aligundua kuwa 3M ndo ilikuwa Kampuni inayohusika na utengenezaji wa Vitambulisho kwa Makampuni Mengi ya Ndege ikiwepo Pan Am. Akawasiliana na kampuni hiyo akijifanya yeye ni Afsa manunuzi ambaye amedhamiria kutengeneza vitambulisho vipya kwa ajili ya Kampuni yake. Akaomba wakutane na mhusika wa 3M kwa ajili ya maongezi Zaidi. Akakutana na afsa wa Kampuni anayehusika na mauzo na huko akapewa catalogs mbalimbali za vitambulisho walivyo navyo.katika hilo akagundua kitambulisho ambacho kinafanana na vinavyotumiwa na Pan Am. Akamwambia mhusika wa ile Kampuni alitaka apewe copies za sample za vitambulisho ambacho kitawekwa picha na details zake kama mfano ili akawaoneshe wafanyakazi wenzie vitambulisho vile vitakuwaje. Kitambulisho kile kilifanana kabisa na vile vya Pan Am isipokuwa ilikosekana Logo tu.akatengenezewa akachukua akawaoneshe wafanyakazi wenzie kama alivyojinasibu kwa yule jamaa.

Frank alitatua tatizo hilo la kukosekana nembo kwa kuamua kununua mfano wa ndege ya Pan Am. Yaani toy ambapo katika hilo akanyofoa hiyo alama ambayo ni famous sana na kwa umakini akaibandika kwenye kitambulisho chake na kilionekana kama vile vile ambavyo vinatumika na maruban wa Pan Am. Kikwazo kingine akawa amekivuka. Sasa ana sare na kitambulisho. Safari yake ya kuelekea kula bata ikawa inazidi kukaribia.

Akawa amaebakiwa na maeneo mawili Zaidi ya ku clear. Alitakiwa kuwa na leseni ya FAA ambayo kila rubani anapaswa kuwa nayo na pia awe na ufahamu kuhusiana na shughuli za Airlines. Kwanza akaamua kutafuta habari nyingi kadri awezavyo kuhusiana na usafiri wa anga,urubani na pia maneno au terminologies ambazo zinatumika katika kada hii ya usafiri wa anga. Akaanza kuwa anaingia library kujisomea ingawa alikuta vitabu vingi vimekuwa outdated.lakini alijitahidi kupata ABCs za Urubani.

Akaona ili kuweza kupata habari za uhakika na za kuaminika basi aanze kufanya utaratibu wa kupata habari hiz kutoka kwa wahusika wenyewe yaani wafanyakazi na marubani.akaanza kuandaa mahojiano na wafanyakazi wa Pan Am akijifanya yeye ni mwanafunzi anayefanya research project kuhusiana na kampuni hiyo na marubani wake. Lilikuwa ni wazo bora kabisa lenye akili. Alijipatia utajiri wa habari za uhakika pamoja na ufahamu kuhusiana na sera,kanuni na taratibu kama msaidizi wa rubani. Co-pilot. Aina ya ndege zinazotumika na njia za kimataifa zinazotumika.jamaa akawa fiti sana katika eneo hilo.

Zaidi Zaidi alipata kufaham kuhusiana na deadheading. Deadheading ni mfanyakazi wa ndege ambaye anapata kipaumbele cha kusafiri kwa kutumia ndege nyingine kwenda sehemu mbalimbali bure kwa ajili ya kwenda kufanya shughuli flani. Mwajiri ndo anayelipia hii safari kwa kila kitu.hapa frank alitasabamu na kuona sasa ameuchinja.maana akiwa kama rubani pia deadheading atakuwa sometime anasafiri kwenda sehemu mbalimbali duniani kwenda kula bata akilipiwa na kampuni. Mungu ampe nini Frank? Upele? Elimu yote hii aliihifadhi kichwani mwake akiendelea kujikita Zaidi katika kukamilisha mpango wake.

Issue iliyokuwa inafuatia sasa ilikuwa ni kupata leseni ya FAA aligundua kuwa bila leseni hiyo asingeweza kujifanya yeye ni rubani.sababu wakati mwingine marubani walitakiwa kuonesha leseni ya FAA ikiwa angepanda ndege nyingine kama Staff yaani deadheading. Si unajua zile za kibongo hata kwenye daladala wakati konda akidai mchango wa mafuta utasikia “mi stafu” basi ndo na wao ili uonekane staff basi sometime utaulizwa tuoneshe leseni yako ya FAA. Frank aligundua FAA walikuwa na Branch hivyo akajiita Frank Williams na kuwa ametumwa akachukue documents za maelezo ya vitambulisho baada ya kutumiwa mail ndugu yake ambaye ni rubani. Akachukua ule mfano wa vitambulisho toka kwenye barua na vipeperushi vya FAA akaiweka kwenye printer na kuifanya iwe ndogo akaibandika kwenye karatasi maalum na kulaminate. Shabash ! frank alikuwa tayari ameshaula.huwezi amini ilikuwa copy right kama zile zile za marubani.alitabasamu tena na kurusha ngumi hewani ya kujipongeza huku akianza kufurahia jinsi ambavyo atakuwa anakula bata na watoto wakali.
6a00d8341c39e853ef015431fb2881970c-320wi.jpg
frank akiwaza amezungukwa na watoto wakali.

Frank sasa alikuwa amekamilika.ana kila kitu. Leseni ya FAA, leseni ya urubani, Sare na Ufaham kuhusiana na kazi hiyo. Yaani kifupi alikuwa yupo Gado Ile mbaya. Ukimcheck hivi we mwenyewe unaingia King kuwa jamaa ni Rubani..mkipiga stories za mambo ya huko hewani ..unaweza jikuta una come jinsi alivyokuwa fresh.

Safari tayari ya kuanza kula bata na kutapeli Mabank duniani


Basi mshkaji akakaza mwendo akiwa ametinga sare zake za kirubani na vitambulisho vyake vyote akiwa anatumia jina la Frank Williams akaenda mpaka Bank kwenda kufungua Account akiwa ametinga sare au uniform za marubani akitembea kimikogo kabisa kwa kujiamini. katika mabenk yote aliyopita walikuwa wakimheshimu sana maana miaka hiyo ya 1960s marubani walikuwa wanatesa sana kitaa...kama una demu wako hajielewi elewi trust me rubani angeweza kukupora kirahisi sana akamgonga akakuachia maumivu. yaani walikuwa wanaonekana mambo safi sana na wanaheshimika ile kinoma.tena Zaidi yeye kutoka Kampuni kubwa ya kimataifa. hawakujua. hawakujua maskini, kuwa huyu alikuwa bwana mdogo tu tapeli msanii wa kiwango cha standard gauge.
frank-abagnale-pilot.jpg

Frank akawa amekuwa mcharo ile mbaya. Mademu wengi walikuwa wakimzimia..hasa wale mademu wafanyakazi wa kwenye ndege na si unajua walivyo wakali… basi wengi wakawa wanamjia tu kwa nyuma "frank tunakuzimia" n.k. jamaa hakuwanyima haki yao.akawa anawapa tu.anawapa, anawagaia,anawakita na mashine,anawapa mkono,akawa anawacharaza bakora,anawapiga kwa ukuni...si unajua ukishakuwa mwana utamaduni humchapi mwanamke kwa fimbo...unamchapa kwa ukuni.watu wa kale toka zamani.... Ikawa yeye ni mtu wa kuwa na list. Anatick tu huyu tayari, huyu tayari..huyu bado next week. Kumbe aogope nini na uzushi upo pembeni?

Kwa kujiamini kabisa akaamua kusafiri kama deadheading kuelekea Miami..si umewahi zisikia beach za Miami ?(tamka mayami) alipanda pipa ndege ya Eastern Airline 127 akiwa na sare zake na kujaza form akiweka details zote. Akiwa huko ndani akaenda mpaka kukaa sehemu inaitwa cockpit huko alikaa kwenye seat na kuwa tayari kwa swali lolote ambalo angeulizwa na marubani. unajua kosa moja tu lingemfanya wamshtukie na wampeleke segerea kunyea debe? Jamaa alikuwa anajiamini ile mbaya akakaa mle ndani ame chill tu kama mtalaam ile kinoma.

Kinyume na matarajio yake marubani wala hawakujishughulisha naye kule mbele kwenye chumba chao mwishowe wakatua Miami na hapo akashusha pumzi za kushukuru..afadhali.kutoka hapo Frank akagundua sasa atakuwa kila mara anasafiri kama deadheading kwa miaka kadhaa ijayo.ilikuwa bure na alikuwa anaweza kwenda sehemu yoyote ya dunia ambako angeenda ku cash zile check zake fake. Jamaa akawa anakula bata tu na watoto wakali toka mataifa mbalimbali. Wakati anahojiwa anasema hivi vitu vitatu vilimsaidia sana katika shughuli zake za utapeli hapa duniani.1. mwonekano wake 2. Umakini wake katika kutambua mambo 3. Kufanya utafiti wa kina kabla ya kufanya jambo lolote.
pan-am-pay-check2.jpg

Anasema alijifunza jinsi ya kuweza kutapeli kwa kupitia cash baada ya kufanya utafiti kwa kuangalia details flan flan kwenye check. Na kuhakikisha kuwa anazichezea hizo namba katika namna ambayo itachukua muda sana kugundua kuwa zile namba zimechezewa check ni fake. Hivyo alikuwa akiziandika zionekane ni za mbali sana ili zichukue muda mrefu kufuatiliwa na hvyo kumfanya aweze kujitolea pesa tena na tena katika bank hiyo hiyo.

Zaidi Zaidi frank alikuwa anafanikiwa sababu alikuwa pia anafungua akaunt ya ukweli kwa jina la kufikirika.na mara kadhaa alikuwa akitumia check deposit ya ukweli na kuwapa bank address ambayo alikuwa kiishi au sanduku la barua ambalo angepokea check husika. Hizo information zilikuwa zinafanya transaction iwe ya kuaminika kabisa.akawa anajiandikia check kwa jina lingine na kwend ku draw pesa katika banks mbalimbali hapa duniani. Inawezekana hata bongo alifika…(ila sidhani miaka hiyo tulikuwa bado sana). Na pale bank husika ilipokuja kugundua kuwa check ilikuwa ni fake yeye alikuwa tayari ameshaondoka yupo pande nyingine ya dunia...
l7obPab.jpg
..................................................................................................................................
SEHEMU YA PILI

Frank aliendelea kuishi maisha haya ya kuhama hama na kuwakwepa mapolisi kila sehemu huku akiendelea kula bata na watoto wakali. Kiufupi maisha yalikuwa yamemnyookea hasa, ingawa alikuwa anaishi kwa mashaka kiasi flani lakini alikuwa smart sana. Maelfu ya dollar alizokuwa anatapeli kwenye mabenk alikuwa anazificha kwenye masanduku salama ya kuhifadhia pesa (safe deposit boxes) kila sehemu ya nchi ili hizo pesa zitumike ikiwa atapata msala. Alishajua kuwa amechagua kuishi maisha ya namna hiyo hivyo anapaswa kuwa tayar tayari wakati wowote akipata msala. Mtu mwingine ungefikiria kuwa jamaa jinsi alivyokuwa na pesa ana anavyokula bata na mademu kila sehemu alikuwa ana enjoy sana. Hapana. Alifikia hatua akachoka maisha ya kuwakwepa mapolisi na akawa wakati mwingine anakuwa mpweke sana.kwenye mahojiano anasema kila mtu aliyekutana naye hakuweza kudumu naye maana alikuwa anajitambulisha kwa fake name. si jina lake halisi.hivyo akawa hadumu na marafiki. Mademu anagonga tu halafu anaanza mbele hataki kudumu na demu muda mrefu maana ilikuwa ni risk sana.”hivyo ye anapita tu” ....

Frank alishajua kuwa yale maisha hayakuwa ya kudumu hivyo alikuwa anaishi kwa umakini sana lakini alijua kuna siku tu angekamatwa. Kweli siku hiyo ilifika. Alikuwa akisafiri kuelekea Miami akiwa kwenye ndege kama kawaida deadheading..yaani anasafiri bure. Ndege aliyopanda ikatuka Dade County na akiwa ndani ya ndege maofisa wa polisi watatu wakamfuata na kuanza kumhoji. Yeye alikuwa amejenga utulivu mzuri tu akidai kwa kujiamini kabisa kuwa yeye ni Frank William na kuwa ni Pilot bado wale maofisa walimchukua kwa ajili ya mahojiano Zaidi.

Akiwa anahojiwa frank akatoa kitambulisho chake fake na kwa kuwahakikishia kabisa akawapa majina ya marubani,wafanyakazi,masela kibao wa kazini wengine wa PanAm aliokuwa anafanya nao kazi. polisi walipowapigia jamaa hao waliwahakikishia kuwa jamaa ni mwana/mfanyakazi mwenzao wapo naye kitambo tu wanapiga naye mzigo PanAm bila shida yoyote tena mtu peace sana hana noma wala kokoro. Na Frank alikuwa mjanja sana aliweza kujichanganya na wenzie kila alipokuwa akisafiri na wakamwamini kuwa ni Rubani kweli kweli. Polisi walipopata huo uthibitisho kwa masikitiko, wakamwomba msamaha kwa kumsumbua na kumchelewesha. Akawaambia wasijali anajua wapo kazini na dunia imeharibika hivyo wanatimiza wajibu wao. hamna noma peace and love.na polisi walihisi pengine angeweza washtaki kwa kumharass..jamaa aliwahakikishia yale yamepita na yaliyopita si ndwele wagange yajayo...wakapeana tano na mapolisi akaondoka zake.kuanzia hapo akaamua kutulia kwanza kidogo kwa muda flan kwa kiingereza tunaita ku lay low for a while. Atulie kwanza kucheck hali ya hewa.

FRANK AWA DAKTARI WA WATOTO

Akiwa Atlanta Frank alifanikiwa kupata eneo flan limetulia sana ambalo vijana wengi walikuwa wamechukua apartments akaamua naye apange eneo hilo kwa mwaka mmoja. Na huko alijiandikisha kama ni doctor akiwa anajaza mkataba wake wa kupanga hizo apartment. Na kudai ni daktari ambaye alikuwa amekuja kupata mapumziko ya mudA mrefu kutokana na kupiga kazi kwa muda kwa miaka mingi akiwa daktari wa watoto yaani pediatrician. mshkaji alikuwa msanii kinyama.

Basi jamaa akawa amejenga utulivu maeneo hayo.anakula tu pesa zake za kuwaibia mabenk.wewe unahangaika kuwatapeli waswahili wenzio maskini laki laki zao.mwenzio anayaibia mabenki hata dhambi hapati sana.uongo? Siku moja ametulia home anacheck zake movies akasikia hodi. Kwenda kufungua akakutana na jamaa mmoja ambaye alijitambulisha kuwa ni doctor. Frank akaona huu sasa msala kakutana na doctor mubashara kabisa kaja kumtmbelea.maana alijua ishu yake ingebumbuluka.wakiwa katika maongezi alijitahidi sana kutengeneza utulivu na mwishowe akaja kugundua yule doctor hakuwa interested sana kuzungumzia masuala ya kazi.alikuwa alikuwa mtu wa watoto sana… hivyo huko kwenye mademu sasa ndo akamkuta frank kwenye profession yake kabisa aliyozaliwa nayo...sehemu husika .. wakawa wanapiga sana stories kuhusu mademu na kuanza kuwagonga ..wakagundua wote ni wazee wa mabinti na hivyo wakawa marafiki sana.

Yule doctor akamwomba Frank siku moja amtembelee katika hospital anayofanya kazi.pasipo kigugumizi frank alikubali. Na ikawa anamtembelea kila mara na mwishowe frank akawa anafahamiana na wafanyakzi wengi tu pale hospitalini. Si unajua mtoto wa mjini anavyojichanganya haraka na watu.hii ilimsaidia sana maana aliweza sasa kujifunza juujuu kuhusiana na udaktari wa watoto.mwishowe hata aliruhusiwa kuwa anaingia library huko alijitahidi sana kujifunza udaktari wa watoto kama ambavyo alikuwa akijinasibu.

Jamaa alionekana kufit sana kwenye hii nafasi alionekana anaipenda sana kazi na mwishowe siku moja meneja wa ile hospital akataman aonane na frank waongee kuhusu ajira pale kazini. Yaani alimpenda frank akapenda naye afanye kazi katika ile hospital. Dah…. Frank akaona huu sasa msala,ishakuwa noma.maana hakuwa daktari wa ukweli Zaidi ya usanii tu.akawa anajaribu sana kukwepa hiyo hali lakini jamaa alikuwa akimsumbua kila wakati kuwa waonane waongee. Mwishowe akakubali. Na yule meneja akamwambia kitu ambacho zaidi kikamshangaza frank.alimwomba kuwa awe anasupervise wanafunzi wa udaktari wanaokuja mafunzoni shift za usiku kuchukua nafasi za daktari ambaye alikuwepo aliyepata dharura.frank alikataa… lakini meneja alimshawishi sana.kabla ya hapo frank alikuwa amepewa nafasi ya kuwasimamia wagonjwa mbalimbali pale hospitalini baada ya kuwa amepata kibali cha kufanya kazi Jimbo la Georgia.

Frank alikuwa na ujanja flan kukwepa maswali ambayo alikuwa hayafaham pindi aulizwapo. Ikiwa ingetokea angeulizwa kitu ambacho hakijui basi angekifanyia mzaha au utani na mwishowe kingepotezewa.yaani ilikuwa huwezi mbananisha kwenye maelezo ambayo hayajui...atakuuzia uzia chai mtacheka ishu itapita. Basi baada ya kuachia ile kazi ya usimamizi wa wagonjwa kwa mhusika mwingine siku zote ule uwezo wake wa kufanya masikhara na utani vilimsaidia sana kuficha ukweli kuwa hakuwa amesomea udaktari. Zaidi zaidi wafanyakazi wengi walikuwa wakimpenda maana alikuwa mtu wa chai sana na ucheshi kuwafanya wacheke muda mwingi kumbe mshkaji ndo anafukia fukia mashimo kwa style hiyo.hakuwa na beef na mtu wala ujivuni.alikuwa mtu wa watu sana.Basi aliendelea ku maintain ile nafasi yake kama daktari msimamizi sababu hakuwa akilazimika kufanya kazi yenyewe Zaidi ya kusimamia inavyofanywa na madaktari wengine.

Siku za mwizi ni arobaini. Siku moja mtoto aliletwa chumba cha wagonjwa wa dharura akiwa amejeruhiwa mguu.frank akaitwa kwenda kusaidia. Naye aligundua hapo ndipo rangi yake itajulikana kama ni nyekundu au njano.akaona isiwe shida haraka naye akawaita wale vijana waliokuwa mafunzoni akawakabidhi ile kazi halafu yeye akasimama serious kuwaangalia wakipiga kazi.huku akikagua kagua.nao kwa kutaka kupata sifa kwa msimamizi wao ambaye ni frank wakapiga ile kazi vizuri sana. Lakini jambo hili lilianza kumpa shida kiasi kikubwa sana. Sasa alianza kuwaza kuwa anacheza na maisha ya watu hivyo akaona si suala la kulifanyia mchezo. Frank akaamua kuondoka hapo hospitalini maana alishagundua kuwa angeweza kuhatarisha maisha ya mtoto.aliamua kujiuzulu baada ya muda mfupi wa lile tukio alikuwa ameshafanya kazi kwa miezi kadhaa haukufika mwaka. Akaamua kuelekea jimbo la Lousiana.

MAISHA YA FRANK LOUSIANA AKIWA NI MWANASHERIA

Frank akiwa Lousiana siku moja alikutana na moja ya mademu aliowahi kuwagegeda miaka ya nyuma. Huyu dada alikuwa mfanyakazi wa kwenye ndege. Frank alimwambia yule dada kipindi kile kuwa alikuwa ni co-pilot yaani rubani msaidizi. sasa akwambia si hivyo tu ila pia alikuwa ni mwanasheria. Alisomea urubani na pia alikuwa Mwanasheria.frank akawa anaendelea kumgegeda yule mrembo kwa mara nyingine tena. anajilia tu kiulani. ukitaka kupata mademu wakali unatakiwa uwe mjanja mjanja.

Siku moja wapo kwenye party usiku wakila bata yule dada akamkutanisha na mwanasheria aliyekuwa akifanya kazi kwa mwanasheria mkuu pale jimboni. Yule jamaa akavutiwa na Frank sababu Frank alidai kuwa yeye alipata Degree yake ya Sheria toka Chuocha Harvard. Jamaa akaona hiki kichwa sana maana Harvard wanaosoma kule si watu wa mchezo mchezo.ni Vipanga hasa si Chuo cha vilaza hata kidogo. Jamaa akamwambia kuna nafasi katika ofisi ya Mwanasheria mkuu. Akamwambia ambacho alipaswa kufanya ni kupeleka tu transcript yake kwa ofisi ya mtihani na kuomba nafasi ya kufanya mtihani ili akifaulu aajiriwe kwa hiyo nafasi.

Hii ilikuwa changamoto ambayo ilimpa hamu pia ya kujaribu, akiamini nayo atashinda tu.baada ya kufanya maongezi na mwanasheria frank aliamua kwenda kutengeneza transcript bandia/fake kutoka chuo kikuu cha Harvard. Alifanya kwanza utafiti ni kozi gani zinafundishwa chuo cha Harvard.alikusanya kila ambacho kilihitajika kwa ajili ya kutengeneza mfano wa transcript hiyo. Aisee… mpaka amemaliza ile transcript ilikuwa kama original.yaani mle mle….ingawa hakuwa amewahi kuiona transcript halisi toka chuo cha sharia.ilionekana kuwa ni yenyewe kabisa na akaamua kwenda kujaribu.

Hatua iliyofuatia ilikuwa ni kufanya mtihani .hivyo frank akanza kujifunza sheria kwa week kadhaa kabla hajaenda kufanya mtihani.alipoona na mambo mengi tayari anayafahamu aliedna kujiandikisha kwa ajili ya kufanya mtihani.akawapa transcript yake ya magumashi. akaruhusiwa kufanya.Alichemsha…si unajua hakuwahi kusoma sheria katika maisha yake yote. Lakini alikuwa na advantage..ule mtihani uki fail unaweza tena kuja kufanya tena na tena.unaruhusiwa kurudia.hivyo akarudia tena na this time jamaa alipasua kinoma na akapewa leseni ya kufanya kazi kama mwanasheria.

Na hapo hapo akaomba kazi kwa mwanasheria mkuu wa hilo jimbo ikafanyika interview.akafanikiwa kuajiriwa kama legal assistant akiwa anafanya kazi kama upande wa corporate law.akawa mbali na marupurupu mengine analipwa mshahara wa usd 13,000 kwa mwaka miaka hiyo. Ulikuwa mshahara mkubwa sana. Jamaa alionesha kipaji cha ajabu sana cha utapeli na usanii katika historia hapa duniani.katika ile ofisi kulikuwa na mfanyakazi mwingine mpya aliajiriwa ambaye yeye alisoma Harvard kiukwel kweli. Jamaa akawa ana mghasi sana kwa kutaka kila mara wapige stories za chuo na kutaka kuzungumzia jamaa wengine ambao walisoma pale chuo wakamaliza mwaka huo.akaona hii sasa itakuwa issue jamaa asije akamuumbua bure. Akaamua kuachana na kazi yake hii ya uana sheria na kuamua kutafuta kazi nyingine.

Akaamua kurudia ile kazi yake ya kwanza.lakini safari hii akaamua kuwa anafanya kazi shirika la ndege la Trans World Airways(TWA) hivyo akajipatia sare,akatengeneza leseni mpya ya FAA,na kadi na kila kitu kilichotakiwa kama alivyofanya kule PanAm. Akaanza kupiga kazi tena akisafiri sehemu mbali mbali duniani na ku Cash bank mbalimbali ambazo kipindi kile hakuzigusa.

FRANK AKIWA UTAH (Profesa wa Sociology)

Jamaa katika pita pita yake akafika mpaka Jimbo la Utah hili jimbo lilimvutia kwa uzuri wake na pia kuw ana warembo wengi sana. Jamaa akenda mpaka maeneo ya kampasi za chuo...daah aliona watoto wakali sana.asikwambie mtu.udenda ulimtoka akajua hapo sasa inabidi kupiga kambi ili aweze kuwagegeda ipasavyo watoto warembo. Nia alikuwa nayo ,uwezo (pesa) alikuwa nao na sababu pia alikuwa nayo.

Jamaa akaomba kazi chuoni ili afundishe. Alipata akawa anawapiga pindi watoto warembo hapo chuoni.huku jioni anawapangia ratiba ya kuwagegeda.apewe nini na shetani?acha awachape watoto warembo.

Jamaa akaamua sasa ahame kile chuo akaombe chuo kingine kufundisha chuo cha Brigham Young University. Akafanya appointment akijifanya yeye ni Profesa wa Sociology. Akawa amewasiliana na Dean na kumwambia alifanya kazi ya kufundisha kwa miaka kadhaa kabla hajaacha na kuwa Rubani. Na akasisitiza sasa anataka kurudi katika kazi aliyokuwa akiipenda sana. Kazi ya ualimu. Yule dean alivutiwa sana na uzoefu mbalimbali aliokuwa nao frank na pia uchangamfu wake.

Akiwa na vyeti mbalimbali feki Frank akafanikiwa kupata interview na Dean akaamua kumwajiri akiwa amevutiwa naye sana. Akakubali kumpa ajira akiwa amepewa kozi moja aifundishe kwa semester nzima. Jamaa akaamua kwenda library kujiandaa kwa ajili ya kufundisha kozi hiyo. Hatimaye kwel akapewa mkataba wa kuajiriwa kwa semester moja awapige kipindi watoto wa kidosi akiwa kama Profesa Frank.alionekana kufurahia kazi hii mpya ingawa ilikuwa ni kwa muda tu maana hakuwa amepata mkataba mkubwa. Anapiga vipindi lakini pia anapata muda jioni wa kuwagegeda watoto wazuri ambao wanasoma pale chuoni na salary anapata kama kawa. Jamaa alikuwa anaua ndege wawili kwa jiwe moja.kazi na dawa. Kazi hii hakudumu nayo sana kwa kuwa dean alimtaka kuwa asubiri nafasi itokee ya kudumu kwa kuwa chuoni hawakutaka tena kuajiri walimu wa muda mfupi.

SAFARI YA KWENDA CALIFONIA.
Frank akaondoka zake Utah huku akiwa amejilia kiasi cha kutosha nanii za watoto wakali wabichi wa UTAH…akaamua kuelekea Califonia. (Unaukumbuka wimbo wa Tupac califonia Dream? Hili jimbo nalo lina maraha yake huko Marekani. Binafsi niliwahi fika huko kumekucha hasa) akiwa anaelekea huko akafikiria kurudia tena kazi yake ambaya huifanya vizuri zaid. Kuandika check za magumashi.kipindi hiki akawa amepata uzoefu mkubwa zaidi katika kipengele hiki. Aliweza kuandika check kubwa kubwa za maelfu Zaidi ya mara ya kwanza.aliweza kujikusanyia Zaidi ya USD 100,000 kwa kipindi hicho. Ukiziconvert kwa sasa zinakuwa nyingi Zaidi.

Alikuwa kijana mdpgo mwenye mkwanja wa kutosha kwa umri wake….alikuwa na ukwasi mwingi tu huyu bwana mdogo.bado alikuwa na upweke kiasi flani.maana kumbuka alikuwa ana vitambulisho mbalimbali.mara doctor,mara mwanasheria,mara profesa,mara…. Yaani ili mradi jamaa aliweza kuwa kila kitu.angeamua hata kufake kuwa yeye ni baba yako ungemwamini nakwambia.angekuja angekueleza yeye ndo baba yako kweli kweli huyo uliye naye siye..na angeweza hata kumshawishi mama yako…usiombee ukutane na frank mtaalam.jamaa alikuwa kichwa hasa.

Basi katika pita pita zake akafanikiwa kumpata mtoto mmoja mkali sana.wakapendana. huyo binti alikuwa ni mfanyakazi wa kwenye ndege. Na nikuambie kitu? Ukitaka watoto wakali sana… angalia wafanyakazi wa kwenye ndege,aisee ni wazuri sana..kama umepanda panda ndege wengi wao ni wazuri sana.sema yale maumbo yetu ya miss bantu huyapati.

SEHEMU YA MWISHO.


Basi frank akawa amempenda sana yule mtoto na alitamani kabisa kuwa waishi wote na katika kuzidiwa na mapenzi ye mwenyewe akaamua tu kumwambia ukweli yule binti.akajichana ye mwenyewe. Unajua hakuna kitu kigumu kama kukaa na siri…trust me ni ngumu sana yaani sometime unatamani hata uende porini ukaseme siri yako then baada ya hapo unajisikia kama umetua mzigo mkubwa.kama tu ile story ya mfalme aliyekuwa na masikio ya punda. Yeye aliamini kwa kumwambia huo ukweli basi yule mwanamke atamsamehe na kuyachukulia yale kama ni madhaifu yake na wakasonga mbele pamoja wakiishi real sasa.maana jamaa alikuwa hata hujui leo ye ni frank au john au abel....

Mshkaji alifanya kosa. Usiwaamini sana mademu… jamaa alitegemea kuwa demu angemwona amekuwa mwaminifu na sasa wasonge mbele kumbe sivyo.dem akaenda kumchoma FBI na kuwalezea alipo. bahati nzuri Jamaa wa machale alifanikiwa kuwatoroka akawa tena anaishi maisha ya kimachale machale. Jamaa akasafir mpaka ufaransa. Na akiwa katika ndege akakutana na demu mmoja mkali mfanya kazi wa kwenye ndege wakaanza mahusiano. Aligundua kuwa baba wa yule demu anamiliki duka la kuprint pictures na stationary. So akawa anatamani sana akutane na baba wa yule binti.kweli ikatokea akakutana na baba ya bint yule.frank akamwambia mzee kama atakuwa tayari kupiga naye kazi.yaani waprint kazi moja yenye mshiko kwa ajili ya PanAm.frank akamwambia mzee anampa tenda ya kuprint check 10,000 za payroll kwa wafanya kazi wa PanAm.yule mzee hakuwa na hiyana akaona mchongo si ndo huu. Akapiga kazi

Frank akazichukua hizo checks na kuanza kuzitumia katika Mabank kadhaa hapo hapo ufaransa.akajikusanyia makwaru kwaru (pesa) kibao. Halafu haraka sana akapanda mwewe kurudi USA ambako pia aliendelea kujikumbia mkwanja kwa njia zake haramu za kimazabe mazabe.

Muda si mrefu baada ya kurudi US. Siku moja Manjagu wakambananisha airport ya Boston akiwa anataka kupanda mwewe akale bata jimbo lingine. Jamaa wakamweka kwanza korokoroni ili waendelee kukusanya ushahidi mbalimbali kuthibitisha kama alikuwa ni yeye yule jamaa mtukutu sana Frank A.jr hata hivyo Manjagu /polisi walishindwa kupata kwa usahihi ushahidi wa kutosha yeye ni nani hasa. Walikuwa wamweka tu korokoroni hajapelekwa hasa segerea kwenyewe.ushahidi wa kutosha ukawa umekosekana na mwishowe akaachiwa kwa dhamana akiwa ameponea chupuchupu kuja kukamatwa na FBI ambaye alikuwa ametumwa kwenda kumtafuta. Jamaa ikawa kama wamempiga chura teke… si unajua humkomoi ukimpiga chura teke unamwongezea mwendo. Basi akazidi kuwa jasiri badala ya kukatishwa tamaa au kuingiwa woga.

Baada yu ya kutoka akaenda kuazima sare za walinzi au sercurity guard na kwenda kusimama pale pale uwanja wa ndege ambako mamwela walimkamata masaa kadhaa yaliyopita. Alikuwa ameshikiria mfuko mkubwa maalum ambao alikuwa anasubiria watu waweke deposits/pesa zao kila wanapokuwa wanapita au kusafiri kama ulivyo utaratibu. Wakawa hawana shaka wanaenda wanaandikisha zinahesabiwa wanakuja wanaweka kwenye ule mfuko/begi maalum alioshika frank wanaendelea na shughuli zao. Lile begi lilipoanza kujaa aliamua kulibeba kupeleka kwenye gari alilokuwa amekodi. Lilikuwa zito maana kulikuwa kumewekwa mapene kichele (pesa nyingi sana). Basi wale jamaa wengine wakaamua kumsaidia mshkaji pasipo kujua wanamsaidia mwizi katika mchakato wa kuondoka na pesa za wizi.jamaa siku ile ile moja tu alipiga zaidi ya usd 60,000 akaweka begani akalala nazo mbele.ilikuwa noma ile mbaya…. Polisi walikuja kumgwaya hapo baadaye si kwa usanii ule.

Kukamatwa

Frank akawa anaonekana ameshindikana karibia kwenye kila kitu alichokuwa akifanya.alifanikiwa kuwakwepa manjagu na hata FBI kwa kila mpango mpya.aliendelea kufikiria namna ambavyo ataendelea kupiga mkwanja mrefu. Akaja na wazo lingine.aliamua kuwa kwa sasa hatakuwa anasafiri peke yake. Atakuwa anasafiri na warembo kibao. hii itasaidia aweze kuwa ana cash mkwanja zaidi .maana unapokuwa umezungukwa na mademu watu hawakutilii shaka hata kidogo hivyo akaona aibuke na mbinu hi ya kutembea na watoto kadhaa wakali.

Akiwa anatembelea Arizona Frank akaweza kufanya mchakato wa kuoana na Director/Mkurugenzi aliyekuwa anahusika na masuala ya wanafunzi vijana katika vyuo vya serikali jimboni hapo.yaani kuwapeleka vyuo mbalimbali wanapoomba na pia kushughulika nao wanapomaliza kwa masuala ya ushauri na kazi. Akawa amaeongea naye uwezekanao wa kuajiri wanawake wengi kama maafisa uhusiano kwa ajili ya PanAm. Na akamwambia wanawake ambao atakuwa amewachagua watapata hata nafasi ya kwenda kutembelea Ulaya kipindi cha majira ya joto. zaidi zaidi hao wanawake watapewa mpaka uniforms au sare za PanAm,watapewa mshahara na barua za ajira pindi wamalizapo tu masomo yao.

Ilikuwa patashika pale chuoni watoto wazuri wengi waliomba hiyo nafasi… kila mtu alitamani awe mfanyakazi wa kwenye ndege..na si unajua watoto wakali wanapenda maisha yale ya kuzunguka tu na mwewe angani huku wakial bata sehemu mbalimbali duniani.katika kusagula sagula humo ndani akajipatia watoto nane wakaliiiiiii balaa.hawa walikuwa wakisisimkwa na vinyweleo kusimama wakiwaza jinsi ambavyo wataizunguka dunia ndani ya mwewe.halafu wakawa wanawaza pia jinsi ambavyo watakuwa wanalipwa kula bata. Just imagine unaenda kula bata na bado unalipwa pia.hawakujua.hawakujua.

Lengo la Frank lilikuwa kuwatumia hao mademu wakali kwenda ku cash zile check zake za kimagumashi hivyo akawa anaandika check za malipo makubwa kuliko hata ya kawaida. Akiwa huko huko bado alikuwa anawala kwa zamu tartiiiiibu.kama Analia vile.kwa hiyo muda wote akawa anazunguka nao wakiwa wamevaa zile sare wakifurahia sana na akawa anaenda nao bank ku cash zile pesa na huko hawakuweza kumtilia mashaka hata chembe maana unawezaje kumtilia mashaka mshkaji amezungukwa na watoto wakali wa kibongo,kilatino,kitasha n.k tena wamevaa sare za PanAm. Huwezi.kumbe jamaa anawapa tu za chembe kimya kimya anafinya mpunga wa kutosha kutokana na wao.inasadikiwa jamaa alikusanya mpunga wa zaidi ya usd 300,000 miaka hiyo. Si mchezo.

FRANK ANAHAMISHIA MASHAMBULIZI UFARANSA (MWANDISHI WA MOVIES ZA HOLLYWOOD)

Alipoona hii imefanikiwa akaamua tena apumzishe hii mbinu ili asije akashtukiwa. Akaamua kwenda Montpellier huko Ufaransa. Haikuwa mbali na alipokuwa amezaliwa mama yake. Akamua kutulia kwanza kwa muda kwenye nyumba tu ya wastani akiwa amebadilisha jina anaitwa Robert Monjo na akijifanya yeye ni mwandishi wa movies toka Hollywood.karibia mwaka hivi alijitahidi kuishi maisha ya kawaida tu.alikuwa amechoka sana na maisha ya kukimbia kimbia manjagu na FBI.

Siku za mwizi zilikuwa zinakaribia …na jamaa alishaacha hata kuzihesabu maana si unajua wanasema siku za mwizi ni arobaini?so kama unaiba hakikisha ukifika 39 unaacha. Jamaa mmoja mgwadu sana wa FBI alikuwa anaitwa Joseph Shea huyu alikuwa amekomaa ile mbaya kumtafuta Frank kwa miaka na miaka.maana FBI si kwamba walikuwa hawana taarifa zake.walikuwa nazo ila walikuwa bado hawampata ile bumper to bumper wanamlia tu timing. zaidi zaid ya kusikia tu mshkaji kapiga huku.wakienda hayupo,wanasikia tena kapiga bank flan wakienda hayupo. Jamaa alisema ye atakomaa naye tu mpaka kieleweke iwe mchana au usiku,iwe masika au kiangazi. Hakuna kulala.

Miezi kama minne hivi Frank akiwa France jamaa wa FBI alishapata taarifa hizo. Unajua ilichukua miaka mingi sana kufahamu kuwa Frank hakuwa mtu mzima ni bwana mdogo tu ambaye akili zimemzidia ameamua kuzitumia kihuni. Yule FBI alikutana na mmoja wa wafanyakazi wa ndege ambao frank alikuwa amewakamua. Akamwonesha picha kuwa anamtafuta jamaa.. yule demu akakiri anamfaham jamaa na kuwa yupo ufaransa sehemu flan ame chill tu.

Manjagu wa Ufaransa wakatonywa kuwa kuna mshkaji mmoja hafai ameshaziumiza banks mbalimbali Zaidi ya Usd 2.5 Million so yupo kitaani kwao wakamcheck. Wale wafaransa wakaona hii sasa issue yule mpigaji yupo nchini mwao.wakaanza mfuatilia na kuja kumkuta frank anafanya shopping mtaani kwenye kigrocery flani karibu na maskani mwake. Wakamdaka kumpeleka Montpellier Polce Station kumfungulia mashtaka kwa makosa aliyokuwa amewatendea pale ufaransa. Baada ya mahojiano frank alikuwabli kuwa yeye ni Frank A. Jr lakini akakataa kueleze kiundani makosa yake yote.hakutaka kuwapa habari yoyote kuhusiana na makosa yake. Ana bahati sana angekuwa ni mbongo halafu kakamatwa bongo akingepata kisago cha mbwa mwizi mpaka angeanza kuimba.

Ndani ya week frank akawa amepelekwa kwa pirato huko ufaransa na kukutwa na misala kibao..yaani alikutwa na madhambi au makosa mengi tu kwa mujibu wa sheria yakiwemo hayo ya utapeli. Wakampeleka kunyea debe segerea ya ufaransa kwa mwaka mmoja gereza moja la watu watukutu sana la Perpignan…. Aliishia tu kufungwa miezi sita. Ila hali ya mle ndani ilikuwa mbaya sana.wakamtoa.

Akapelekwa Sweden na baadaye Ufaransa. Huko akifanikiwa mara kadhaa kuwatoroka Manjagu na FBI na kuanza kuishi maisha ya kimachale machale… mwishowe akajikuta anasakwa ile mbaya.FBI wakamweka katika ile list yao ya wanted. Akajikuta hana pa kujificha na mwishowe alikuja kukamatwa akiwa amejificha huko New York si unajua mkono wa sheria ni mrefu sana. Na wale manjagu walishaona huyu jamaa si saizi yao wakampeleka kumkabidhi kwa wazee wa kazi wa FBI ( Female Body Intruder… ha haha am kidding bwana si maana hiyo) huko wakampeleka kwa pilato ili akapate stahiki zake kwa madhambi aliyowatendea wanagenzi mbalimbali.

Jamaa wakamhukumu kifungo cha miaka 12. Huko Virginia Gereza la Petersburg. Na hata hivyo akapata parole akiwa na miaka 26 akiwa ametumikia miaka 5 nyuma ya nyondo. Yaani alikuwa mpaka muda huo amechezea mvua 5 tu katika 12. Akaachiwa na kupata nafasi ya kuanza maisha mapya.

Baada ya kutoka segerea jamaa akaanza kuranda randa mtaani akitafuta vibarua. Ila life lilishakuwa gumu kinoma jamaa hakuzoea ku hustle namna ile na makashkash kibao akikimbizana na life.akawa anakamata kamata tu vijikazi kiasi vya kumtoa angalau asilale na njaa.alikuwa mara nyingi akijitahidi isijulikane kuwa alikuwa ni tapeli na alishawahi fungwa.lakini mwishowe waajiri wake wakawa wanakuja kufaham ukweli na kumfukuza.

Baada ya muda Frank akaanza kuwa frustrated … yaani kama kupagawa flani hivi kimawazo sababu alijua kabisa ana kipaji ambacho sehemu flan mtu anaweza akakihitaji. Hivyo akawa anawaza kutafuta mteja ambaye angekuwa interested na ujuzi wake na hivyo kufaidika nao. Hivyo akaamua kutafuta namna ya kujitangaza. Kwa kushangaza kabisa watu ambao wangefaidika naye walikuwa ni FBI. Hawa FBI ndiyo ambao wangeweza faidika na kipaji alichokuwa nacho. FBi walikuwa wanahitaji kufaham namna mbavyo wahaalifu wanatumia akili kufanya uhalifu wao ili waweze kuwakamata wahalifu hao. Frank akaanza kuwapa lecture bure.alijua pia kwa kutoa elimu hii alikuwa analipa kwa jamii aliyokuwa ameiumiza kwa utapeli wake.kabla ya muda mrefu kupita ikaja kazi ambayo ingeweza kumlipa elimu aliyokuwa nayo ikawa inahitajika sana na makampuni mengi duniani. Makampuni mengi yakagundua yanaweza kuokoa pesa nyingi mamilioni au mabillion kutoka kwa matapeli ikiwa watakuwa na mtaalam wa utapeli ambaye atawasaidia. Hivyo frank akawa ni mtu ambaye anatumika kwa ajili ya kuwapa taarifa muhimu za kuzuia matapeli.

Jamaa akawa anaitwa huku na kule akawaelekeze na wanampa mkwanja wa maana hasa. Na mpaka leo hii frank anaheshimika na makampuni mengi akiwa amefungua kampuni yake ya kutoa ushauri na kulingana na website yake ya www.abagnale.com frank amekuwa akienda kupiga lecture,akifanya consultation duniani nzima na kutoa semina na makongamano na vile vile akaamua FBI awe anawapa ushauri bure kabisa ingawa wao walikuwa wanataka wamwajiri.yeye aliona aitumikie FBI kwa nia hiyo ya kuwapa ushauri bure.

Jamaa ameandika vitabu vingi tu,Makala na mahapisho mbalimbali na ku design check ambazo ni salama zinazotumika na wafanyabiashara mbalimbali wakubwa duniani. Kiuhalisia hakuna shaka kabisa kuwa jamaa amekuwa akijitahidi sana kusahihisha makosa aliyoyafanya miaka ile ya nyuma na kipaji au akili yake kaipelekea katika mambo ya kujenga zaidi na si kuwapiga wenye makampuni na bank kama zamani na kula papuchi tu muda wote. Na jamaa ukimcheki amechange sana kwa sasa akiwa na mke ambaye wameishi naye Zaidi ya miaka 25 na kufanikiwa kupata watoto wa3. Jamaa amekuwa mtu wa dini sana kwa sasa. Anaenda church na kushirikiana na wadau wengine katika kujenga taifa. Ukimcheck kwa kweli ame change sana. Kwa sasa anaishi huko Midwest na mkewe na watoto wake vidume watatu.anakula kihalali. tuacheni uhalisi ndugu zanguni.....

frank-abagnale-jr-and-family-opening-night-of-the-broadway-production-DB38TR.jpg
 

Monday, October 23

 



Wako watu ambao uwepo wao katika ulimwengu wamechangia kwa namna moja au nyingine kuufanya huu ulimwengu uwe jinsi ulivyo. Wako wengine ambao wamechangia kwa kiwango kikubwa kuifanya 'mifumo' ya dunia iwe jinsi ilivyo. Mara nyingi watu hawa tunawasoma kwenye vitabu endapo kama waliishi miaka mingi iliyopita na endapo kama bado wako hai huwa ni watu tunao wahusudu na kuwachukulia kama mifano ya kuigwa.

Lakini wako watu ambao ni vigumu kuwahusudu au kuwaandika katika vitabu vya historia kutokana na jinsi ambavyo walichangia kubadilisha mifumo ya kimaisha dunia. Moja wapo ya watu hawa ni Wezi ambao mimi binafsi napenda kuwaita 'Wezi wa Daraja la kwanza' (First Class Thieves). Hawa wamekuwa toka enzi za kale na wamekuwa wanaushangaza ulimwengu kwa kiwango cha akili walichotumia na uthubutu walionao katika kutekeleza matukio.

Moja wapo kati ya wezi hawa ambao wamechangia kwa kiasi kikubwa kubadilisha mifumo ya kiusalama ni mtu ambaye ameandika historia katika ulimwengu na hususani taifa la ufaransa kwa kutekeleza tukio kubwa zaidi la ujambazi na lenye thamani kubwa zaidi ambayo mpaka leo hii bado hajatokea mtu mwingine katika nchi ya ufaransa aliyefanikiwa kutekeleza tukio kubwa kama hilo na kwa mafanikio. Yeye binafsi hakuiba ili tu apate kutajirika pekee na kuishi maisha ya anasa bali pia aliiba kwa kuwa aliamini huo ndio wito wake (destiny) na aliiba ili kuudhihirishia ulimwengu kuwa anaweza. Jina lake aliitwa Albert Spaggiarri.




May 1976: Nice, Ufaransa


Alfred Spaggiari moja ya watu mashuhuri kwenye jiji la Nice nchini ufaransa na swahiba mkubwa wa Meya wa jiji la Nice Bw. Jacques Medécin, Spaggiari ambaye shughuli zake alikuwa amebobea kwenye upigaji picha za mitindo na matukio muhimu zaidi ya kiserika na binafsi alikuwa ameitisha kikao kilichohudhuriwa na watu wapatao ishirini katika nyumba yake ya mapumziko ya mwisho wa wiki iliyopo nje kidogo ya jiji la Nice. Kikao hicho hakikuhusu upigaji picha au siasa bali aliitisha kikao hicho cha siri na aliwaalika wahalifu kadhaa ili awashirikishe mpango wa siri aliokuwa nao. Kati ya watu hao 20 watu watano walikuwa ni wawakilishi wa ukoo wa Mafia wa usisili ( Sicilian Mafia) aliowaakika kutoka Italia.
Akiwa anafungua kikao hicho Spaggiari aliwaeleza kuwa amewaita hapo ili awashirikishe kwenye tukio la wizi la kihistoria na ambalo anaamini litakuwa na thamani kubwa sana kiasi kwamba hawataitaji kuiba tena maishani mwao ili kuishi maisha ya hali ya juu waliyoyapenda.

Spaggiari akawaeleza kuwa amedhamiria kuiba katika Kuba (vault) ya benki ya Société Générale. Ambayo ndiyo ilikuwa benki kubwa zaidi katika nchi ya ufaransa kwa kipindi hicho na moja ya benki kubwa zaidi duniani.
Lakini kabla hajaendelea zaidi na 'hotuba' yake watu kadhaa waliokuwepo kwenye kikao hicho waliangua kicheko cha dharau na kusema kwamba walidhani kuwa wameitwa kwenye kikao hicho labda 'celebrity' Spaggiari alikuwa ana ugomvi na 'celebrity' mwenzake kwahiyo alitaka awalipe wakamfanyie 'umafia' lakini kamwe hawakutegemea mtu 'mboga saba' kama Spaggiari ati atake kuwashirikisha wao kuhusu tukio la ujambazi kwani wanaamini kuwa Spagiari hajui chochote kuhusu uhalifu wala hajui hata "a e i o u" za matukio ya ujambazi.
Spaggiari aka kaa kimya kwa sekunde kadhaa huku macho yake yakiangaza kwa wahudhuriaji wote wa kikao hicho na macho yake yakakutana na mzee mmoja wa makamo aliyekuwepo pia kwenye kikao hicho ambaye walifahamiana vyema na Spaggiari. Spaggiari akampa ishara kuwa awaeleze watu hao waliohudhuria kikao hicho kuwa yeye ni nani, yeye Spaggiari halisi ni nani, awaeleze kiundani wamfahamu Spaggiari zaidi ya yule wanayemsoma kwenye magazeti, zaidi ya Spaggiari 'mboga saba' wanaye mjua.



UTAMBULISHO MFUPI WA "MPIGA PICHA" ALBERT SPAGGIARI

Albert Spaggiari alizaliwa Desemba 14, 1932 katika mji mdogo wa Hyerés ambapo mama yake alimiliki duka kubwa la mavazi ya ndani ya wanawake (lingerie).
Akiwa bado yuko katika shule ya upili, katika shule yao Spaggiari alitokea kumpenda msichana ambaye alikuwa ni mtoto wa Mkuu wa shule. Mara nyingi Spaggiari alijikuta anaingia kwenye matatizo na walimu kutokana na kumshushia kipigo kijana mmoja wa kisenegali ambaye alipata ufadhili wa kusoma shuleni hapo lakini naye alionyesha hisia za kumpenda binti huyo. Kutokana na Spaggiari kuingia kwenye matatizo mara kwa mara na walimu hakufanikiwa kumaliza shule kwani alifukuzwa baada ya walimu kuchoshwa na tabia zake.

Licha ya kutokuwepo shuleni Spaggiari aliendeleza uhusiano wake na yule mtoto wa Mkuu wa shule
Katika juhudi za Kutaka kumuonyesha huyo binti kwamba yeye sio hoe hae Spaggiari akamuahidi huyo binti kumnunulia pete ya almasi yenye thamani kubwa sana. Uhalisia ni kwamba Spaggiari hakuwa na hela lakini kutoka moyoni alipania kuitekeleza ahadi huyo ili azidi kumfanya mpenzi wake ampende zaidi.

Hivyo basi Spaggiari akamshawishi rafiki yake mmoja kuwa usiku wa siku moja ana mpango wa kuiba pete ya almasi katika duka mojawapo hapo mjini kwao.. Rafiki yake akakubali na wakapanga siku wakatekeleza tukio lakini kwa masikitiko makubwa wakakamatwa.
Baada ya kukamatwa na kushtakiwa mahakamani, Spagiarri alihukumiwa kwenda jela.
Lakini kutokana na umri wake mdogo wa miaka 17, serikaki na Spagiarri wakakubaliana kuwa akajiunge na jeshi badala ya kukaa jela.
Hivyo basi Spaggiarri akajiunga na jeshi kitengo cha wanajeshi wa kutumia parashuti.

Mwaka 1953 Spaggiari alishiriki katika vita ambayo majeshi ya Ufaransa yaliivamia koloni lao la Indochina (Vietnam ya sasa na maeneo yanayoizunguka). Spaggiari alikuwa ni mwanajeshi hodari na aliwahi kujeruhiwa mara mbili katika mapambano na kutokana na uhodari wake alitunukiwa nishani ya heshima.
Lakini ni kana kwamba wizi ulikuwa ndani ya vinasaba vya Spaggiari kwani akiwa huko huko Vietnam na kabla vita haijaisha yeye pamoja na rafiki yake walivamia duka moja mjini Hanoi na baada ya upelelezi walibainika.
Hii ilipelekea Spaggiari kufukuzwa jeshini na kurudishwa ufaransa na kufunguliwa mashtaka na akahukumiwa miaka mitano.

Spaggiarri akatumikia kifungo na mnamo mwaka 1957 akarudi uraiani.
Baada ya kurudi uraiani Spaggiari akajihusisha na kufanya kazi katika viwanda vya kutengeneza makabati ya kuhifadhi vitu vya siri (Safes) na pia akafanikiwa kupata msichana mrembo aliyeitwa Marcelle Audi ambaye kwa kipindi hicho alikuwa anafanya kazi kama Nesi na akafanikiwa kumuoa.
Baada ya kumuoa waliondoka ufaransa na kuelekea nchini Senegal ambapo kwa kipindi hicho bado lilikuwa ni koloni la Ufaransa na wakaishi mjini Dakar. Kwa bahati mbaya hawakufanikiwa kukaa sana Senegal kwani mwaka 1960 Senegal ilipata Uhuru na ikawalazimu warejee tena Ufaransa.

Baada ya kurejea Ufaransa Spaggiarri akaanza kujihusisha na vikundi vya uzalendo vya nchi za ulaya ambavyo vilikuwa vinapinga wazungu kuachia makoloni ya Africa.
Kikundi ambacho kilimvutia sana Spaggiarri kiliitwa OAS (Organisation de al'rmée Secrète). Kikundi hiki kilijihusisha na shughuli za kishushushu kusaidia kushawishi serikali ya ufaransa isiachie koloni la Algeria na pia kilifanya shughuli zake kudhoofisha harakati za watu wa Algeria kudai Uhuru. Spaggiari akajiunga na kikundi hiki mwaka 1961.
Rais wa ufarasa wa kipindi hicho (Rais De Gaulle) mwanzoni alikiunga mkono kikundi hiki lakini kadiri muda ulivyoenda na kuonekana wazi kuwa suala la kuipatia Uhuru Algeria haliepukiki, Rais De Gaulle akakipiga marufuku kikundi cha OAS na vikundi vingine vyote vyenye mlengo huo.

Baada ya harakati zao za OAS kupigwa marufuku Spaggiari akabakia na kinyongo kikubwa sana dhidi ya Rais De Gaulle. Hivyo basi mwaka huo huo wa 1961 akasafiri mpaka nchini Hispania kwenda kuonana na mmoja wa waanzilishi wa kikundi cha OAS mzee aliyeitwa Jenerali Pierre Lagaillarde. Sababu kubwa ya kumfuata ni kwamba Spaggiari alikuwa anahitaji apewe ruhusu ya kumdungua kwa risasi Rais De Gaulle ili kulipiza kisasi kwa "kuwasaliti" OAS na 'raia' wa Ufaransa kwa kuunga mkono Algeria kupewa Uhuru.
Jenerali Pierre akamwambia kuwa ampe 'ramani' yake jinsi alivyopanga ni namna gani atampiga risasi Rais De Gaulle.
Bila kusita Spaggiari akamueleza mpango wake, kuwa msafara wa Rais De Gaulle huwa unapita katika mji mdogo wa Hyerès na huwa wanapita mbele ya duka la mama yake Spaggiari (mama yake Spaggiari alikuwa ni mfanyabiashara wa mavazi ya ndani ya akina mama (langarie)). Hivyo Spaggiari akamueleza Jenerali Pierre kuwa atakaa juu ya paa la duka la mama yake na atakaa na bunduki ya wadunguaji na Msafara wa Rais ukupita atampiga risasi Rais De Guelle.

Jenerali Pierre akakubaliana naye kuwa arudi ufaransa na akatekeleze mpango huo lakini akampa onyo kuwa siku hiyo atayotakaa juu ya paa la duka la mama yake, asifyatue risasi kabla hajapata amri ya moja kwa moja kutoka kwake (direct command). Spaggiari akakubali na kurejea ufaransa.
Siku ya siku ikafika, Spaggiari akakaa juu ya paa la duka la mama yake, msafara wa Rais ukapita mbele ya duka, Spaggiari akasubiri 'direct command' kutoka kwa Jenereli Pierre ili amfyatulie risasi Rais De Guelle, akasubiri na kusubiri, amri haikuja na msafara wa Rais ulitokomea mbali na macho yake.
Wiki chache baadae Spaggiarri akakamatwa na kushtakiwa kwa makosa ya kujihusisha na vikundi vya 'kigaidi'. Spaggiarri akagundua kuwa Jenerali Pierre 'alimuuza'.
Mahakama ikamuhukumu kifungo cha miaka minne jela. Spaggiari akatumikia miaka yote.

Siku ya kutoka jela ni mke wake Audi pekee aliyemkuta nje ya geti la jela akimsubiri waende nyumbani. Spaggiari akamuapia mkewe kuwa hataki tena kujihusisha na harakati zozote wala siasa. Kuanzia sasa kitu pekee anachokitaka ni kuwa mume bora kwake.
Spaggiarri hakuwa anatania, akafungua ofisi yake ya upigaji picha katika jiji la Nice. Akafanya kazi kwa bidii usiku na mchana na ndani ya miaka michache akaibukia kuwa ndiye mpiga picha bora zaidi katika jiji la Nice, na harusi zote za hadhi ya juu ni Spaggiari ndiye alipiga picha, matukio yote muhimu ya kiserikali na binafsi, tenda ya kupiga picha alipewa Spaggiari. Punde si punde Spaggiari akawa moja ya watu mashuhuri zaidi katika jiji la Nice, na akafahamiana na kila mtu muhimu kwenye jiji la Nice. Mpiga picha Spaggiari akawa moja ya raia wanaoheshimika zaidi jijini Nice.
Lakini licha ya mafanikio na heshima yote, kana kwamba uhalifu umeandikwa kwenye vinasaba vyake, roho ya Spaggiari ilitaka zaidi! Sio pesa zaidi, sio umaarufu zaidi, hapana roho ya Spaggiari ilitamani kuiba! Kufanya tukio moja kubwa kuudhihirishia ulimwengu umahiri wake katika wizi.
Roho ya Spaggiari iliwasha kwa kiu ya kutaka kuiba, na alijua bayana roho yake haitotulia mpaka pale atakapo tekeleza walau tukio moja maridadi la wizi. Na ili kujiridhisha Spaggiari akaamua kuwa atafanya tukio la wizi ambalo litasimuliwa vizazi na vizazi.



Turejee kwenye Kikao cha "Mpiga Picha" Spaggiari na wenzake


Baada ya wote waliokuwepo kwenye kikao hicho kusikia historia hiyo ya Spaggiari walishikwa na bumbuwazi. Wote waliduwaa kwani baadhi yao waliwahi kusikia minong'oni mtaani kuwa mpiga picha Spaggiari ni 'mtundu mtundu' lakini hawakutegemea kama huo 'utundu' wake aliwahi kuhusika kwenye maisha ya hatari kama jinsi ambavyo wamesimuliwa kwenye kikao hicho.
Kwa ufupi kwa historia hiyo fupi, Spaggiari alivuna heshima kutoka kwa watu wote ambao walikuwa wamehudhuria kikao hicho lakini swali moja likabaki hewani, je mpango wake ni upi juu ya utekelezaji wa kuiba benki hiyo ya Société Générale, naye Spaggiari akawajibu kuwa hicho ndicho alichowaitia hapo kuwa wakae chini wote watoke na mpango kabambe wa kuiba katika benki hiyo na yeye yuko tayari kusikia mawazo yao kwanza.

Baadhi ya waliokuwepo kwenye kikao kile hasa wale wanachama watano kutoka ukoo wa Mafia wa usisili, wakatoa maoni yao. Wakasema kuwa kama anaweza kuwapa uhakika kuwa katika tarehe fulani mahususi benki hiyo itakuwa na kiwango kikubwa cha fedha basi wao wanaweza wakasaidia wapate silaha na kuweka mpango madhubuti wa kuivamia hiyo bank na kupora hela. Baada ya wanachama hao wa Mafia kutoa maoni hayo Spaggiari akawapa jibu la kuwashangaza sana, kuwa hakubaliani na mkakati huo kwasababu anataka kwamba tukio hilo watakalotekeleza anataka waweke mpango wa kutumia akili zaidi badala ya kutumia mabavu na silaha.

Baada ya maoni hayo kukataliwa wengine nao wakatoa maoni kwamba labda wamteke mtoto au mke wa meneja wa benki kisha watumie kigezo hicho kumshawishi meneja awasaidie kuiba katika benki yake. Wazo hili nalo lilipingwa na Spaggiari na akawaeleza kuwa hataki ukatili wowote utumike katika kutekeleza tukio hili. Mzee mmoja veterani wa kikundi cha OAS ambaye alikuwepo yeye akasema kuwa anatamani afahamu siku ambayo benki yoyote kubwa inakuwa na kiwango kikubwa cha fedha kisha wailipue ili kuikomesha serikali kwa 'kusaliti' kikundi chao cha OAS. Spaggiari akamjibu kwa kifupi tu kuwa kama akitaka afanye tukio lolote kwa ufanisi anatakiwa aweke hisia za chuki pembeni. Hivyo wazo lake hilo la kulipua benki kwa kisasi alikuwa analipinga.

Wale jamaa watano wanachama wa ukoo wa kihalifu wa Mafia, ambao walisafiri kutoka Itali kuja kuhudhuria kikao hicho wakainuka wote kwa pamoja na kumwambia Spaggiari kuwa wanaondoka. Wanahisi kuwa licha ya kuwa ni kweli kama walivyosikia kwenye kikao hicho kuwa amewahi kushiriki katika mipango ya hatari katika maisha yake lakini wanahisi kuwa kwasasa Spaggiari ana ndoto za mchana na hayuko kwenye uhalisia kwasababu kama anakataa maoni yote yaliyotolewa hawaoni uwezekano wowote wa kikao hicho kuzaa mkakati wenye uhalisia wa kutekeleza tukio la ujambazi.
Spaggiari akawasisitiza kuwa wakae chini wasikilize maoni mengine yakiwemo maoni yake lakini wanachama hao wa Mafia wakamwambaia kuwa hawako tayari kuendelea na kikao hicho kwani wanadhani mkakati wowote utakaowekwa hapo utakuwa ni kana kwamba wanaenda kujitoa sadaka kwani haiingii akilini watu muwe na dhamira ya kuiba benki alafu msitumie silaha. Mafia hao wakainuka, wakaaga na kuondoka.

Kwahiyo Spaggiari akabakia na watu 15 pekee kwenye kikao hicho wengi wao wakiwa ni wanachama wa zamani wa kikundi cha OAS. Na alivyowaangalia nyuso zao aligundua dhahiri kuwa ndani ya dakika chache kama hatowapa mpango wowote wa kuwashawishi kuhusu hilo tukio nao wangeweza kuinuka na kuondoka.
Spaggiari akaenda mpaka kwenye kabati la pembeni lililopo kwenye sebule hiyo na kutoka na boksi dogo la saizi ya kati na kulibeba kwa mikono miwili mpaka kwenye meza iliyokuwepo katikati ya sebule na kisha akawaomba wote wainuke na kusogea karibu na meza.
Baada ya wote kusogea karibu na meza Spaggiari akatoa makaratasi kadhaa kutoka kwenye lile box na kayatandaza juu ya meza.

Makaratasi yale yalionyesha ramani na mpango mji wa jiji la Nice. Kuna makaratasi yalionyesha nyumba kwa nyumba na jengo kwa jengo kwa jiji lote la Nice. Makaratasi mengine yalionyesha juu ya mifumo ya barabara ya jiji zima. Makaratasi mengine yalionyesha juu ya mfumo ya maji taka ya jiji zima na hapa katika karatasi hizi za mifumo ya maji taka ndipo hasa Spaggiari aliwataka awaeleze kuhusu mpango wake anao ufikiria. Katika karatasi hiyo inayoonyesha mfumo wa maji taka, Spaggiari akawaonyesha mahali ambapo benki ilipo na akaweka alama kwenye karatasi kisha akawaonyesha mfereji wa maji taka wa chini kwa chini ( Sewer) ambao unapita karibu kabisa na benki hiyo na pia akaweka alama kwenye mfereji huo kisha akawafafanulia zaidi. Akawaeleza kuwa upande ambapo mfereji huo unapita na kupakana na benki ni takribani mita 5 tu kutoka kwenye mfereji mpaka kwenye Kuba (Vault) ya benki. Hivyo basi kama wataweza kuchimba shimo la chini kwa chini (tunnel) lenye urefu wa mita 8 kutoka kwenye mtaro huo wa maji taka kuelekea upande wa benki basi watakuwa wamefika katikati ya sakafu ya vault ya benki ya Société Générale na kitu pekee kitakachobaki ni kutoboa tundu dogo kwa kwenda juu na watakalolitumia kuingilia ndani ya vault kutoka kwenye tunnel walilochimba kutoka mtaroni. Huo ndio ulikuwa mkakati wake.
Spaggiari aliwaangalia nyuso za wale waliokuwepo kwenye hicho kikao na alikuwa na uhakika kuwa wamevutiwa na mkakati huo ingawa walikuwa na maswali kadhaa.

Spaggiari akatoa fursa waulize maswali na swali la kwanza lililokuwepo kwenye vichwa vya wengi lilikuwa je, watakapokuwa chini wanachimba hilo shimo (tunnel) hawatashtukiwa kutokana na makelele na mitetemo watakayo sababisha. Spaggiari akawajibu kuwa japokuwa tunnel la urefu wa mita 8 wanaume kama wao 15 wana uwezo wa kulichimba ndani ya siku hata 3 lakini ili kuzuia kusababisha kelele na mitetemo amepanga kuwa shimo hilo litachimbwa taratibu kana kwamba wanakula chakula kwenye sahani kwa kutumia kijiko. Haijalishi itachukua wiki au miezi mingapi.

Swali lingine lilikuwa je itakuwaje kama vault ina 'sensors' za kuhisi mitetemo au sauti? Spaggiari akawajibu kuwa kuhusu hilo wampe kama siku tatu atafahamu hiyo vault ina 'sensors' zipi na ni namna gani watakavyo jiahami nazo.

Spaggiari akauliza kama kuna swali lingine. Hakukuwa na swali. Kisha akawaukiza, "who is in?" ("Nani atashiriki nami kwenye hili?") wote 15 waliobakia kwenye kikao hicho walikubali kushiriki katika tukio hilo.
Spaggiari akawaeleza kuwa anawapa wiki moja kila mtu akamalize ratiba zake alizokuwa nazo, mwenye familia akaage na kudanganya anavyoweza kwani wakikutana baada ya hiyo wiki moja watakuwa na wiki kadhaa au pengine miezi kadhaa ya kutekeleza tukio hilo ambalo halijawahi kufanyika kabla.
Wakaagana, wakatawanyika.



SPAGGIARI NA GENGE LAKE WANAINGIA 'KAZINI'



Wakati wenzake wakiwa wamerudi makwao kuaga familia zao ili warejee baada ya wiki moja kwa ajili ya 'kazi', yeye Spaggiari kesho yake alifika mpaka kwenye benki ya Société Générale na akaomba kuwa mteja afunguliwe sanduki jipya kwa ajili ya kuhifadhi vitu vyake vya faragha/siri ( safe deposit box) katika vault. Baada ya kukamilisha taratibu zote za kujaza nyaraka za maandishi na kulipia gharama za huduma hiyo hatimaye akapelekwa na muhudumu wa benki mpaka kwenye vault na kuonyeshwa kisanduku ambacho kitakuwa chake. Kisha muhudumu akatoka nje ya mlango ili kumpa faragha Spaggiari ahifadhi vitu vyake. Baada ya kuachwa peke yake Spaggiari akatoa saa kubwa ya muito (alarm clock) ambayo ilikuwa kwenye kibegi kidogo alichokuja nacho. Saa hii ilikuwa na ukubwa wa kufanana kabisa na saa kubwa ya ukutani. Lakini ilikuwa nzito zaidi. Na ilitengenezwa kuwa saa ya muito ambayo muda uliotegeshwa ukifika Saa inaita na kutetema (vibration). Spaggiari akaitegesha saa hiyo iwe inaita usiku wa manane. Kisha akaiweka kwenye kisanduku chake alichoonyeshwa. Kisha akakifunga kisanduku, akatoka nje akakabidhi funguo ya kisanduku kwa muhudumu na kurudi nyumbani.

Baada ya wiki moja kupita na wenzake kurudi kwa ajili yakuanza kazi, kwanza kabisa Spaggiari akawapa muhtasari juu ya alichofanikisha mpaka mda huo. Akawaeleza kuwa hawahitaji kuhofu kuhusu 'sensor' za mitetemo au sauti kwakuwa ameng'amua kuwa vault hiyo haina 'sensor' zozote zile. Walipo muuliza amejuaje, akawaeleza kuhusu Saa ya muito aliyoiweka kwenye hiyo vault na kuitegesha iwe inaita muda wa usiku. Na akawaeleza kuwa kwa siku kadhaa amekuwa akichunguza na hajaona taharuki yoyote kutoka kwa walinzi au alarm za ulinzi za benki zikilia hivyo ana uhakika kabisa hakuna 'sensors' zozote kwenye hiyo vault.

Spaggiari alikuwa sahihi kabisa kwani vault hiyo ni kweli haikuwa na sensor zozote, wenyewe wenye benki waliamini kuwa vault hiyo ilikuwa haiingiliki kwa namna yoyote (utterly impregnable) kwasababu mlango wake wa chuma ulikuwa mnene zaidi ya kuta tatu za nyumba ya tofali zikiunganishwa pamoja na mtu alihitajika kuingiza namba maalumu (combination) na kutumia funguo kubwa mbili maalumu ili aweze kuufungua. Pia kuta za hiyo vault zilikuwa haiwezekani hata mtu kuzigusa akiwa nje kwani vault ilikuwa kati kati ya jengo la benki na kuta zake zilikuwa nene kiasi kwamba zinazidi hata unene wa kuta tatu za nyumba ya kawaida.

Baada ya Spaggiari kuwapa wenzake muhtasari huo, kawaeleza kuwa hivyo basi saa hiyo ya muito watakuwa wanaitumia kama muongozo wa ziada ili wawe wanachimba kwa usahihi zaidi kuekekea chini ya sakafu ya vault (pinpointing). Baada ya kupeana muhtasari, Spaggiari akaondoka na wenzake ili akawaonyeshe eneo la kazi.

Walitumia boti ndogo kusafiri katika mto Rivera mpaka mahali ambapo kiwango kidogo cha maji ya mto yanachepuka na kuingia katika mtaro mkubwa wa maji taka unaokusanya maji na kupita karibu na benki waliyotaka kuiba. Walipofika hapa walitumia maboya kuelea juu ya maji machafu ya mtaro yaliyojaa kinyesi cha binadamu na uchafu mwingine, walielea kuelekea mbele kwa takribani dakika ishirini wakiwa na ramani zao mikononi mpaka walipofika sehemu waliyoihitaji.

Baada ya kufika hapo Spaggiari akawapa maelekezo kuwa wanatakiwa wachimbe moja kwa moja bila kupindisha hata kidogo kwenda mita 8 ndani na kama watakuwa sahihi baada ya kufikisha mita 8 hizo alarm aliyoiweka kwenye vault ikilia basi wataisikia juu ya vichwa vyao, ikimaanisha kwamba wako chini ya sakafu ya vault.
Pia Spaggiari akawagawanya wenzake kwenye shift za kufanya kazi. Akawaambia kuwa kutakuwa na makundi mawili, kila kundi litafanya kazi kwa masaa kumi wakati huo wengine watakuwa wamelala na akawasisitiza kuwa ni lazima walale kwa masaa kumi. Kwahiyo shifti zilikuwa mbili, masaa kumi kazini na masaa kumi kulala. Pia akawakataza wasiguse kabisa pombe au kahawa kwa muda wote ambao watakuwa wanafanya hiyo kazi.

Siku iliyofuata kazi ilianza. Kazi ilifanyika bila papara, taratibu na kwa umakini mkubwa. Kazi ikaendelea kwa siku kadhaa, wiki kadhaa na baada ya miezi miwili hatimae walifikisha tanuru (tunnel) la urefu wa mita 8. Baada ya kufikisha umbali huo Spaggiari akawaambia wasubiri usiku wa manane kusikiliza saa ya muito ili wajue kama wako sahihi au la. Ilipofika usiku wa manane alarm ya saa iliyowekwa kwenye vault na Spaggiari iliita, na waliisikia juu ya vichwa vyao kabisa. Wakapongezana kwani sasa walikuwa na uhakika asilimia mia moja kuwa wako sahihi, walikuwa wako chini ya sakafu ya vault na kilichobakia ilikuwa ni kutoboa hiyo sakafu na kuchukua 'mwali wao'.
Spaggiari akawaambia wenzake kuwa inabidi wapumzike kwa siku mbili kuisubiria Bestille Day ndipo watoboe sakafu na kuchukua mwali wao.

Bastille Day (siku ya Uhuru wa Ufaransa) ambayo husheherekewa kila mwaka tarehe 14 July na kwa mwaka huu 1976 ilikuwa inaangukia siku ya alhamisi, hivyo hii ilifanya kuwe na siku nne za mapumziko (alhamisi na ijumaa (sherehe za Bastille Day) Jumamosi na jumapili (mapumziko ya mwisho wa juma)). Kwahiyo Spaggiari alitaka wapate muda wa kutosha kwa siku nne ili wachukue fedha na vitu vingi kadiri wawezavyo.

Hatimaye alhamisi ikawadia na Spaggiari na genge lake wakamalizia kutoboa sakafu ya vault na kuingia ndani. Jambo la kwanza walilolifanya baada kufanikiwa kuingia ndani ya vault ni kuchomelea mlango wa vault kwa ndani ili mtu aliyepo nje asiweze kuufungua.
Kazi ikaanza na Spaggiari kwa kutumia uzoefu aliokuwa nao wa kufanya kazi kwenye viwanda vya kutengeneza 'safes' akawaongoza wenzake katika zoezi la kufungua visanduku. Kazi ilifanyika mchana na usiku kwa siku ya kwanza ya alhamisi na kesho yake siku ya Ijumaa Spaggiari akawaambia wenzake wapumzike kwa masaa machache ili nao washerehekee sikukuu ya Bastille kama wenzao walioko huko mitaani. Hivyo basi Spaggiari akatoka kwenye vault na kurudi mtaani kununua mvinyo pamoja na vyakula vya anasa na kurudi navyo kwenye vault kwa ajili ya kusheherekea. Baada ya kumaliza kula na kunywa kazi iliendelea usiku na mchana siku hiyo ya ijumaa, jumamosi na ilipofika jumapili mchana walikuwa wamefanikiwa kufungua yapata visanduku 400 vilivyokuwa na fedha taslimu, vito vya thamani, hati fungani na vitu vinginevyo vya thamani kubwa. Inakadiriwa kuwa thamani ya 'mzigo' wote ambao Spaggiari na genge lake walipata unafikia Faranga Milioni 60 za ufaransa (60 million French Frans).

Ilipofika muda wa mchana siku ya Jumapili mvua ilianza kunyesha na Spaggiari akahisi mitaro waliyotumia kuingilia inaweza kujaa maji na hivyo kufanya zoezi la kutoka kuwa gumu hivyo basi akawaamuru wenzake waondoke kabla mvua haijawa kubwa. Lakini kabla hawaondoka aliwaambia wenzake kuwa anahitaji kufanya jambo moja la muhimu la mwisho. Huku akionekana akiwa na hisia na msisimko wa hali ya juu, spaggiari alichukua kopo la rangi alilokuwa amekuja nalo pamoja na brashi ndogo ya kapakia rangi, kisha akausogelea ukuta mmoja ndani ya vault na kuandika maandishi makubwa yaliyo someka; "SANS ARMES, NI HAINE, NI VIOLENCE" ("Without weapons, nor hatred, nor violence" ("Pasipo silaha, wala chuki, wala ukatili")).
Hiyo ndio 'falsafa' aliyotaka kuifikisha kwa ulimwengu mzima kujitambulisha yeye ni 'mwizi daraja la kwanza' wa dizaini gani.
Baada ya hapo wakafungasha mizigo yao, wakatokomea.


'Maisha' Baada ya Tukio..

Siku ya jumatatu benki ya Société Générale ilifunguliwa na shughuli ziliendelea kama kawaida pasipo yeyote kung'amua kuwa kuna jambo lilitokea ndani ya vault. Na kama ilivyo ada ilipofika majira saa Tatu na nusu asubuhi wafanyakazi wawili walielekea kwenye chumba cha Vault kukifungua ili kuruhusu wateja kuhifadhi vitu na wengine kuchukua vitu walivyohifadhi. Walipofika mlangoni wakaingiza namba maalumu na kisha kama ilivyo utaratibu wakaingiza funguo mbili katika matundu mawili juu ya mlango na kuzungusha funguo lakini jambo la ajabu mlango haukufunguka. Walihangaika kuzungusha funguo karibia nusu saa lakini mlango haukufunguka.

Baada ya juhudi zote hizo bila mafanikio wakaamua watoe taarifa kwa meneja msaidizi wa benki aliyeitwa Pierre Bigou. Bw. Pierre baada na yeye kuhakikisha kuwa mlango ulikuwa haufunguki ikabidi aagize aitwe muhunzi ili aje kuwasaidia. Dakika chache baadae muhunzi alifika na akaanza kuukagua mlango, na ndani ya dakika kumi na tano akawa ameng'amua kuwa mlango umechomelewa kwa ndani na hakuna namna ambayo wanaweza kuufungua wakiwa nje.

Sehemu ya mapokezi baadhi ya wateja walikuja kwa ajili ya kutumia visanduku vyao vya kwenye vault walianza kupaniki na ilimbidi meneja mwenyewe wa benki ahusike kuwatuliza na kuwaondoa wasiwasi. Meneja alitumia maarifa yake yote ya huduma kwa wateja kuwaondoa hofu wateja wake na kuwataka wawe watulivu, " Nothing to worry about monsieur. A minor technical problem madame. Your valuables are quite safe but there may be a slight delay" ("ondoa hofu muheshimiwa. Ni tatizo dogo tu la kiufundi. Vitu vyenu viko salama ila itachukua muda kidogo kurekebisha.") Meneja wa benki Bw. Jacques Guenet alisikika akiwatuliza wateja wake.

Baada ya muhunzi kugundua kuwa mlango huo hautaweza kufunguka kwa nje akapendekeza kuwa watoboe ukuta ili kuingia ndani. Viongozi wa benki wakakubali na kazi kutoboa ukuta ikaanza. Kutokana na unene wa ukuta na kutoboa kwa makini ili wasisababishe hasara nyingine, ilichukua takribani masaa matatu kutoboa tundu kubwa kiasi la kumuwezesha mtu kupita. Yule muhunzi ndiye alikuwa mtu wa kwanza kuchungulia ndani na alipochungulia alipatwa na mshangao kana kwamba amepoteza fahamu kwa sekunde kadhaa. Hakuamini alichokuwa anakiona ndani ya vault. Huku bado akiwa na mshangao alimgeukia Meneja wa Benki aliyekuwa amesimama nyuma yake na kumwambia kwa mshangao, "Merde de putain" ("you have been robbed" ("Mmeibiwa")).

Baada ya wote bumbuwazi kuwaisha kutokana na kutoamini macho yao walichokuwa wanakiona mbele ya macho yao, hatimae wakapiga simu polisi na haraka sana polisi wakawasili. Baada ya Polisi kuwasili na kuingia ndani ya vault nao pia hawakuamini kile walichokuwa wanakiona mbele ya macho yao. Wote kwa pamoja macho yao yaliganda kwenye Ujumbe ulioandikwa kwenye ukuta, "sans armes, ni haine, ni violence" (Pasipo silaha, chuki wala ukatili).



KUKAMATWA, KUSHTAKIWA NA KUWA 'HURU' TENA

Ndani ya miezi miwili polisi walifanikiwa kugundua kuwa Spaggiari ndiye muhusika mkuu wa tukio lile. Haijulikana hasa ni namna gani polisi walifanikiwa kugundua kuwa Spaggiari ndiye alikuwa 'mastermind' wa tukio lile, kwani kumekuwa na maelezo mengi sana yanayokinzana lakini angalau ufafanuzi unaoonyesha uhalisia kidogo ni kwamba mmoja wapo wa watu walioshiriki tukio lile alipopewa mgao wake wa fedha pia alipewa na miche kadhaa ya dhahabu (gold bars) na bila kutumia akili au kuwa na subira akauza mche mmoja ndani ya wiki chache baada ya tukio. Baada ya siku kadhaa mtu aliyeununua mche huo aliripoti polisi kuwa ameuziwa mche wa dhahabu unaofanana kabisa na moja ya miche inayoripotiwa kuwa imeibiwa kwenye vault ya benki ya Société Générale.
Polisi wakamfatilia huyo mtu na wakafanikiwa kumtia nguvuni na baada ya kumuhoji kwa siku kadhaa akawataja wenzake wote akiwemo Albert Spaggiari.

Polisi waliposikia kuwa Spaggiari ndiye alikuwa kiongozi wa tukio hilo, walishikwa na butwaa kwani Spaggiari alikuwa ni moja ya watu mashuhuri na anayeheshimika zaidi jijini Nice. Na kipindi wanapata taarifa hii alikuwa yuko safarini mashariki ya mbali akiwa amemsindikiza rafiki yake Meya wa jiji Bw. Jacques Médecin, katika ziara ya kiserikali.

Siku ambayo Meya na Spaggiari wanarejea Nice kutoka mashariki ya mbali, Spaggiari alikamatwa hapo hapo uwanja wa ndege na kufunguliwa mashtaka ya kuhusika kupanga na kushiriki tukio la ujambazi katika benki ya Société Générale.

Kesi hii ilitikisa vyombo vya habati ulimwengu mzima na umaarufu wa Spaggiari ukaongezeka maradufu na mwenyewe alionekana kufurahia haswa jinsi alivyokuwa anazungumziwa kila kona ya Dunia.

Wakati kesi ikiwa inaendelea Spaggiari akatunga hadithi ambayo kwa bahati mbaya Jaji aliyekuwa anasikiliza kesi hiyo aliiamini na akawa anatamani kujua kiundani. Spaggiari aliwaeleza kuwa alifanya tukio hilo ili kukiwezesha kiuchumi kikundi cha siri cha wazalendo kilichoitwa 'Catena' (neno la kifaransa linalomaanisha 'Chain' (mnyororo)).

Spaggiari akawaeleza kuwa hayuko tayari kuwapa taarifa za kikundi hicho Polisi kwani hawaamini bali yuko tayari kutoa taarifa kwa Jaji huyo peke yake. Hivyo basi ikawekwa ratiba maalumu ambayo Spaggiari alikuwa anapelekwa ofisini kwa Jaji na kila walipokutana alikuwa anampa kikaratasi alichokiandika kwa mafumbo (coded message) na ilikuwa inamlazimu Jaji akune kichwa haswa ili kung'amua kilichoandikwa na Spaggiari kuhusu siri za hicho kikundi cha 'Catena'.

Katika moja ya vikao vyao na Jaji, Jaji akiwa 'bize' kung'amua Ujumbe huo wa mafumbo Spaggiari aliinuka kutoka kwenye kiti kana kwamba anataka kumkaribia Jaji ili ampe ufafanuzi. Lakini jambo la ajabu alikimbia kwa spidi ya ajabu mpaka dirishani na kujirusha nje kwa uhodari wa hali ya juu (kumbuka aliwahi kuwa mwanajeshi kitengo cha Parashuti). Ofisi ya Jaji ilikuwa juu ghorofa ya Tatu katika hilo Jengo la mahakama, lakini kutokana na Spaggiari kujirusha kwa uhodari alitua chini juu ya paa la gari bila kudhurika. Kisha akakimbia kuvuka barabara na kulikuwa na piki piki inamsubiri.

Baada ya kukwea juu pikipiki akageuka kuwaangalia juu dirishani maaskari pamoja na Jaji waliokuwa wanachungulia wakiwa hawaamini kilichotokea ndani ya sekunde chache. Spaggiari akapayuka kwa nguvu "Au revoir" (kwaherini). Kisha akatabasamu kwa dharau na inasemekana akawaonesha kidole cha kati. Kisha kwa mwendo wa kasi na uhodari pikipiki ikapotea mbele ya upeo wa macho yao. Hiyo ndio ilikuwa mara ya mwisho kwa mamlaka za serikali za ufaransa kumuona Spaggiari.

Wiki mbili baadae mtu mwenye gari ambalo Spaggiari alitua alipo ruka kutoka ghorofani alipokea cheki ya thamani ya faranga 5,000 pamoja na kikaratasi kikisema ni kwaajili ya matengenezo ya paa la gari lake.
Pia kuna tetesi ambazo zimeenea mno toka kipindi hicho mpaka sasa kuwa mtu aliyempakia Spaggiari kwenye pikipiki na kumtorosha alikuwa Christian Estrosi bingwa wa Dunia wa mbio za pikipiki ambaye baadae alikuja kuwa waziri katika serikali ya Ufaransa.

Baada ya kutoroka Spaggiari alielekea nchini Argentina na kuishi huko na kufanyiwa upasuaji wa kubadilisha muonekano (plastic surgery). Inasemekana Spaggiari alikuwa anarudi mara kwa mara nchini Ufaransa kumuona mkewe Audi na Mama yake.

Akiwa nchini Argentia inasemekana kuwa alikuwa karibu sana na CIA akiwasaidia kufanikisha shughuli ambazo CIA hawakutaka kujihusisha nazo moja kwa moja kwa kuhofia jina la idara yao kuchafuka ikitokea siri kuvuja.
Mfano mzuri ni jinsi ambavyo Spaggiari (au daniel jina walilotumia CIA kumtambua (code name)) alishirikiana na Michael Townley afisa wa DINA (kitengo cha ushushushu cha nchi ya Chile) kuchora mchoro na kulipua gari la balozi wa Chile nchini Marekani.

Skandali hii ilichangia kwa kiasi kikubwa kuzorotesha mahusiano ya kidiplomasia kati ya marekani na Chile na hakuna aliyejua uhusika wa CIA mpaka pale mwaka 2000 ambapo CIA waliweka hadharani nyaraka kadhaa za siri baada mda wake wa usiri kupita.

Albert Spaggiari alifariki June 8, 1989 kwa kansa ya koo kutokana na matumizi ya sigara.
Fedha, Vito vya thamani, hati fungani na nyaraka nyingine za siri zilizoibwa na Albert Spagiari na Genge lake havijapatika mpaka leo hii. Tukio hili limebakia katika vichwa vya Wafaransa kama tukio kubwa pekee la wizi wa vitu vya thamani ya juu zaidi na lililotekelezwa kwa umaridadi na akili nyingi au kama Spaggiari mwenyewe alivyolielezea; "Sans armes, ni haine, ni violence" (Pasipo silaha, chuki wala ukatili").

-